Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20220225-051728_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20220225-052906_Opera%20Mini.jpg
 
KAMA ulikuwa unadhani dili la udhamini wa Kampuni ya GSM katika Ligi Kuu Bara limekufa, pole yako kwani kampuni hiyo na Shirikisho la Soka nchini (TFF) wamerudi mezani kuujadili upya mkataba huo ili GSM iendelee kuidhamini ligi.

GSM ilitangaza kujitoa kama mdhamini mwenza wa Ligi, Februari 7 kwa madai ya kutotimizwa kwa makubaliano ya mkataba baina yao, TFF na Bodi ya Ligi (TPLB).

Mmoja wa viongozi wa juu wa TFF aliyeombwa kuhifadhiwa jina lake, alilidokeza Mwanaspoti kuwa, tayari wameanza mazungumzo ya kuona ni namna gani GSM atarejea kuendelea kuwa mdhamini mwenza wa Ligi Kuu.

“Kinachofayika sasa ni kuona ni namna gani changamoto zilizojitokeza zinawekwa sawa na mazungumzo yanakwenda vizuri na kuna matumaini kwa kiasi fulani wa kupata muafaka wa jambo hili ili GSM arudi Ligi Kuu,” alisema kigogo huyo.
Screenshot_20220225-132003_Instagram.jpg
 
UEFA imethibitisha, Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ilyokuwa ichezwe jiji la St Petersburg May 28, 2022 imehamishiwa Paris kufuatia vita ya Urusi dhidi ya Ukraine inayoendelea hivi sasa.
Screenshot_20220225-133416_Instagram.jpg
 

Sijui kwanini hii kauli yako huwa Inanichekesha sana..

Heri ya Mwaka Mpya kwa mara nyingine tena Auntiee

Sent using Jamii Forums mobile app
Tufurahi tu auntie yangu
Hivi si unajua maisha flani hivi huna stress eenh huna mtu wa kukupangia sijui usiende sehemu flani au usifanye hivi au ukitoka mtu ananuna

Yaani unaishi maisha yako mwenyewe unafanya unachojisikia wewe najua unanielewa vizuri ninavyomaanisha dear
 
• Moja kati ya video zilizogusa hisia za wengi ni hii video ya Raia wa Ukraine ambaye ni Baba wa Mtoto anayeagana nae hapa wakati akimsafirisha Mtoto wake kwenda kwenye maeneo salama na yeye akibaki kupambania Nchi yake.

Serikali ya Ukraine imetangaza kuwa ni marufuku kwa Wanaume wenye umri wa kuanzia miaka 18 hadi 60 kuondoka nchini humo badala yake wametakiwa kubaki ili wapigane kuitetea Nchi yao.
Screenshot_20220225-135036_Instagram.jpg
 
Tufurahi tu auntie yangu
Hivi si unajua maisha flani hivi huna stress eenh huna mtu wa kukupangia sijui usiende sehemu flani au usifanye hivi au ukitoka mtu ananuna

Yaani unaishi maisha yako mwenyewe unafanya unachojisikia wewe najua unanielewa vizuri ninavyomaanisha dear

Umenifanya nimecheka ki faller Auntie
Nakuelewa vyema sana...Na hiyo stress ni juu ya nini? Na Dunia ilivyo na vitu Mob namna hii vya kutupa raha..

Enjoy Life Auntie..Tukutane pale Kijiwe Mishikaki


Sent using Jamii Forums mobile app
 

Umenifanya nimecheka ki faller Auntie
Nakuelewa vyema sana...Na hiyo stress ni juu ya nini? Na Dunia ilivyo na vitu Mob namna hii vya kutupa raha..

Enjoy Life Auntie..Tukutane pale Kijiwe Mishikaki


Sent using Jamii Forums mobile app
Umeona eenh auntie katika maisha kuna kitu nimejifunza me sasa hivi sikaribishi stress ya aina yeyote ile

Kijiwe mishkaki napendaga mishkaki ya nundu jamani sema sasa hivi nimehamia kijijini ila napamiss sana ile salad yao ile
 
Umeona eenh auntie katika maisha kuna kitu nimejifunza me sasa hivi sikaribishi stress ya aina yeyote ile

Kijiwe mishkaki napendaga mishkaki ya nundu jamani sema sasa hivi nimehamia kijijini ila napamiss sana ile salad yao ile
Lini umehamia Kijijini Auntie?

Ndiyoooo..Wale watu ile Mishikaki sijui wanaweka nini? Wakishirikiana na wale Vijana wa pale Upanga....Umeshaijaribu na yao?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hhahahhaha kijiji cha hapahapa jijini auntie sio mkoani

Upanga ipi hiyo sio hapa njia ya kutokea muhimbilia au
Ooooooh!!! Usiniambie Kijijini hapa hapa Jijini Auntie!!!Ni sawa...

Dah!!!Hiyo hiyo...Achana na wale kama unaenda Takukuru...Wale wapo nyuma ya Aga Khan ile shule ya watoto..Wale watu balaa lao siyo dogo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bondia Mtanzania Tony Rashid ameibuka Mshindi kwa kumpiga Bondia wa Afrika Kusini Bongani Mahlangu kwa point katika pambano la round 12 ushindi ambao umempa mkanda wa ABU.
Screenshot_20220226-033820_Instagram.jpg
 
Club ya KRC Genk ya Ubelgiji leo imetangaza rasmi kumpandisha Mtanzania Kelvin John katika timu ya wakubwa akitokea Timu ya U-21, Kelvin amekuwa na wakati mzuri akiwa na kikosi cha vijana na hata January 2022 alifunga hart-trick katika ushindi wa 4-1 dhidi ya Royal Antwerp

Screenshot_20220226-034003_Instagram.jpg
 
Hii ni video fupi inayosambaa iliyorekodi sehemu ya amri za kijeshi zilizotolewa na Wanajeshi wa Urusi ndani ya ardhi ya Ukraine ambao waliwataka Wanajeshi wa Ukraine waweke silaha zao chini na kusalimu amri lakini Wanajeshi hao wakakataa na badala yake Russia ikaamua kuwashambulia na kuwaua Wanajeshi wote.
Screenshot_20220226-034142_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom