


Farhan Jr
MZEE HASSAN DALALI 'FIELD MARSHAL' NURU KWENYE GIZA LA SIMBA
Mchana wa leo tulifika pembezoni kidogo mwa Jiji la Dar Es Salaam, mpaka Mbagala huko Majimatitu kuonana na Mwenyekiti wa zamani wa klabu ya Simba, HASSAN DALALI
Baada ya interview nzuri sana na CLOUDS FM, tukapata wasaa wa kupiga stori na Mzee huyu mwenye historia kubwa ya klabu ya Simba, nami nitakuwa nawamega kidogo kidogo
Mzee Hassan Dalali mwenyewe anapenda kujiita 'Darasa la saba' katika maswali yangu nikataka kujua kitu kuhusu yale alowahi kuyafanya kwenye kipindi cha Uongozi wake kama Mwenyekiti Simba
Anaanza kunipa stori kwanza kuhusu ule uwanja wa Bunju! Anasema jumla ya hekari za uwanja ule ni 25 ambapo aliununua enzi za uongozi wake 2007, ikiwa ni kiasi cha takribani million 106
Kutokana na ukata mkubwa enzi zile akalazimika kutoa kwanza kiasi cha Tshs 4,000 (Elfu nne) kama kishika uchumba wa kile kiwanja anasema ndoto yake kubwa ilikuwa ni kuona Simba inamiliki uwanja wake
Nikamuuliza hivi karibuni umewahi kufika Bunju? Akacheka na kusema amefika mara nyingi na mpaka halisi wa uwanja ule anaufahamu huku akisema kwa macho tu anajua kuna baadhi ya nyumba zipo ndani ya kiwanja cha Simba (zimejengwa kimakosa)
Hii kitu hata serikali walipokuja kupima wameamuru baadhi ya nyumba zipo ndani ya himaya ya Simba hivyo, zinapaswa kubomolewa! Kifupi Mzee Dalali anaujua ule uwanja, anakwambia hata akisimama tu anajua kila mpaka
Wakati tukiendelea na mazungumzo yetu ya kawaida nje ya MIC, nikamuuliza ana kumbukumbu gani juu ya uwanja ule? Basi hapa ananipa mkasa mkubwa sana
Anasema siku ya kwanza baada ya klabu kuununua uwanja huo akalazimika kwenda kukagua mipaka ya uwanja akiwa kama Mwenyekiti! Mzee Dalali anasema wakati anakatiza kwenye pori (kumbuka Bunju ilikuwa pori haswa) kwa mshangao mkubwa...
ITAENDELEA......Simulizi za Mzee Dalali, mtazipata na yale msoyajua hapa