Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20220329-065607_Opera%20Mini.jpg
 
RONALDO KUKOSA MKWANJA WA BONASI
.
Nyota wa Manchester United, Cristiano Ronaldo atakosa mkwanja wa bonasi kama watamaliza msimu huu wa 2021-2022 bila ya taji lolote.
.
Ronaldo alirejea Old Trafford katika dirisha la majira ya kiangazi mwaka jana huku mkataba wake ukiwa na makubaliano ya bonasi atakayopewa mbali na mshahara wake wa Pauni 480,000 anaoingiza kila wiki.
.
Endapo Man United ingetinga fainali ya Ligi Mabingwa Ulaya itakayofanyika Mei jijini Paris basi nyota huyo wa Kimataifa wa Ureno angepata bonasi ya Pauni 2.5 milioni (Sh 7.6 Bilioni) lakini sasa imekula kwake. Ronaldo ameweka rekodi mbovu katika historia ya soka lake ya kukosa mataji yote.
Screenshot_20220329-072545_Instagram.jpg
 
LA PULGA AFIKIRIA KUTUNDIKA DARUGA ARGENTINA
.
Lionel Messi huenda akastaafu kuchezea timu ya taifa ya Argentina baada ya fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika Qatar Novemba mwaka huu.
.
“Bado sijafahamu baada ya Kombe la Dunia nitafanya nini, sijafahamu kitakachofuata. Lolote linaweza kutokea. Nitajaribu kuchambua kwani mambo ni mengi kabla ya kufanya uamuzi wowote,” amesema Messi.
Screenshot_20220329-072927_Instagram.jpg
 
SUREBOY AMPA KIBURI NABI
.
“Tunaendelea kufurahia ubora wa viungo wetu ambao kiukweli wamekuwa wakifanya kazi nzuri mpaka sasa. Katika mechi zetu kuna wakati tunaweza kumkosa mmoja, lakini bado unaona timu ipo katika kiwango cha ubora,”
.
“Unaweza kuangalia tumemkosa Aucho, ila kuna Sure Boy amekuwa na kazi bora tangu ameingia katika timu. Amekuwa na kitu kikubwa anapocheza na Bangala, Feisal au Mauya. Hiki ni kitu kizuri kwa mustakabali wa timu katika eneo hilo.”
Screenshot_20220329-075456_Instagram.jpg
 
“Erik Ten Haag anapaswa kwenda kufundisha klabu ya mpira na sio klabu ya biashara, Manchester United ni klabu ya biashara hakuna Kocha atafanikiwa kwasasa” Louis Van Gaal
Screenshot_20220329-075716_Instagram.jpg
 
“Virgil Van Djik ana bahati kucheza EPL ambayo haina Drogba, Lampard, Tevez, Rooney, Shearer wala Thierry Henry ndio maana ni rahisi wao kusema yeye ni beki bora” Michael Ballack

Kuna ukweli ndani yake??____
Screenshot_20220329-075847_Instagram.jpg
 
Mmiliki wa zamani wa Chelsea, Roman Abramovich aliwahi kukaa jukwaa moja na mashabiki liitwalo Shed End, akiitazama Chelsea ikicheza huku akishangilia kwa mzuka kama Mashabiki wengine

Screenshot_20220329-080001_Instagram.jpg
 
Mmiliki wa zamani wa Chelsea, Roman Abramovich na maafisa wengine watatu waliokuwa kwenye ujumbe wa amani kati ya Urusi na Ukraine inasemekana walipata hitilafu ya kiafya kutokana na sumu

Inaaminika kati ya Machi 3-4 mwaka huu, ujumbe huo ulipitia maumivu makali ya macho na ngozi, ila kwasasa hali zao zinaendelea vyema baada ya matibabu

Bado haijajulikana nani wahusika kwakuwa wajumbe wa pande zote mbili walipata changamoto hiyo

Chanzo: SKY SPORTS ]
Screenshot_20220329-080209_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom