Makapuku Forum

Makapuku Forum

Saul Anatua Chelsea
.
Imeripotiwa kuwa Chelsea wamefikia Makubaliano na Atletico juu ya uhamìsho wa mkopo wa kiungo Saul Niguez kwa dau la euro milioni 5.
.
Saúl atatua London muda wowote kusaini mkataba.
Screenshot_20210831-211155_Instagram.jpg
 
Spika wa Bunge Job Ndugai ameomba radhi Wakristo na Watanzania wote kwa ujumla waliokwazika na kauli yake aliyoitoa leo asubuhi Bungeni akieleza mstari wa Biblia ambapo taarifa hiyo ya Bunge imesema alichokua anamaanisha ni Yusufu na sio Yesu.

Alichomaanisha Spika ni kwamba "Yusufu alitembea na Mke wake kutoka Nazareti kwenda mpaka Yerusalemu kuhesabiwa" na sio Yesu kama alivyotamka, kilichotokea ni hali ya kibinaadamu ya ulimi kuteleza ambayo inaweza kumtokea Mtu yeyote.... imeeleza taarifa hiyo.
Screenshot_20210831-211550_Instagram.jpg
 
Mkataba wetu ndio mkataba mkubwa zaidi wa kutengeneza jezi Afrika Mashariki na Kati. Biashara ya jezi ni kubwa.

Hakuna design yoyote ambayo mpaka sasa imeonekana mtaani (hazijavunja), tunataka jezi yetu ionekane kwa machoni kwa watu kwa mara ya kwanza siku ya uzinduzi.

Uzinduzi utafanyika Jumamosi September 4 kuanzia saa 1:00-3:00 usiku. Kutakuwa na wageni walioalikwa, haitakuwa kwa kila mtu wengine watafatilia kupitia luninga na mitandao ya kijamii.

Jezi yetu ni nzuri tumeangalia mambo mengi, tumezingatia ubingwa, fashion ili mtu avae hata akitaka kwenda maeneo mengine.

Zitaanza kupatikana kwenye maduka ya Vunjabei siku hiyohiyo jezi zitakapozinduliwa. Fred Vunjabei

Screenshot_20210901-180023_Instagram.jpg
 
Boxing ni mchezo ambao huwezi kumsifia mwenzako ndio maana sio mchezo wa masheikh, kumsifia mtu ni ishara za kumuogopa. Masheikh watabaki mashabiki lakini sio boxer halafu kila linalosemwa kwako wewe unaitikia hewala.

Mohamed Ali alikuwa anawatukana wapinzani wake, kwa nini nikisema mimi naonekana nimekosea? Boxing ni mchezo wa tambo na majivuno.

Mimi najivunia ni bora na ubora wangu unaonekana takwimu, namba hazidanganyi.

Kama ni rahisi watengeneze Mwakinyo mwingine mwenye thamani ya nyota nne kama inawezekana.

- Hassan Mwakinyo
Screenshot_20210901-180227_Instagram.jpg
 
Boxing ni mchezo ambao huwezi kumsifia mwenzako ndio maana sio mchezo wa masheikh, kumsifia mtu ni ishara za kumuogopa. Masheikh watabaki mashabiki lakini sio boxer halafu kila linalosemwa kwako wewe unaitikia hewala.

Mohamed Ali alikuwa anawatukana wapinzani wake, kwa nini nikisema mimi naonekana nimekosea? Boxing ni mchezo wa tambo na majivuno.

Mimi najivunia ni bora na ubora wangu unaonekana takwimu, namba hazidanganyi.

Kama ni rahisi watengeneze Mwakinyo mwingine mwenye thamani ya nyota nne kama inawezekana.

- Hassan MwakinyoView attachment 1919866
Huyu dogo naye kalewa sifa

Ni mchezo wa hatari. It is always one serious blow to the head away from permanent brain damage. Atunze hela anazopata vizuri ili huko mbele ya safari zije zimsaidie maana wengi wao huwa hawamalizi vyema.
 
Sipigani kufurahisha watu, napigana kwa ajili ya kufikia ndoto zangu. Nipoingia kwenye boxing sikuomba ushauri wala kuandika sehemu naomba maoni kwa hiyo watu hawawezi kunipangia.

Watu wana nafasi yao kwangu lakini na mimi nina matakwa yangu binafsi, hakuna mtu aliwahi kufanikiwa kwa kuwaridhisha watu.

Nafikiri jamaa kama ana hamu ya kupigana mapambano ya ndani, kuna akina Selemani Kidunda wa uzito wake anapaswa aoneshe kuwa amemaliza.

Juzi Yordenis kampiga Manny Pacquiao kalipwa dola milioni tatu, natamani ningekuwa naongelewa mimi lakini unanikutanisha na promoter ambaye anapambania milioni 50, mimi atanilipa kiasi gani?

Kama ilivyokuwa hatuwezi kumuona Mtume tena, ndivyo ambavyo haliwezekani hilo pambano.

- Hassan Mwakinyo
Screenshot_20210901-180441_Instagram.jpg
 
Ninaposema hakuna mtu wa kupigananae Tanzania, haimaanishi mimi ni bora kuliko watu wote au hakuna mtu atakaeweza kunipiga. Huu ni mchezo ngumi hazina mwenyewe.

Mimi nina heshimu nilipo kwa sababu najua nilipotoka, leo kuna ma-boxer wengi sana lakini ukimzungumzia Mwakinyo ni pekeyake kwa sababu rekodi yangu haifanani na ya mtu yeyote.

Kwa hiyo, apatikane kwanza mtu mwenye rekodi kama ya Mwakinyo, ili nitakapopigananae mbali ya kupata pesa tu lakini ikitokea nimepoteza sishuki kwenye viwango vya ubora kwa sababu nimepigwa na bingwa.

Mfano, bondia nitakayepinanae [Julius Indongo] sina wasiwasi hata akinipiga sishuki kwenye viwango vya ubora kwa sababu ameshacheza na watu wakubwa zaidi yangu lakini nikimpiga haitashtua, watu watanisifu na kwenye ubora haitanipandisha sana kwa sababu tayari nipo juu.

Mtu akishafikia kwenye ubora nilipo mimi tunaweza kukaa kuzungumza nalipwaje ili tupigane sio kuandika kwenye mitandao kwamba kuna beberu linagombaniwa. Ngumi za kulipwa hazipo hivyo.

Mimi nina uongozi, hata unapomtaka mwanamke kwa ajili ya kuoa kuna taratibu zake sio kuandika kwenye mitandao mimi nataka kumuoa fulani.
Screenshot_20210901-180904_Instagram.jpg
 
Sijawahi kusikia katika rekodi ya kidunia hata huko Ulaya yanakotengenezwa magari kwamba kuna promoter ameandaa Rolls Roys watu wapigane, isipokuwa watu wanapewa mikanda ambayo wanapata pesa za kununua magari, wajenge na wawe na viwanda vya kutengeneza magari kupitia heshima walioyoipata kwa kutwaa mikanda.
Screenshot_20210901-180227_Instagram.jpg
 
Aina ya taji ambalo nalishikilia ni WBC Africa, kwa hiyo sipaswi kucheza na bondia ambaye anatoka nje ya Afrika. Kwa rekodi ambayo ninayo sasa hivi, wengi ambao ni wazuri Afrika rekodi zao haziko kama zangu kwa hiyo yeye [Julius Indingo] ndio ana rekodi kama yangu lakini ni Muafrika anayeishi Marekani.

Kwa sababu amezaliwa Afrika [Namibia] na ameanzia Afrika ni halali kupigananae kwa aina ya taji ambalo nikonalo.
Screenshot_20210901-181205_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom