Makapuku Forum

Makapuku Forum

UNAAMBIWA:

Sheria ya Makosa ya Mtandao (2015) inaeleza kuwa ni kosa kwa Mtu yoyote kufanikisha utumwaji au kutuma maudhui yoyote ya kidigitali yenye kumdhalilisha/ kuumiza hisia Mtu mwingine, adhabu yake ni faini isiyopungua Tsh. Milioni 5 au kifungo kisichopungua miaka mitatu au Jela au vyote.
Screenshot_20220203-190258_Instagram.jpg
 
UNAAMBIWA:

Watu wanaokutwa na UTI mara kwa mara wanaweza kuwa na mawe kwenye figo, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya mfumo wa mkojo katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dkt Remigius Rugakingira, ameshauri watu wanaokutwa na UTI mara kwa mara wafanye uchunguzi wa kina kwani wanaweza kuwa na mawe kwenye figo.

Dkt Rugakingira amesema kuna baadhi ya bakteria kwenye mfumo wa mkojo ambao wanafanya utengenezaji wa mawe kuwa mkubwa "Mtu anayetibiwaa UTI mara kwa mara anaweza kuwa na bakteria wengi ambao wanatengeza mawe kwenye figo kwa hiyo, ni bora akafanya uchunguzi wa kina"

Amesema Hospitali ya Benjamin Mkapa wanaweza kuyabaini mawe hayo kupitia teknolojia ya vipimo ikiwemo CT SCAN na Utrasound na kuwa wanaweza kutibu tatizo hilo pasipo upasuaji kwa kuwa wana mashine ya Shock Wave Lithotripsy (SWL) ambayo ni mashine inayotumia teknolojia kuyeyusha au kuyaponda mawe na kuyatoa kwa njia ya mkojo.
Screenshot_20220203-190418_Instagram.jpg
 
Raia wa Kenya, Augustine Wanyonyi(34) amefikishwa Mahakamani kwa tuhuma za kuiba Biblia kwenye supermarket Jijini Nairobi ambapo amejitetea kwamba alitaka kuhubiri neno la Mungu badala ya kujiua kutokana na changamoto za kimaisha zinazomkabili baada ya nyumba yake kubomolewa.

Augustine amesema aliiba Biblia mbili ya kwake na nyingine ya Mke wake "Niliiba Biblia ili nisome, nielewe na kuhubiri neno la Mungu badala ya kujiua kutokana na matatizo yanayonikabili, nyumba yangu imebomolewa eneo la Mukuru kwa Njenga "

Alifanya tukio hilo January 30 ambapo camera za CCTV za supermarket zilimnasa akiwa na Biblia hizo ambazo hakuzilipia, atafikiswa tena Mahakamani kwa ajili ya kupewa hukumu February 16, 2022.
Screenshot_20220203-193245_Instagram.jpg
 
Rais wa Marekani Joe Biden amesema Kiongozi wa kundi linalojiita Dola la Kiislamu, Abu Ibrahim al-Hashemi al-Quraishi amejilipua mwenyewe katika operesheni iliyofanyika leo kaskazini-magahribi mwa Syria.

Afisa wa Marekani amesema al-Qurayshi alijilipua mwenyewe wakati wa operesheni hiyo, Al-Quraishi alirithi nafasi ya Abu Bakr al-Baghdad alieliongoza kundi hilo wakati lilipochukuwa udhibiti wa maeneo makubwa nchini Syria na Iraq.

Baghdad aliuawa Oktoba 2019 na Wanajeshi wa Marekani katika operesheni nchini Syria baada ya wapiganaji wa Dola la Kiislamu kushindwa katika uwanja wa vita.

Operesheni ya leo imekuja wakati IS ikijaribu kurejesha makali yake kwa kufanya msururu wa mashambulizi kwenye kanda hiyo yakiwemo ya siku 10 ya mwezi uliyopita yaliyolenga kuliteka gereza.
Screenshot_20220203-193452_Instagram.jpg
 
Baadhi ya Vyuo Vikuu vya Umma nchini Afghanistan vimefunguliwa tena kwa mara ya kwanza tangu kundi la Taliban lilipochokua madaraka mwezi August,2021.

Utawala wa Taliban umetangaza kuwa Wanafunzi wa kike wataruhusiwa kuhudhuria masomo lakini endapo tu watatenganishwa na Wanarunzi wa kiume na mtaala utafuata kanuni za Kiislamu.

Nchi mbalimbali duniani zilishinikiza Taliban kuruhusu elimu kwa Watoto wa kike kama sharti la kupewa misaada ya kiutu, Jumuiya ya Kimataifa imekuwa ikifuatilia kwa karibu endapo utawala huo mpya ungeanzisha sheria kali kama ilivyokuwa wakati wa utawala wake katika miaka ya 90, sheria hizo ziliwazuia Wasichana kupata elimu na Wanawake kufanya kazi.

Chini ya utawala wa Taliban, Wanafunzi wa kiume watahudhuria masomo asubuhi na wa kike mchana ili kuendana na mfumo wa kutenganisha jinsia.
Screenshot_20220203-193658_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom