ZENGWE JANGWANI
Na @davidfelician10
Tusilale hivi hivi bila ya hii kitu
Kabla ya Michuano ya Champions league Africa kuanza, timu ziliingia Sokoni kusajili na malengo yao makubwa ilikuwa ni michuano hiyo
Naam, Ngoma nagwa, Ngoma ngumu, timu imetolewa tena hatua ya Awali kabisa
Hii watu wanamezea lakini wengine ni ngumu kumeza
Nikiangalia Return of Champions,, nashindwa kumeza mate
Nikiutazam mkataba wa Kilimanjaro na Zanzibar,, hii nayo ndo nashindwa kabisa kufungua hata macho
Tuliwatuma Sokoni wanasafiri mpaka Nchini Dr Congo,, wakatuletea Yannick Bangala, Djuma Shaban, Jesus Moloko, FISTON MAYELE
Lakini tukawatuma mpaka UGANDA kwa Khalid Aucho
Mzee wangu Kijijini kulee Kanyigo akawa ananiuliza vipi walishafika hao wachezaji?
Majibu yangu yalikuwa magumu, nimjibu vipi wakati baadhi yao hawakuwa na ITC,, daah Mzee wangu ilibidi nimzimie Simu, lakini Bahati nzuri majirani walimpa Matokeo DHIDI YA Rivers United
Walivyowawamba jumla ya Mabao mawili kwa YAI na timu kutupwa Nje ya Michuano
Na hivi Sasa Mzee yule anauliza, Je Kuna FAIDA gani sasa ya wale wachezaji kusajiliwa
Nikamjibu Kuna TPL, NGAO YA JAMII NA MAPINDUZI CUP
Nasikia simu ameivunja na hataki kusikia tena Jina la YANGA SC, DAIMA MBELE NYUMA MWIKO