Makapuku Forum

Makapuku Forum

Askari wa Jeshi la Polisi Kituo Kikuu cha Kati Mbeya mwenye namba E 9073 Novatus Peter Kalambo(48) amejinyonga kwa kutumia mkanda wa suruali nyumbani kwake mtaa wa Mwambene Kata ya Mwakibete Jijini Mbeya.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ulrich Matei amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kubainisha kuwa askari huyo alijinyonga chumbani kwake kwa kutumia mkanda majira ya ya saa 11 jioni machi 15,2022 "Askari huyo alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya moyo, hadi umauti unamkuta alikuwa kwenye mapumziko ya ugonjwa"

Matei ametoa rai kwa Askari na Wananchi kutokata tamaa pindi wanapokumbwa na maradhi.

Marehemu ameacha Mke na Watoto watatu na taratibu za kusafirisha mwili kwenda Sumbawanga Rukwa zinaendelea.
Screenshot_20220316-203730_Instagram.jpg
 
"Mwaka mmoja wa Mama Hassan hili ni kubwa kuliko, Serikali imekamilisha mchoro wa Arts and Sports Arena itakayochukua Watu takribani 15,000, Mheshimiwa Mohammed Mchengerwa (Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo) mkutano na Wanahabari Dodoma leo, huu ni mchoro wa Arena ya Dodoma yenye umbo la ngoma ya kiafrika, tunakwenda hatua ya pili sasa, ujenzi" ——— aandika Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Tanzania Dr. Hassan Abbas
Screenshot_20220316-204020_Instagram.jpg
 
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Adam Malima ametembelea eneo kulikotokea ajali jana usiku Wilayani Handeni mkoani Tanga na kuua Watu wanne.

RC Malima amezungumza na baadhi ya walioshuhudia ajali hiyo ambao wamemueleza kwamba ilitokea baada ya Toyota Coaster ikiwa na abiria ikitokea Korogwe kuelekea Handeni kugonga baadhi ya Wananchi waliokuwa wakisaidia kuziba pancha kwenye hiace iyokuwa imeegeshwa pembeni ya barabara.

"Hiace ilikuwa imepasuka tairi na kulikuwa na Wanakijiji wanasaidia kubadilisha tairi, wakati coaster inakuja akawa anaelekezwa asimame lakini kwasababu haikuwa na taa ikagonga wale wanakijiji waliokuwa wanasaidia na kuanguka huko bondeni, kwa hiyo waliopata ajali wengi ni Wananchi” shuhuda

RC ameongozana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Safia Jongo ambapo Majeruhi wa ajali hiyo wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Handeni wakiendelea na matibabu.
Screenshot_20220316-204211_Instagram.jpg
 
Huku Uingereza ikiendelea kujaribu kulifanya taifa hilo kutovuta sigara ifikapo mwisho wa muongo huu, Ripoti mpya imeeleza kwamba huenda hatua inayofuata ni kupiga marufuku Watu walio na umri wa chini ya miaka 25 kununua sigara.

Kama ilivyoripotiwa na gazeti la The Times katika siku za hivi karibuni, New Zealand imeanzisha marufuku ya mwaka baada ya mwaka ambayo inazuia Mtu yeyote aliyezaliwa baada ya mwaka 2008 kununua sigara au tumbaku katika maisha yake na pia sasa hivi kuna hoja ya kuongeza umri halali wa uvutaji sigara nchini Uingereza hadi 19, 20, 21, au hata 25.
Screenshot_20220316-204321_Instagram.jpg
 
Ikiwa ni miaka 25 sasa toka Bondia Mike Tyson kung’ata sikio la Bondia Evander Holyfield mwaka 1997 wakati wa pambano la ngumi, kampuni ya Tyson inazindua pipi za bangi, zenye umbo la sikio zinazoitwa "Mike Bites."

Kampuni ya Bangi ya Mike Tyson ilitangaza habari hiyo kupitia mtandao wa Twitter siku ya Jumanne tarehe 15 March ikisema kwamba pipi hizo zitauzwa katika zahanati za miji ya Massachusetts, California na Nevada nchini Marekani.

Tyson amekubaliana na idea hii ya pipi za bangi na kuandika “Masikio haya kwa kweli yana ladha nzuri”

Baba wawili Nigendako kuna ujumbe wako huku
Screenshot_20220316-204444_Instagram.jpg
 
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe leo Jumatano Machi 16, 2022 ameongoza kikao cha kamati kuu ya chama hicho baada ya kutoka gerezani alikokaa kwa miezi nane.

Machi 4, 2022 Mbowe na wenzake watatu walitoka gerezani baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kuwasilisha hati ya kutokuwa na nia ya kuendelea na kesi iliyokuwa imefunguliwa dhidi yake na wenzake watatu katika Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi jijini Dar es Salaam.

Kikao hicho kiliendelea jijini Dar es Salaam ambapo wajumbe na viongozi waandamizi wa chama hicho wanashiriki na baadhi ya wajumbe akiwamo Tundu Lissu, Godbless Lema wakishiriki kwa njia ya mtandao.
Screenshot_20220316-204658_Instagram.jpg
 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula amepokea nakala ya Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Malawi nchini, Andrew Kumwenda leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Baada ya kupokea nakala ya hati hizo Balozi Mulamula amemuahidi Balozi mteule ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake ya kibalozi wakati wote atakaokuwepo nchini.

“Leo nimepokea nakala ya hati za utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Malawi na tumefarijika kwa Mhe. Rais Chakwera kumteua Balozi huyu mara baada ya Balozi wa awali kumaliza muda wake wa uwakilishi, hii ni ishara ya
uhusiano wa karibu, undugu na urafiki uliopo baina ya Tanzania na Malawi,” amesema Balozi Mulamula

Kwa upande wake Balozi Mteule wa Malawi, Andrew Kumwenda amesema kuwa Malawi na Tanzania siku zote zimekuwa na uhusiano mzuri wa kidiplomasia na jukumu lake kama Balozi ni kuhakikisha uhusiano huu unazidi kuimarika.
Screenshot_20220316-204837_Instagram.jpg
 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Damas Ndumbaro amefanya mazungumzo na Uongozi wa juu wa Shirika la ndege la Umoja wa Falme za Kiarabu la Emirates kwa lengo la kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo Tanzania ambapo vitaweza kuonwa na abiria wapatao milioni 90.2 wanaosafiri kila mwaka kupitia ndege za shirika hilo.

Pia, vivutio hivyo vya utalii vya Tanzania vitakuwa vikitazamwa na mamilioni ya abiria wa Shirika hilo wakati ndege zitakapokuwa zikiruka (takeoff) katika viwanja mbalimbali duniani.

Waziri Ndumbaro amebainisha alipokutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa Shirika hilo Dubai ambalo mbali na kusafirisha abiria milioni 90.2 duniani kote pia husafirisha abiria wapatao milioni 20 ambao huunganisha ndege nyingine.

Katika hatua nyingine, Dk Ndumbaro amesema katika mazungumzo hayo wamekubaliana ziandaliwe makala tano (Documentaries) za kuelezea vivutio vya utalii vya Tanzania ikiwemo Zanzibar, Serengeti, Ngorongoro pamoja na Mlima Kilimanjaro.

'' Shirila la ndege la Emirates ni Shirika kubwa sana Duniani lengo letu kama nchi ni kuhakikisha abiria wapatao milioni 90.2 wanaviangalia vivutio vyetu kisha wanavipenda halafu wanatembelea Tanzania'' amesisitiza Dk Ndumbaro.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Masoko wa Afrika wa Shirika la ndege la Umoja wa Falme za Kiarabu la Emirates, Badr Abbas amesema Shirika la Emirate lipo tayari kufanya kazi na Tanzania katika kuhakikisha vivutio vya utalii vya Tanzania vinajulikana.
Screenshot_20220316-205030_Instagram.jpg
 
CAF imelitangaza bao la Pape Sakho wa Simba alilofunga dhidi ya RS Berkane kwenye uwanja wa Mkapa Dar limekuwa bora la wiki kwenye Kombe la Shirikisho Afrika ikiwa ni mara ya pili baada ya lile alilofunga dhidi ya Asec Mimosas kuwa bao bora la wiki katika michuano hiyo.
Screenshot_20220316-205235_Instagram.jpg
 
KOCHA wa timu ya Taifa Tanzania, Kim Poulsen amemtaka mchezaji wake Simon Msuva kumaliza utata wake na klabu yake ya Wydad Casablanca ili arejee uwanjani.

Msuva yupo nje ya uwanja baada ya kuwa na mvutano na klabu yake hali iliyomfanya arudi nchini na kuendelea kujifua kivyake.

Akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya kumita mchezaji huyo kwenye kikosi chake, Poulsen alisema anafahamu Msuva yupo nchini na mara kwa mara anazungumza nae kuona namna gani anamsaidia.

“Mara kwa mara huwa nazungumza nae na nimemuambia kabisa ahakilishe anamaliza suala lake na timu yake kwa sababu anatakiwa acheze kwa haraka” alisema Kim.
Screenshot_20220316-205516_Instagram.jpg
 
Baada ya kichapo cha bao 1-0 ilichopata Manchester United dhidi ya Atletico Madrid Cristiano Ronaldo anaungana na Lionel Messi ambaye timu yake ilitolewa wiki iliyopita kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya. Nani utamisi zaidi shoo zake kwenye UEFA msimu huu?
Screenshot_20220316-205628_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom