Makapuku Forum

Makapuku Forum

Baada ya Marekani na umoja wa Ulaya kukubaliana kuiwekea vikwazo vikali Russia vya kiuchumi ikiwemo Marekani kuziwekea vikwazo Benki za Russia, Rais wa Ukraine ameibuka na kusema vikwazo pekee havitoshi kukabiliana na Putin.

Rais huyu ambaye yupo sehemu iliyofichwa ili kuzingatia usalama wake amesema vikwazo pekee haviwezi kumfanya Adui yake Putin asitishe kuivamia Ukraine hivyo kuna hatua zaidi ya vikwazo zinapaswa kufanyika.
Screenshot_20220226-034302_Instagram.jpg
 
Bei ya mafuta imepanda na kuvuka dola mia moja kwa mara ya kwanza tangu miaka saba iliyopita ambapo ongezeko hili linatajwa kusababishwa na hofu juu ya ugavi baada ya Mzalishaji mkubwa wa mafuta Urusi kufanya mashambulio nchini Ukraine.

Bei ya mafuta ghafi kwenye Bara la Ulaya sasa imefikia dola 105 na senti 79 kwa pipa, inafahamika kwenye Nchi zinazozalisha mafuta duniani Urusi ni Mzalishaji muhimu baada ya Saudi Arabia miongoni mwa nchi za shirika la wauzaji mafuta la OPEC.
Screenshot_20220226-034547_Instagram.jpg
 
UEFA imesema Fainali ya Ligi ya Mabingwa 2022 itachezwa Jijini Paris nchini Ufaransa, hii ni baada ya Urusi kuvuliwa uenyeji wa Mechi hiyo kufuatia uvamizi wa Taifa hilo nchini Ukraine.

Fainali ya shindano hilo ilitarajiwa kuchezwa huko St Petersburg May 28 lakini kwa sasa UEFA imesema haitochezwa tena katika uwanja wa Gazprom na badala yake utachezwa Stade de France Jijini Paris.

UEFA imemshukuru Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kwa msaada wake binafsi na kujitolea kuwa mwenyeji wa mchezo huo wa kifahari zaidi wa Klabu za Ulaya.
Screenshot_20220226-034800_Instagram.jpg
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais ( Muungano na Mazingira) Dk Seleman Jafo leo Ijumaa Februari 25, 2022 ametembelea ofisi za Mwananchi Communications LTD jijini Dar es Salaam.
Screenshot_20220226-035127_Instagram.jpg
 
Rais wa Russia, Vladimir Putin amelitaka jeshi la Ukraine kuondoa uongozi uliopo madarakani wa Rais Volodymyr Zelensky huku akiutuhumu kuwa wa kigaidi na genge la watumiaji wa dawa za kulevya
Putin amewashtumu raia wa Ukraine kwa kutuma vifaa vya kivita kwenye makazi ya watu na miji mikubwa ikiwamo Moscow hali inayotishia usalama na kuongeza hofu.
Tuhuma hizo huenda zikaleta hali ya hofu huku ikidaiwa kuwa Urusi inazitumia kama sababu ya kuua raia wa Ukraine.
Screenshot_20220226-035236_Instagram.jpg
 
MANULA, KAPOMBE, KIKOSI BORA CHA WIKI CAF
.
Hiki Hapa Kikosi Bora cha wiki Kombe la Shirikisho Afrika:
1. Aishi Manula (Simba SC)
2. Bandile Shandu (Orlando Pirates)
3. Yasin Hamed (Al Masry)
4. Herve Ngomo (AS Otoho)
5. Dimtri Bissiki (Cotton Sport)
6. Ilyes Jelassi (Al Masry)
7. Shomari Kapombe (Simba SC)
8. Belaid Hamidi (JS Soura)
9. Fagrie Lakay (Pyramids)
10. Junior Makiesse (AS Otoho)
11. Aymen Harzi (Al Ahly Tripoli)
Screenshot_20220226-045124_Instagram.jpg
 
KISA SERIKALI, FIFA YAIFUNGIA KENYA
.
Hatimaye Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) limeshusha rungu kwa taifa la Kenya kutokana na serikali kuingilia usimamizi wa soka.

Kufungiwa kwa Kenya kulitangazwa na Rais wa FIFA, Gianni Infantino, japo alisema kifungo chenyewe ni cha muda usiojulikana ikimaanisha inaweza ikawa cha muda mfupi au mrefu kulingana na namna gani mataifa hao yataweka mambo yao sawa.
.
“Tumelazimika kusimamisha kwa muda usiojulikana mwanachama wetu Kenya. Hii ni kutokana na serikali kuingilia shughuli za soka. Wamesimamishwa mara moja kwa muda usiojulikana na wanajua nini cha kufanya kabla ya kurudishwa au kuondolewa kifungoni,” amesema Infantino.
.
Kenya ilijikuta katika vitabu vibaya vya FIFA baada ya tukio la Novemba 11 mwaka jana Waziri wa Michezo, Balozi Amina Mohamed, alipotangaza kulivunja Shirikisho la Soka Kenya (FKF) chini ya Rais Nick Mwendwa na kuteua kamati shikilizi ikiongozwa na Jaji Mstaafu, Aaron Ringera.
Screenshot_20220226-075833_Instagram.jpg
 
Kisa Vita, Mkomola akwama Ukraine
.
Nyota wa zamani wa Yanga, Yohana Mkomola anayekipiga Girnyk-Sport Gorishni Plavni inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza nchini Ukraine , amesema licha ya kuishi mji ambao haujashambuliwa lakini amekwama kutoka baada ya anga kufungwa.
.
Mkomola amejiunga na timu hiyo kwa mkopo Februari 7 mwaka huu akitokea Vorskla Poltava inayoshiriki Ligi Kuu nchini humo.
.
“Mimi nipo Portava huku bado hakujashambuliwa, jamaa wanaonekana wanapiga sana kwenye sehemu ambazo kuna kambi za jeshi, bado sijajua leo hali itakavyokuwa.”
.
Mkomola aliondoka nchini 2019 na kujiunga kwenye timu ya Vorskla Portava na baada ya kutopata nafasi alitolewa kwa mkopo kwenye klabu ya Ingulets.
Screenshot_20220226-080024_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom