Mwaka 2014 Urusi walifanikiwa kutwaa Rasi ya Crimea ya kusini mwa Ukraine, Na kuanza kuwaunga mkono waasi ambao pia wanaiunga mkono Urusi ambao waliteka sehemu kubwa za Mashariki mwa Ukraine.
Urusi walitwaa Pwani hiyo hasa baada ya kutokea kwa Mapinduzi Ukraine mwaka huo huo 2014 ambayo yalimuondoa madarakani Rais wa wakati huo Viktor Yanukovych ambae anatajwa kwamba alikua ni kibaraka mkubwa wa Urusi.
Na mpaka sasa sehemu kama Donetsk na Luhansk kutokea Ukraine ni maeneo ambayo yalijitangaza kuwa huru na hata vita iliyokua inaendelea Ukraine kabla ya hii inayotaka kutokea ilikua ni kutokea vikosi vya hizo sehemu ambazo zinataka kuendelea kujiongoza zenyewe.
Na inasemekana Urusi amekua akitoa msaada wa kijeshi kwa waasi hao ili kuiondoa kabisa serikali ya Ukraine, Na ndio maana nao serikali ya Ukraine mpango wao wa kujiunga NATO ni kutaka kupata msaada ya usalama ambao unazidi kuwa hatarini sababu ya Urusi kufanya mbinu nyingi hatari za chinichini.
Moja ya hatari nyingine inayoendelea pia ndani ya Ukraine, Ni mipasuko ambayo kuna watu wanatamani kuwepo chini ya Urusi na wengine wanataka kubaki kama walivyo.
Kwenye mgogoro huo NATO haikuingilia moja kwa moja, Lakini jibu lao lilikua ni kupeleka wanajeshi wa ziada katika nchi za Ulaya Mashariki kwa mara ya kwanza, zikiwemo Estonia, Latvia, Lithuania, Poland na Romania.
Sasa hali hiyo ndio inawafanya Urusi kila siku kupiga kelele kwamba vikosi hivyo viondolewe, Ina maana kama NATO wataendelea kupeleka vikosi zaidi Ukraine ni kuzidi kuongeza tishio zaidi kwa usalama wa Urusi.
HIVYO BASI, Chanzo cha mgogoro wa Urusi na Ukraine ni; Urusi hataki kuona Ukraine akijiunga na NATO kwa hofu ya usalama kwake wakati nao Ukraine wanataka kufanya hivyo kwa hofu ya usalama ndani yake yote ni kwa sababu ya matendo ambayo wanadai yanafanywa na Urusi ndani ya nchi hiyo.
WW3
Kama vita itazuka inaweza kua Vita ya Tatu Ya Dunia, sababu itahusisha mataifa mengi kwa wakati mmoja na zaidi ni hofu ya matumizi ya silaha za Nyuklia ambazo zinaweza kuathiri karibia dunia nzima. Na ikumbukwe Urusi yeye anaungwa mkono na Korea Ya Kaskazini, Venezuela na China ambazo nazo ni nchi zenye nguvu nzuri tu kijeshi.
MWISHO.