Makapuku Forum

| Nasreddine Nabi:
.
“Nimewaambia wachezaji sitaki kusikia hata wanazungumza ishu za Simba kwani matokeo yao hayatuhusu na nimewataka wazingitie na kufikiria zaidi mechi zetu zinazotukabili,”
.
“Nimewaambia kabisa nikimkuta mchezaji yeyote anafanya hivyo au mtu yeyote katika benchi langu la ufundi akiijadili Simba au timu nyingine juu ya matokeo yao nitawapa adhabu zilizopo kwenye miongozo yao ya kazi.”
.
“Yanga tuna mechi zetu ambazo sasa zitazidi kuwa ngumu, nimewaambia kuanzia sasa kila mchezo utakaokuwa mbele yetu utakuwa ni sawa na fainali ngumu ambazo ni lazima tuzishinde,”
Screenshot_20220128-171546_Instagram.jpg
 
MSIKIE TRY AGAIN KUHUSU KIBARUA CHA KOCHA PABLO FRANCO
.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba, Salim Abdallah ‘Try Again’ amezungumzia Kuhusu kocha Pablo Franco kunyooshewa vidole na baadhi ya mashabiki, Try again amesema kocha hana shida.
.
“Kocha amechukua ubingwa wa Mapinduzi, amefanya vizuri kwenye mechi nyingi tangu alipojiunga na Simba, sioni tatizo la kocha.
.
“Japo nasisitiza si jambo la kawaida kwa Simba kupoteza mechi mfululizo, inaumiza na yanamuumiza kila mwana Simba hivyo tunaangalia nini cha kufanya.
.
“Kama klabu tutafanya uamuzi sahihi kwa wakati sahihi, mashabiki na wapenzi wa Simba watulie Simba ina viongozi makini na tutapata majibu sahihi kwenye hili,” amesema.
.
Kuhusu kuuweka rehani ubingwa, Try Again amesema “Ndio kwanza tuko kwenye mechi za mzunguko wa kwanza, bado tuna mechi nyingi msimu huu ambazo tunaamini tukijipanga vizuri tutatetea ubingwa wetu msimu huu,”.
Screenshot_20220128-171943_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom