Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20210831-075639_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20210831-075654_Opera%20Mini.jpg
 
MIKONO YA KIHAMU YA FARHAN JR

TAJIRI GSM, ONE THING ABOUT FOOTBALL, IS NOT FOOTBALL

Aliwahi kuulizwa Kocha Sir Alex Ferguson, ni nani mtu muhimu sana kwako kwenye setup nzima ya Manchester United? Nae akasema kiwepesi sana, ni DAVID GILL

Akaendelea kusema "Listen to me Kids, one thing about football is not about football" akiwaambia Wanafunzi kutoka Chuo cha Havard kitivo cha Biashara

Kwa kifupi Fergie alimaanisha kitu kimoja kuhusu mpira, huwa wala hakihusu mpira! Yani mafanikio ya Manchester United yalianzia kwenye eneo la viongozi, kuanzia Matajiri, Bodi na Mtendaji Mkuu David Gill

Naona Tajiri GSM anavyopambana sana kuirejesha Yanga Afrika kwenye ramani, haswa zaidi kuwekeza uwanjani kwenye kikosi hii process inaitwa INSTANT SUCCESS! Wanachojaribu kukifanya Yanga kiliwahi kufanywa na Chelsea (Tutaongea siku)

Lakini naomba nimwambie kitu Tajiri GSM kwa elimu yangu ndogo sana, pale Chelsea walikuwa na Michael Emenalo akipambania mipango (Plans implementor), Roman aliweka pesa ila yeye ndie alizigeuza pesa kuwa Mataji, alikuwa Mtendaji mzuri sana

Nachokiona kwa Wananchi, sio uwanjani bali ni eneo kubwa la utawala! Wanapaswa kuweka nguvu kubwa kujenga timu kali ya Utawala (Executive) hawa watageuza pesa zake kuwa Mataji pale Yanga

Naomba nimpe pia mfano mwingine Tajiri GSM, wale Waarabu wa Manchester City nchini ya Sheikh Mansour Bin Zayed waliwahi kumuhitaji Pep Guardiola wakati yupo mapumziko ya mwaka mzima Jijini New York

Guardiola aliwaambia mna pesa nyingi sana ila bado hamna ushindi! Akampa majina mawili Mwenyekiti wa City, Khaldoon Mubarak, alimpa jina la Ferran Soriano na Txiki Berigistein! Hawa ni miamba na ndio walikuwa mihimili ya FC Barcelona

Txiki sasa yupo City na ndie Director of Football na Soriano sasa yupo City ndie Mtendaji Mkuu wa Klabu, ndipo hapo Pep akasogea baadae kujiunga na City akiamini tayari timu imetimia na wanaweza kufanya kitu kikubwa barani Ulaya

Tajiri GSM umemaliza kusajili sasa pambana kusaka Watawala, unda timu ya ushindi kuanzia ofisini na Yanga itarejea pale unapotaka! Kinachokutokea ndicho kinawatokea Arsenal, wana timu ya Viongozi ambao hawana Uzoefu
Screenshot_20210831-133554_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

Kila Mshindi ana historia ngumu ya maisha yake, kwenye kila stori ya mafanikio ya Mwanaume sio lazma nyuma awe Mwanamke

Kuna muda nyuma ya mafanikio ya Mwanaume ni dharau alizopitia, shida kali alizopitia na kuna muda akalazimika kuweka maisha yake hatiani

Cristiano Ronaldo alipotimiza umri wa miaka 15 akiwa kwenye timu ya SPORTING CP ya kwao Ureno aligundulika ana shida kubwa sana ya moyo

Kitaalam wanaita RACING HEART! yani mapigo yake ya moyo yanakimbia kuliko kawaida, eidha awe anacheza au hachezi! Chukulia mfano moyo unavoenda mbio ukimaliza kukimbia, basi Ronaldo ilikuwa vile hata kama hakimbii

Madaktari wa SPORTING CP walipompima wakasema wazi ni tatizo linaloweza kutamatisha maisha yake ya soka, kulikuwa na uwezekano wa kijana kutangaza kustaafu soka akiwa mdogo sana

Timu ya Madaktari bado ikaendelea kutafuta suluhu ili kuokoa kipaji hiki kikubwa, ndipo waliposema kijana apasuliwe ili kumuweka sawa, ingali bado hawakuwa na uhakika wa Fundi kupona

Alipigiwa simu Mama yake mzazi, Dolores Aveiro asafiri kwa ndege ya Jioni kutoka San Antonio mpaka Lisbon kuamua hatma ya Mwanae na yeye atasaini karatasi! Mama alifika na akaruhusu wampasue Kijana wake

Ronaldo aliingizwa Theater na timu ya Wataalam zaidi ya 10 akiwa Daktari bingwa wa Magonjwa ya Moyo, Dr Almando Cunha akiongoza timu! Inasemekana ni moja kati ya upasuaji mrefu zaidi kwenye hospital hiyo

Kuanzia asubuhi mpaka saa saba Mchana ndipo Ronaldo anatolewa, Madaktari wakatoa taarifa kuwa Kijana atakuwa sawa! Hatimae Ronaldo alipona na akarejea Uwanjani baada ya muda

Wataalam wanasema, kasi aliyonayo kwasasa haikuwa hivyo kabla ya upasuaji! Inasemekana baada ya upasuaji uwezo wake wa kukimbia uliongezeka maradufu

Na hii ndio historia ya Cristiano Ronaldo kabla ya kuwa Staa wa dunia

Screenshot_20210831-133944_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

SIMBA WANAHITAJI TENA AFISA HABARI KAMA HAJI MANARA?

Wale waliosoma Language 1 Advanced Level na wale wa Linguistics Chuo Kikuu mtakubaliana nami kuhusu COMPETENCE vs PERFORMANCE! Alielezea sana Mtaalam Noam Chomsky

Ukienda mbali zaidi kwa kutumia contextual meaning utagundua kuwa Noam Chomsky ni kama anatuambia kuna uhusiano mdogo sana kati ya KUJUA vitu na KUWASILISHA vitu

Haji Manara anaweza asiwe msomi mkubwa sana wa level ya PhD au Masters ila ana kitu cha kipekee kwenye uwasilishaji, ni talanta Mungu anawapa watu!

Ndio maana Noam Chomsky alisema "Competency preceeds Performance" lakini kwenye Developmental psychology napo kuna Maswali, Je uwasilishaji ni kipimo cha Mtu kujua? Je kufeli kuwasilisha ni kipimo cha Mtu kutojua? Yamebaki maswali

Nimeanza kwanza kumpa Haji sifa zake, Mnyonge mnyongeni ila ile haki yake hata kama ni nyepesi kama punje ya haradani basi tumpe! Anastahili sifa hizo kwenye PERFORMANCE, Mtu sana!

Swali kubwa sana niliulizwa na Mjomba wangu kutoka nyumbani Morogoro! JE SIMBA WANAHITAJI MTU KAMA HAJI TENA?.....

Awali ya yote namnukuu Kaka yangu Shaffih Dauda aliwahi kusema "Itafika muda Manara hatohitajika ndani ya Simba, sio chuki bali Mfumo" alisema Kaka mnamo Mei 13, 2021

Nami nianzie hapo kujenga msingi wa hoja zangu! Kwanza nijibu kuwa HAPANA SIMBA HAWAHITAJI TENA HAJI MWINGINE TENA

Awali historia ya Wasemaji (Spokesman) ilianzia 1929 White House, Jijini Washington nchini Marekani, chini ya Rais Herbet Hoover, ndie yeye alituletea dunia Mtu kwa ajili ya kuisemea Taasisi

Lakini hii ikaja mpaka kwenye Mpira wetu wa miguu! Sasa kuna kitu kinaitwa TRANSFORMATION vs DEVELOPMENT, Wataalam wa mpira walisema..... INAENDELEA
Screenshot_20210831-134124_Instagram.jpg
 
SIMBA INAHITAJI TENA AFISA HABARI KAMA HAJI MANARA? (FINAL)

Nikasema kitu kuhusu TRANSFORMATION vs DEVELOPMENT! Mabadiliko dhidi Maendeleo! Ni lazima kwanza tujue nini maana ya Maendeleo

Kwa mujibu wa vitabu vya historia vinasema "Its a gradual change, from lower to higher and each stage is better than the proceeding one" kifupi ni mabadiliko ya kihatua, kila hatua ni bora kuliko iliyopita

Ipi hadhi ya Simba kitaasisi? Tayari wapo mbali, tayari wamefanya mabadiliko na wanaendelea kupiga hatua! Lakini kila hatua itakuwa bora kuliko iliyopita, baadhi ya vitu vitaachwa na baadhi kuongezwa

Niliwahi kujihoji ni yupi Afisa Mawasiliano wa Manchester United? Nikapata majibu kuwa anaitwa Charlie Brooks walimtoa kutoka Kampuni ya NIKE, lakini wapo wakina Karen Shotbolt na wengine wengi kwenye kitengo

Lakini kwanini hawasikiki? Ni kwakuwa wanaishi kwenye misingi yao! Wakitekeleza majukumu yao yote kwa 100%

Kwanini nimesema wanatimiza kwa asilimia mia? Naomba tufahamu kuwa Media Officer/Director of Communication kazi yake sio kuongea tu! Pengine tufahamu kuongea kwa niaba ya taasisi ni sehemu yake ndogo sana! Hii ni kazi ya CEO, Mwenyekiti au Rais

West Ham United mnamo 2019 walitangaza nafasi ya kazi ya Afisa Habari! Kwenye majukumu wakataja baadhi wakasema; kazi yake ni kuandaa press kwa ajili ya Makocha na wachezaji, kuandaa na kuandika story kutumia kwenye digital platforms

Kusimamia Wachezaji kwenda kwenye Interview na Matangazo ya Wadhamini, kufanya kazi kwa karibu na Media na kudumisha mahusiano (sio kugombana) na kuwasilisha taarifa za klabu kwa maandishi (Press Release)

Hapa tumegundua wana kazi nyingi sana! Lakini wanasisitiza zaidi kutumia maandishi (Formal way) kuliko maneno maana kuna kupunguza au kuongeza kitu tofauti na Bodi au Viongozi walichokutuma

Huo ndio mfumo wa Media Officers duniani huko kwenye klabu zao! Walipo Simba ni vyema wakafuata mfumo huo
Screenshot_20210831-134124_Instagram.jpg
 
Bosi Yanga atoa neno

“Matokeo mabaya tuliyopata yanatujenga kuboresha upungufu ulioonekana. Ni mapema sana kukosoa usajili kwani timu ndio bado, ina nafasi ya kukaa pamoja muda mrefu ili kujiweka fiti kabla ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika,
.
“Naiona Yanga iliyo bora msimu ujao, nauona utakavyokuwa ushindani mkubwa ndani na nje kutokana na kusajili wachezaji wengi wenye uzoefu na walio na uchu wa mafanikio.”
.
- Gharib Said Mohamed
Screenshot_20210831-134829_Instagram.jpg
 
Hassan Kessy atua KMC
.
Beki Hassan Kessy amejiunga na klabu ya KMC kwa mkataba wa mwaka mmoja, baada ya kumaliza mkataba wake na Mtibwa Sugar aliyoitumikia msimu uliopita.
.
Kessy ni kama safari yake ya kwenda kucheza soka la kulipwa nje inafutika kwani baada ya kurejea nchini nakujiunga Mtibwa Sugar, alikaririwa akisema ataondoka tena lakini kujiunga kwake na KMC ni kama kunafuta matumaini hayo.
.
Kessy anatua kuziba pengo lililoachwa na Israel Patrick aliyetua Simba.
Screenshot_20210831-135006_Instagram.jpg
 
| Camavinga REAL MADRID
.
Eduardo Camavinga fundi anaripotiwa kuwa muda wowote atatangazwa rasmi kama mchezaji mpya wa Real Madrid kutoka Rennes.
.
Ofa ya Real Madrid ya Euro milioni 31 (€31m) imekubaliwa, na tayari kinda huyo amefanya vipimo vya Afya kujiunga na Real Madrid akiitosa PSG na Man United.
Screenshot_20210831-135144_Instagram.jpg
 
7 | Supastaa wa Manchester United Cristiano Ronaldo anatarajiwa kupewa jezi yake namba 7 huko Old Trafford.
.
Mshambuliaji Edinson Cavani atachukua jezi namba 21 ya Dan James aliyejiunga na Leeds United kwa dau la Euro Milioni 30.
Screenshot_20210831-135457_Instagram.jpg
 
| Shikhalo KMC
.
Aliyekuwa kipa wa Yanga, Faruk Shikhalo amejiunga na klabu ya KMC kwa mkataba wa mwaka mmoja kuitumikia timu hiyo.
.
Shikhalo anaenda kukutana na kipa mkongwe, Juma Kaseja ambaye amejihakikishia nafasi ya kuanza kwenye kikosi cha KMC.
Screenshot_20210831-135741_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom