Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mwamba huyo kushoto anaitwa ALAAN KEEGAN 'The voice of Old Trafford'

Mtu hatari ndie MC wa dimba la Old Trafford, anatangaza lineups na magoli pale OT

Juzi kati wakati anamtambulisha Ronaldo alianza kwa mbwembwe,

"By popular demand, let me introduce to you the number Cristiano Ronaldo"

Mtu wa nongwa sana
Screenshot_20210914-173025_Instagram.jpg
 
Kampuni ya simu za mkononi ya Apple inatarajia leo hii kuonesha matoleo mapya aina nne ya Iphone 13 ambayo ni iPhone 13 mini, iPhone 13, iPhone 13 Pro na iPhone 13 Pro Max.

Hata hivyo imeelezwa kwamba hakuna matarajio makubwa ya mabadiliko kwenye muonrkano wa simu hizi mpya bali mabadiliko makubwa yanayotarajiwa ni processor yenye spidi zaidi, camera yenye picha nzuri zenye ubora zaidi na betri ambayo inakaa na chaji kwa muda mrefu.

Apple pia iatarajiwa kutambulisha aina mpya ya apple watch ambayo itakua na kioo kikubwa tofauti na sasa, pia inatarajiwa wataonesha aina mpya ya airpods pro, iPad na Macbook. View attachment 1937421
Hapo kwenye MacBook ndiyo patamu hapo... 😍😍
 
Kuna vitu vingi tulipitia na hatukutegemea kama vingetokea, kulikuwa na changamoto ya kupata VISA kwa sababu kwa wakati ule mipaka ilikuwa imefungwa, Tanzania ilikuwa kwenye red zone.

Tulipoenda ubalozi wa Nigeria wanasema hakuna VISA, kwa hiyo kabla hata ya kupata tiketi, kila hatua ilikuwa na changamoto hadi tunafika uwanjani siku ya mchezo.

Ukiangalia uwanja tuliotakiwa kucheza haukuwa na vigezo vyote vya CAF, walisema hakutakuwa na mashabiki lakini baadaye unaona kuna watu 1000 hadi 2000. Unaambiwa kutakuwa na taratibu za kujikinga na Corona lakini ukiangalia watu unakuta zaidi ya nusu hawajavaa barakoa na kule kulikuwa na case kubwa ya maambukizi ya Corona.

Unaweza kuwa na mpango wa kufanya lakini unaweza usifanikiwe kutekeleza. Naweza kusema Nigeria kunafanana na DR Congo, mambo mengi ya mpira hayapo katika mpangilio mzuri.

Wajiandae vizuri, wachukue tahadhari na wawe tayari kwa chochote ambacho hakijatarajiwa.

- Barbara Gonzalez akizungumzia mambo waliyokutananayo Nigeria walipokwenda kucheza dhidi ya Plateau United na ushauri wake kwa Yanga ambao wanajiandaa kwenda kucheza dhidi ya Rivers United.
Screenshot_20210914-173146_Instagram.jpg
 
Zahera kumsaidia Nabi huko Nigeria
.
Mwinyi Zahera wiki hii atatambulishwa Yanga kama Mkurugenzi wa Ufundi wa soka la vijana, lakini uongozi umemshauri amsaidie kocha mkuu Nabi kwenye Mechi ya ugenini dhidi ya Rivers United.
.
Zahera mwenyewe amekili kuwa ilikuwa lazima wapate wakati mgumu kucheza na Rivers kwani hawakuwa pamoja wachezaji wote kufanya maandalizi kama iliyokuwa wapinzani wao.
.
Za chinichini zinaeleza kwamba Nabi amekalia kuti kavu na endapo akishindwa kupindua matokeo huko Nigeria ndo basi tena atafungashiwa vilago.
Screenshot_20210914-180232_Instagram.jpg
 
Hizi ni picha za matukio mbalimbali kutoka kwenye uzinduzi wa Mkakati wa Uelimishaji na Uhamasishaji wa Sensa ya Watu na Makazi, uzinduzi umefanyika Dodoma na Mgeni Rasmi alikuwa Rais Samia Suluhu Hassan.

Wasanii Diamond Platnumz, Alikiba na Nandy ni miongoni mwa waliopata fursa ya kuperfom kwenye uzinduzi huo mbele ya Rais Samia.
Screenshot_20210914-181349_Instagram.jpg
Screenshot_20210914-181408_Instagram.jpg
Screenshot_20210914-181425_Instagram.jpg
Screenshot_20210914-181444_Instagram.jpg
 
Yanga ni timu ambayo bado inajijenga kwa sasa hivyo mashabiki wake kuamini timu hii inaweza kufanya makubwa katika michuano ya Kimataifa ni makosa makubwa .

Yanga msimu huu wamefanya usajili mzuri sana ambao kama mwalimu wao akiweza kuunganisha umoja ndani ya kikosi chao na muunganiko ukakubali basi Yanga itakuwa moja timu tishio katika ukanda wa Africa Mashariki.

Kitu kinachoirudisha nyuma Yanga ni kutamani kupata mafanikio kama ambayo wapinzani wao (Simba) wameyapata siku za karibuni. Wakati wanafikiria kufanikiwa mapema wanasahau wapinzani wao ile timu yao waliiunda kwa muda mrefu na walikuwa hawabomoi kikosi cha kwanza kila mwanzo wa msimu kama ambavyo Yanga wanafanya.

Siku zote huwezi kupata kikosi chenye muunganiko bora kama kila siku utabadilisha makocha na pia kusajili wachezaji wengi kila mara ambao utawaleta moja kwa moja kikosi cha kwanza na ukataka Matokeo kwao bila kuwapa muda wa kutosha ili wachezaji waweze kuelewana vilivyo kama ambavyo Simba kikosi Chao kimekaa kwa muda mrefu licha ya kuwa wanafanya maboresho baadhi ya maeneo.

Angalia safu ya ulinzi ya Simba ukitoa Onyango ambaye amekuja msimu ulopita wengine wote ni wachezaji ambao wako pamoja kwa zaidi ya misimu miwili hivyo muunganiko wao ulisha kubali muda mrefu sana hivyo viongozi wa Yanga wanatakiwa kutulia na kumwachia mwalimu kazi ya kusuka timu yao na mashabiki wawe wavumilivu kwani matokeo yatakuja tu baada ya timu yao kuwa sawa.

Kukipa majukumu makubwa kikosi hiki msimu huu ilikuwa ni kukionea Yanga, walitakiwa kusubiri hadi msimu ujao hapo sasa wangeweza kuwa na ndoto ya kufanya vema kwani hadi wakati huo timu yao itakuwa katika muunganiko wa hatari baada ya nyota wao Bangala, Djuma, Moloko, Aucho, Mayele, Makambo na wengine wote kuwa wameshasomana na kila mmoja anajua atacheza vipi na mwenzake.

Yanga sio timu ya kwanza kufanya vibaya hata wapinzani wao Simba walikaa miaka mitano wakiwa na maumivu na baadaye waligundua kosa lao wakajipanga na sasa wanafurahia matunda yao. Yanga kwa sasa inatakiwa kuunda kikosi ambacho kitakaa kwa muda mrefu hii ndiyo dawa ya kuwarejesha katika ushindani bila kufanya hivi kila msimu itakuwa inajijenga bila mafanikio.
Screenshot_20210914-182712_Instagram.jpg
 
Simba leo imecheza mechi ya ya kirafiki katika maandalizi ya msimu ujao katika kambi yao Arusha dhidi ya Aigle Noir ya Burundi na kushinda mabao - yaliyofungwa na Kibu Denis na Bernard Morrison.
Screenshot_20210914-184228_Instagram.jpg
 
Wasanii wanaoishabikia Club ya Simba leo hii wamekutana katika Duka la Mfanyabiashara Vunja Bei na kuzungumza na Waandishi wa Habari kuelekea Simba Day siku ya September 19,2021 pale Uwanja wa Mkapa.

Wasanii waliohudhuria ni wa Bongo Movie na wa Bongo Fleva wakiwemo Monalisa, Bambo, Whozu, Meja kunta , Ben Kinyaia, Mwasiti, JB, Quick Rocka, Tausi, Ally Choki, Natasha n.k

Pamoja na mambo mengine wameomba Mashabiki wa Simba kujitokeza kwa wingi Uwanjani.
Screenshot_20210916-040624_Instagram.jpg
Screenshot_20210916-040650_Instagram.jpg
Screenshot_20210916-040717_Instagram.jpg
 
Mtu ambaye bado hajafahamika jina lake mpaka sasa ameanza tena ameingia kwenye nyumba 9 jana katika kata ya Muriet eneo la Mshikamano kwa Pateli jijini Arusha akiwa amevalia nguo za kike ambapo alivunja milango na madirisha na kuingia ndani.

Mama ambaye alimshuhudia Mtu huyo amesema alivunja dirisha la nyumba yake usiku wa manane akaingia ndani na kuanza kumkumbatia huku akimwambia yeye ni jirani yake na anataka afanye kitu kibaya ila asimuambie Mtu.

"Nilimkuta Mtu kanisimamia pembeni ya kitanda akainama chini akaanza kunikumbatia, nikaanza kum-push nikapiga kelele Vijana wakatoka akakimbia, alikuwa amevaa baibui ni bonge halafu ni mfupi alikuwa ana harufu ya mafuta na aliponishika aliniachia harufu ya mafuta"

Paulo Mbise Balozi wa mtaa huo wa Mshikamano amesema ni kweli alipata taarifa hizo na kuwashirikisha Polisi ambapo baadaye walizunguka na kubaini kupita kwa Mtu huyo.

Mwezi uliopita kuliibuka tena taharuki katika eneo la Murieti baada ya Wananchi kukaa kikao cha kumtafuta Mtu asiefahamika aliyepewa jina la Teleza ambaye alikuwa akiingia kwenye nyumba za Watu usiku huku akiwa na mafuta na kuwabaka Wanawake.
Screenshot_20210916-040950_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom