Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20220316-214303_Instagram.jpg
 
Shirikisho la soka la Ghana limesema sababu ya kuchelewa kutaja majina ya wachezaji walioitwa timu ya taifa kuelekea mchezo wa kufuzu kombe la dunia ni kuepusha kelele mitandaoni ambazo huwa zinaathiri mpaka viwango vya wachezaji
Screenshot_20220316-214520_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

SIMBA NA HADITHI YA KUNUNUA UKWELI

Wakati Barcelona ipo kwenye kiwango bora sana chini ya Pep Guardiola, Media zote duniani ilisifia sana na kupongeza soka lile, hakuna sehemu ambapo Barcelona ilikuwa haitajwi

Wakati Manchester United ama The Famous United ipo katika ubora mkubwa wa Class of 92 kila Mtu aliipa sifa, kila Media iliitaja United lakini ni tofauti na sasa

Wakati Yanga ya Kampa Kampa tena ipo kwenye ubora wake chini ya Yusuph Manji kila Mtu aliisifia, Media zilicover sana story za Yanga na nchi iliimba Yanga, kutokana na ubora

Sasa hivi kwa zaidi ya miaka mitano, Tanzania na Afrika inaitaja Simba sio media za ndani tu mpaka nje na CAF wanatoa mileage ya kutosha sana, kwa zaidi ya misimu minne hivi sasa

Tafsiri yake ni kuwa unapewa sifa au pongezi sio kishkaji bali kwakuwa kuna kazi umefanya, ukiharibu Media hazitobaki, ni mpaka urejee tena kileleni watu watakupa sifa zako

Kuna wakati unaweza kuhisi Simba inatajwa sana! Lakini je haistahili? Kuna wakati unahisi wachezaji wa Simba wanatajwa sana je hawastahili?

Bingwa wa Tanzania bara kwa misimu minne ni Simba, huyo Simba ndie anapeperusha bendera ya Tanzania kwa misimu mitano hivi sasa, unahisi ni sifa za kubumba?? Jibu ni HAPANA

Huyu Pape Ousman Sakho kusifiwa ni kosa?? Top quality goals kuanzia CCM Kirumba mpaka Taifa, kuanzia FA mpaka Shirikisho Afrika! Unahisi Media Zinakosea?

Mfano tu nikikaa redioni kuongea wakati Sakho kafunga mbili Afrika, kisha Mshikaji wangu huko Ifakara kafunga nne kombe la Mbuzi, nikitulia na stori ya nyumbani Ifakara kwa dakika 10 utanielewa?

Media hazijawahi kumkataa Mtu, timu wala Taasisi! Ila uhalisia upo field, ukifanya vizuri unazungumzika kirahisi mnooo!

Mwanafalsafa mmoja aliwahi kusema “We dont cover by favour but we cover on MERIT”

Ukiwa kwenye ubora wako hata ukigusa jiwe litakuwa mkate
Screenshot_20220316-214849_Instagram.jpg
 
Farhan jr

LIONEL MESSI NA ANTONELA, MAANA NYINGINE YA MAPENZI - PART 1

Love doesnt asky why! Waliwahi kusema Wanagenzi kisha wakafunga vitabu vyao! Wakasema tena Wanagenzi kutoka Morogoro kuwa “A true relationship is two unperfect people refusing to give up on each other”

Stori inaanzia 1996 takribani kilometa 10,360 kutoka nilipo Ifakara, Morogoro mpaka Rosario katikati mwa Jiji la Buenos Aires, Argentina palipo na kitongoji kinachoitwa Rosario, nyumbani kwa Lionel Messi

Messi akiwa na umri wa miaka tisa tu siku moja mazoezini kwenye klabu ya Newell Old Boys, alikuwa akipasha na rafiki yake wa karibu wakati huo anaitwa Lucas Sciglia, baada ya mazoezi wakaketi kupata maji

Kwenye stori mbili tatu kati ya Maswahiba hao wawili ndipo Lucas akamwambia Messi kuwa nyumbani kwao wana sherehe usiku hivyo anamualika nae wajumuike wote kwenye sherehe hiyo

Tukirudi nyuma kidogo ni kuwa historia ya maisha ya Lionel Messi ni aibu nyingi, ukimya na alikuwa Kijana wa kujitenga sana! Hivyo alikuwa mzito sana kumkubalia Rafiki yake Lucas, lakini akamtazama na kumjibu nitaangalia kama naweza kuja

Wakanyanyuka zao na taratibu wakawa wanarudi zao nyumbani baada ya mazoezi ya siku ile, huku wote wakiwa wachovu kwakuwa Newell ni timu ambayo ilikuwa serious sana na soka la vijana hivyo mazoezi yake hayakuwa mepesi

Usiku ule Lucas akampitia Lionel Messi ili waende kwenye sherehe hiyo kwakuwa anamfahamu Bwana Gwiji huwa hana mambo mengi sana, hivyo Messi alivaa vyema na wakaanza safari ya kuelekea kwenye sherehe

Kumbuka Swahiba wa Messi, Lucas ndie Binamu wa Antonella ambaye ndie Mke wa Lionel Messi hivi sasa na hiyo sherehe inafanyika hapo nyumbani kwa wakina Antonella, basi hakuna ajuaye! Vijana wakawa wanapiga mguu kuelekea

Njiani wakipiga stori kuhusu EP ya Diamond Platnumz wao huko Argentina, mara kuhusu matamko ya Mwijaku wa huko kwao na labda stori za Bakhresa Harmonize, ili mradi safari isiwe ya kuchosha kati ya Messi na Mshikaji wake

ITAENDELEAAA……..
Screenshot_20220316-215846_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom