Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20220212-083925_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20220212-083948_Opera%20Mini.jpg
 
LWANGA IN DILUNGA OUT
.
Kiungo wa kimataifa wa Simba Mganda Thadeo Lwanga, yuko fiti kuivaa Asec Mimosas katika mechi ya kwanza ya hatua makundi ya mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika itakayochezwa kesho kwenye Uwanja wa Bemjamin Mkapa.
.
"Lwanga kwa sasa yupo fiti na anaweza kucheza mechi ya Jumapili inategemea na Kocha Mkuu, Pablo Franco atakavyoona. Inaweza akaona bado hajawa na utimamu wa mwili kucheza mechi hiyo, au atamwingiza kipindi cha pili, au pia akamwanzisha kwenye mechi hiyo kwa sababu tayari amepona ana amefanya mazoezi kwa muda mrefu na wenzake," amesema Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ally.
.
Ameongeza pia kiungo Hassa Dilunga naye alipata maumivu akiwa mazoezini, lakini bado wanasubiria majibu ya vipimo vya madaktari ili kufahamu hatima yake kuelekea mchezo huo.
Screenshot_20220212-121707_Instagram.jpg
 
NEVES: ARSENAL KAMA WAMEBEBA UBINGWA
.
Kiungo wa Wolves, Ruben Neves amewashangaa wachezaji wa Arsenal walivyoshangilia utadhani wameshinda ubingwa baada ya kushinda bao 1-0 uwanjani Molineux juzi Alhamisi.
.
Hilo lilimshangaza Neves na kusema sasa Wolves ya kocha Bruno Lage ni timu kubwa ndio maana kuna timu zinashangilia kama zimebeba Ubingwa kwa sababu tu zimepata ushindi wa bao moja.
.
“Tumecheza vizuri, shida hatukufunga tu na tumekuwa tukiruhusu mabao mengi ya mipira ya kutenga. Lile bao lao bado kuna utata, kama kulikuwa na faulo au la, lakini hiyo ndio soka. Tumezoea maamuzi ya hivi.
.
“Ila sijawahi kuwaona Arsenal wakishangilia kama vile kwa kipindi cha miaka 10, ilikuwa ni kama wamebeba ubingwa wa ligi.”
Screenshot_20220212-121902_Instagram.jpg
 
Klabu ya Chelsea leo Jumamosi itamenyana na Palmeiras ya Brazil katika fainali ya klabu bingwa duniani kwa ngazi ya vilabu.

Chelsea ️ Palmeiras
Fainali kombe la dunia kwa vilabu
Mohammed Bin Zayed (Abu Dhabi)
1:30 Jioni.
Screenshot_20220212-122030_Instagram.jpg
 
Mchezaji wa klabu ya Yanga, Dickson Job amefungiwa michezo mitatu (3) na kutozwa faini ya Sh500,000 (laki tano) kwa kosa la kumkanyaga kwenye mbavu mchezaji wa Mbeya City, Richardson Ng'ondya jambo lililotafsiriwa kuwa ni mchezo wa hatari.
Screenshot_20220212-122309_Instagram.jpg
 
Afisa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Yanga, Hassan Bumbuli na Haji Manara wametozwa faini ya Sh500,000 (laki tano) kila mmoja kwa kosa kuwashutumu waamuzi wa Ligi Kuu ya NBC kupitia Vyornbo vya Habari.
Screenshot_20220212-122357_Instagram.jpg
 
Kijana Jadon Sancho bado hajatulia, bado hajajipata yule wa Dortmund, sidhani kama ulikuwa uamuzi sahihi kurejea EPL mapema hivyo

Nadhani ilikuwa bado muda wa kupambana kisha kusogea timu kama Bayern Munich pale pale Bundesliga

Watoto wengi wa South London wana vipaji vikubwa sana ila chini ya presha wanapoteana sana
Screenshot_20220212-124408_Instagram.jpg
 
Kijana Jadon Sancho bado hajatulia, bado hajajipata yule wa Dortmund, sidhani kama ulikuwa uamuzi sahihi kurejea EPL mapema hivyo

Nadhani ilikuwa bado muda wa kupambana kisha kusogea timu kama Bayern Munich pale pale Bundesliga

Watoto wengi wa South London wana vipaji vikubwa sana ila chini ya presha wanapoteana sanaView attachment 2117080
Hii ndo anachopitia lukaku na cr7 pale epl, wanacheza under pressure Kisha wanapoteana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom