Makapuku Forum

Makapuku Forum

Farhan Jr

INTRODUCTION TO MUKOKO TONOMBE

Define Mukoko Tonombe, refers to a certain humble talent born and raised in Congo Kinshasa, the former country under Mobutu Sseeko

Umejibu vyema, mwingine mwenye majibu mengine? Mukoko ni Binadamu bora alieichezea Yanga Afrika na kuheshimu mkataba wake mpaka dakika ya mwisho

What are the characteristics of Mukoko Tonombe?

- Kipaji kikubwa
-Mvumilivu
  • Kiongozi Bora
  • Nidhamu kubwa
  • Mchezaji wa nguvu

What are the advantages of Mukoko Tonombe?

-Unyumbufu
-Mfungaji mzuri
-Kukaba sana

Neno lolote kwa Mukoko wakati huu ameondoka? Ndio lipo, naomba nimnukuu Mwanafalsafa Peter Pan aliwahi kusema "Never say goodbye, goodbye means going away, going away means forgetting"

Ndio Peter Pan alisema tusipende kusema kwaheri, kwakuwa kwaheri ni kuondoka, kuondoka maana yake ni kusahau! Bila shaka Watanzania hawataki kusahau ubora wake, bila shaka hii ni see you later, kuwa tutaonana baadae tena

Asante kwa kugeuza Katikati mwa dimba kama membari na Imaam, asanteni kupageuza katikati mwa uwanja kama Tanga na mapenzi, Asante kwa kuwapa nafasi ya Wananchi kuishi tena, kutumaini tena na kuamini tena

Asante kwa kuzibariki nyasi za Mkapa, Asante kwa kumbukumbu za Sokoine na Asante kwa nafasi ya mwisho pale Sheikh Amri Abeid, Arusha! Itasalia kwenye kumbukumbu mpaka pale utakaporejea tena
Screenshot_20220125-163111_Instagram.jpg
 
Alisaini kandarasi ya miaka miwili ndani ya Jangwani, alibakiza miezi sita ya mwisho kwenye mkataba wake

Hatimae Teacher Mukoko Tonombe ameondoka nchini na kujiunga na TP MAZEMBE ya kwao Kongo

Mechi yake ya mwisho kwenye jezi ya Yanga ni dhidi ya Mbuni, alikuwa Nahodha na akatuacha na somo la penati
Screenshot_20220125-163459_Instagram.jpg
 
“Kiukweli ilikuwa ni kitu kikubwa yaani hadi sasa hivi kisaikolojia hata siko sawa na sijatulia kabisa, hii vita sasa imekuwa kubwa na imefika pabaya.
.
“Wanafanya hayo ili kunirudisha nyuma nisifanya kile ninachotaka kufanya, nia yao ilikuwa nilale ndani kule, kiukweli hii imeniumiza na ninaona hawa watu hawana nia njema kabisa.”

- Barbara Gonzalez
Screenshot_20220125-163853_Instagram.jpg
 
BARBRA AFUNGUKA MAZITO SAKATA LA KUKAMATWA
.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzalez amedai kuwa kuna mambo yanaendelea kwenye sakata lake la kukamatwa na Jeshi la Polisi Januari 20 na kukaa ndani kwa masaa nane akituhumiwa kutoa lugha chafu kwa mmoja wa maofisa wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
.
“Mimi niliwajibu (polisi) mbona kesi ilifunguliwa na kufungwa kwa sababu hakukuwa na chochote, wakaniambia hapana nimefunguliwa kesi ya jinai kwamba nimetumia lugha chafu ya matusi, baada ya kauli ile ilinibidi nienda ila cha kushangaza nilipofika nilishikiliwa polisi masaa nane,” amesema Barbara na kuongeza:
.
“Kiukweli jambo hili limenistua na kuniumiza, hiyo siku nilijiuliza sana niwaambie watu nikasema ngoja niache kwanza mechi ya Mtibwa Sugar ipite, ila nilianza kuwatafuta viongozi wa Bodi ya Ligi na TFF ili niwaeleze kuhusu uwanja wakawa wanakata simu zangu,”
.
“Nilijiuliza kusema neno stu..d (upuuzi) na nonsense (ujinga au haina maana) imekuwa leo hii ndio matusi." [via Mwanaspoti]
.
Inaendelea ..
Screenshot_20220125-163853_Instagram.jpg
 
Mashabiki 6 wa Simba wamejeruhiwa baada ya gari waliyokuwa wanasafaria kutoka Dar - Kahama- kwenda Bukoba kupinduka eneo la Mwendakulima, basi hilo aina ya coaster lilikuwa na watu 17 ambao walikuwa wanaenda kushuhudia mechi ya Kagera Sugar vs Simba kesho Jumatano kwenye Uwanja wa Kaitaba.

Screenshot_20220125-164200_Instagram.jpg
 
Mechi ya Yanga vs Mbao ya kombe la shirikisho Azam iliyopangwa kupigwa uwanja wa Benjamin Mkapa Januari 29 sasa itapigwa Uwanja wa CCM Kirumba.

Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh amesema waliwaandikia barua uongozi wa TFF kuhusu mechi hiyo kupigwa Mwanza na TFF wamewakubalia
Screenshot_20220125-164350_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom