Makapuku Forum

Makapuku Forum

Watu 8 wameuawa kwa kupigwa risasi kwenye mji wa Perm nchini Urusi na wengine 20 kujeruhiwa baada ya Mwanafunzi mmoja wa kiume kufyetua risasi katika Chuo Kikuu cha Perm.

Timu ya Upelelezi ya Urusi ambayo inachunguza matukio makubwa ya kihalifu imesema Mshambuliaji huyo ameuawa.

Taarifa za awali zinasema Mshambuliaji huyo ni Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 18 ametambulika kuwa ni Timur Bekmansurov lakini bado haijajulikana kwanini amefanya mauaji hayo.
Screenshot_20210922-042908_Instagram.jpg
 
Chanjo ya Covid 19 imeanza kutolewa kwa Watoto wenye umri wa kuanzia miaka 12 hadi 15 nchini Uingereza kwa mara ya kwanza leo .

Zaidi ya Watoto milioni 3 chini ya umri wa miaka 16 wana sifa za kupata chanjo hiyo na Serikali imesema inatarajia angalau 60% ya Watoto hao wapatiwe chanjo hiyo.
Screenshot_20210922-042957_Instagram.jpg
 
"Askari hawa Waliopambana na Hamza miongoni mwao walikuwa ni Askari 11, ambao kwa mamlaka za kisheria za uendeshaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP amewapa zawadi ya vyeti vya ujasiri na zawadi ya pesa kwa kadri alivyoona inafaa"

"Polisi walipambana kuhakikisha kwamba madhara makubwa zaidi ya yale yaliyotokea hayatokei, nani ambaye hafahamu kama yule Mhalifu (Hamza) angeondoka na zile silaha zilizokuwa na magazine mbili na risasi 60 na nyingine alizokuwa nazo nini kingefanyika"

"Kazi ya Polisi ni kulinda Watu na mali zao, ukielewa sehemu moja Watu wanapiga risasi ukaamua kufa kwa ajili ya Watu wengine sio kazi ya kubeza, kazi ya Upolisi sio kazi ya kuitafsiri kirahisi kama baadhi ya Watu wanavyofanya"

"Niendelee kuwatia moyo Askari waliojeruhiwa katika tukio la mapambano kati ya Polisi na Hamza na niendelee kuzitia moyo Familia zilizopoteza Wapendwa wao"------Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Jumanne Muliro
Screenshot_20210922-043109_Instagram.jpg
Screenshot_20210922-043133_Instagram.jpg
 
Serikali ya Sudan imeripoti kuwa kumetokea jaribio la kuipindua serikali kijeshi lakini limedhibitiwa na sasa juhudi za kurejesha hali ya amani linaendelea.

Shirika la Habari la Ufaransa (AFP) limesema kuwa jaribio hilo liliambatana na mpango wa kutwaa jengo ambalo linatumiwa pia na Shirika la Utangazaji la Sudan.

Msemaji wa serikali ya nchi hiyo, amesema mahojiano na watuhumiwa wa jaribio hilo yataanza muda mfupi ujao.
Screenshot_20210922-043315_Instagram.jpg
 
Wafanyabiashara wakiendelea na biashara zao katika moja ya maeneo mkoani Dar es Salaam licha ya kuwepo kibao kinachokataza biashara kwenye eneo hilo.

Uongozi wa mkoa huo unaendelea na maandalizi ya kuwatoa wafanyabiashara kwenye maeneo yasiyotakiwa, ikiwemo hifadhi za barabara.
Screenshot_20210922-043408_Instagram.jpg
 
The home of the Diego Armando Maradona

Jiji la Naples, Kusini mwa Italia na hilo dimba linaitwa Diego Maradona!

Nyumbani kwa SSC NAPOLI, vinara wa SERIE A hivi sasa
Screenshot_20210922-044322_Instagram.jpg
 
Wapiga FAULO bora duniani

1. Juninho (77 goals)

2. Pele (70 goals)

3. Victor Legrottaglie (66 goals)

4. Ronaldinho (66 goals)

5. David Beckham (65 goals)

6. Diego Maradona (62 goals)

7. Zico (62 goals)

8. Ronald Koeman (60 goals)

9. Rogerio Ceni (GK) (59 goals)

10. Marcelinho Carioca (59 goals)

Juninho
Screenshot_20210922-044530_Instagram.jpg
 
Taifa lake lili-enjoy show kwa kumtazama Makamu wa Rais wa Nchi hiyo Ronnie Brunswijk mwenye umri wa miaka 60 akicheza soka uwanjani kwa dakika 54 akiichezea Timu ya Inter Moengotapoe anayoimiliki ambayo ilicheza na Timu ya Olimpia ikiwa ni mechi ya CONCACAF League.

Picha zake akicheza soka zimekua gumzo duniani kwasababu sio jambo la kawaida kumuona Makamu wa Rais akicheza mechi tena mechi ya Ligi, kingine kilichompa nafasi ya ku-trend ni muda mrefu aliomudu kukaa uwanjani pamoja na umri wake kuwa mkubwa (60), hata hivyo uwepo wake haukusaidia chochote kwenye kufungwa kwani Timu yake hiyo ilitembezewa fimbo sita za moto na mpaka full time ilikua 6-0.

Ronnie Brunswijk amekuwa Makamu wa Rais wa Taifa la Suriname lililopo America Kusini toka July mwaka 2020 na aliwahi pia kuwa Kiongozi wa Kundi la waasi (Jungle Commando) mwaka 1985 nchini humo.
Screenshot_20210922-145210_Instagram.jpg
Screenshot_20210922-145233_Instagram.jpg
 
Shirikisho la soka duniani FIFA limeiadhibu Hungary kwenye mechi zake mbili zijazo za kuwania kufuzu Kombe la Dunia ambapo sasa watacheza bila mashabiki uwanjani kutokana na kitendo cha Mashabiki wake kuwafanyia ubaguzi Wachezaji wa England Raheem Sterling na Jude Bellingham baada ya kipigo cha 4-0 huko Budapest.

Adhabu hiyo inakwenda sambamba na faini ya pound 158,416 (Tsh milioni 501) pamoja na kuwa katika uangalizi katika kipindi cha miaka miwili.
Screenshot_20210922-145454_Instagram.jpg
Screenshot_20210922-145520_Instagram.jpg
 
Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ameiondoa kesi namba 208/2016 iliyokuwa inawakabili Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu na wenzake wahariri wa Gazeti la Mawio, akiwemo Jabir Idrisa na Meneja wa Kiwanda cha Jamana, Ismail Mehboob kwa kuwa hana nia ya kuendelea na kesi hiyo.

Katika kesi hiyo kwa pamoja washtakiwa hao, wanakabiliwa na mashtaka matano ikiwamo kuandika habari za uchochezi kinyume na Sheria ya Magazeti ya Mwaka 2002.

Ilidaiwa kuwa kati ya Januari 12 hadi 14, 2016 jijini Dar es Salaam, washtakiwa Jabir, Mkina na Lissu, waliandika na kuchapisha taarifaza uchochezi zenye kichwa cha habari kisemacho, ‘Machafuko yaja Zanzibar.’
Screenshot_20210922-145630_Instagram.jpg
 
UNAAMBIWA

Mapacha wenye umri mkubwa zaidi duniani kwa sasa ni hawa Wanawake wawili wa Japan waliotajwa kuwa Mapacha Wazee zaidi walio hai ambapo hadi September 01,2021 walikuwa na umri wa miaka 107 na siku 300 na walizaliwa November 05,1913 katika Kisiwa cha Shodoshima.

Majina yao ni Umeno Sumiyama na Koume Kodama na wameivunja rekodi ambayo ilikuwa imewekwa na Kin Narita na Gin Kanie ambao pia walikuwa wanatokea Japan.
Screenshot_20210922-145728_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom