Makapuku Forum

Makapuku Forum

CHAMA MKWANJA MREFU ANASEPA
.
Vyombo vya habari nchini Morocco vimeripoti kuwa kiungo wa Simba, Clatous Chama anatarajiwa kusajiliwa na klabu ya FAR Rabata kwa dau la dola 600,000 (Sh bil 1.3).
.
SA pia tumejiridhisha kwamba Chama jana Jumatatu hakujumuishwa kwenye orodha ya wachezaji wa Simba wanaojiandaa kwenda kambini.
.
Upande wa Chama mwenyewe amekanusha akisema;
“Hizo taarifa nimeziona kwenye Instagram kaka, bado nina mkataba wa miaka miwili na sijaambiwa lolote.
.
Wakati huo huo, wiki moja nyuma mchezaji huyo alikaririwa kupitia ukurasa wake wa Instagram alipokuwa mubashara (Live) akisema yupo tayari kuondoka kwenda timu yoyote kama tu mabosi wa Simba watakubaliana na timu hiyo.
.
Mmoja wa mabosi kutoka Simba amefunguka kuwa ofa ya Chama ni kubwa hawawezi kuiachia ila wanaiweka sawa kabla ya kukamilisha dili hilo.
Screenshot_20210810-102946_GBInsta.jpg
 
OFFICIAL | Kikosi cha timu ya YANGA kitaondoka Dar es Salaam kwenda Morocco kwa Maandalizi ya msimu ujao.
.
Kwa mujibu wa mmoja wa kiongozi wa Yanga ni kwamba timu yao itaondoka katikati ya wiki hii ili kuwahi kambi hiyo itakayoambatana na michezo ya kirafiki na kurejea siku chache kabla ya SIKU YA MWANANCHI.
Screenshot_20210810-103132_GBInsta.jpg
 
Yanga, Simba kukutana Morocco
.
Kikosi cha Simba kinatarajiwa kuondoka leo jijini Dar kuelekea nchini Morocco kwa ajili ya kuweka kambi ya wiki mbili kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao.
.
Yanga nao kupitia mitandao yao ya kijamii wamethibitisha kuweka kambi nchini humo bila kuweka wazi wataenda lini.
.
Maandalizi ya timu hizo yanaanza mapema kutokana na mrundikano wa ratiba za michuano ya kimataifa inayotarajiwa kuanza Septemba 10, huku Ligi Kuu Tanzania Bara ikitarajiwa kuanza Septemba 29.
Screenshot_20210810-111413_GBInsta.jpg
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata na linawashikilia Watu sita kwa tuhuma za kuwashambulia na kuwarekodi video za utupu Watu wawili Mwanaume (Rashid Kawanje) na Mwanamke (Anitha Laurian) na kuzituma mitandaoni wakidai kuwa wamewafumania.

Watuhumiwa hao ni Singiba Buchadi(42), Fundi umeme, Mkazi wa Kongowe mwisho,Dephina Buchadi (42), Mfanyabiashara, Mkazi wa Kongowe, Doratea Mathayo (39), Mkazi wa Kongowe Mwisho, Wilbard Teobard (55), Albert Buchadi (30), na Valenzi Silvester (40).

“Vitendo vya kikatili walivyovifanya Watuhumiwa hao ni pamoja na kutoa adhabu wakati wao si Mahakimu au Majaji, vitendo hivyo havikubaliki kisheria katika Nchi inayofuata mfumo wa utawala wa sheria na kwa sababu hizo watafikishwa Mahakamani haraka iwezekanavyo”———-Muliro Jumanne , Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya DSM

Video nzima ya tukio hilo la madai ya fumanizi ipo kwenye Youtube ya ‘millardayo’ au bonyeza link kwenye Bio hapo juu kuitazama direct.
Screenshot_20210811-041530_GBInsta.jpg
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limemtaka Dereva aliyewagonga Wanafunzi na kisha kukimbia, ajisalimishe haraka iwezekanavyo kituo chochote cha Polisi kilicho karibu na yeye kwani hana uwezo wa kujificha zaidi ya saa 48.

“August 09, 2021 saa 11:15 Alfajiri katika Barabara ya Bagamoyo maeneo ya Afrikana Stendi ya Daladala Wilaya ya Kinondoni gari aina ya Scania liliwagonga watambea kwa miguu wawili (Wanafunzi) waliofahamika kwa majina ya Collins Ngowi (15) Mwanafunzi wa kidato cha pili Shule ya Sekondari Makongo na Salvina Otieno (anayekadiriwa kuwa na miaka kati ya 10-15) Mwanafunzi wa darasa saba Shule ya Msingi Mount Sery (wote wawili baadae walifariki dunia)”

“Mwanafunzi mwingine aitwaye Ashura wa kidato cha tano Shule ya Sekondari Al-hara main alipata majeraha sehemu za mwili na alikimbizwa Hospitali, chanzo cha ajali kinachunguzwa ikiwa ni pamoja na ukaguzi wa gari hilo, Dereva amekimbia baada ya kuwagonga Wanafunzi hao na tunamtafuta, ajisalimishe” ———-Jumanne Muliro, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya DSM
Screenshot_20210811-041652_GBInsta.jpg
 
Muswada wa mapendekezo umefichua mpango wa Majimbo 16 ya Ujerumani na wa Serikali Kuu juu ya kuacha kuwapima Watu maambukizi ya Corona bila ya kulipia.

Wabunge wa Ujerumani wanatarajiwa kuupitisha mpango huo mwezi wa October ambapo sasa Watu watalazimika kujilipia ili kupimwa Corona.

Kwa mujibu wa taarifa pendekezo hilo limetoka kwenye Ofisi ya Kansela na litajadiliwa leo na Mawaziri Wakuu wa Majimbo yote 16 ya Ujerumani.

Pendekezo hilo limetokana na kauli zilizotolewa pia na Waziri wa Afya wa Ujerumani Jens Spahn aliesema kwamba Watu waliokataa chanjo watapaswa kujilipia wenyewe endapo watataka kupimwa maambukizi ya virusi vya corona.

Amesema kwakuwa Wananchi wote wa Ujerumani wamepewa fursa ya kupata chanjo si lazima kwa Serikali sasa kuwalipia Watu wanaotaka kupimwa maambukizi ya Corona.
Screenshot_20210811-041915_GBInsta.jpg
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla leo August 10, 2021 ameshuhudia awamu ya kwanza ya utilianaji sahihi wa mikataba 41 yenye thamani ya Shilingi Bilioni 14.1 kwa ajili ya Ujenzi wa Barabara za Mkoa wa Dar es salaam na kuwataka Wakandarasi kuhakikisha wanakamilisha Miradi kwa wakati na kwa kiwango.

RC Makalla ametoa maelekezo hayo wakati wa hafla ya utilianaji sahihi mikataba baina ya TARURA na Wakandarasi ambapo amesema
mafanikio haya yote ni matokeo ya kazi kubwa na nzuri ya Serikali ya awamu ya sita Chini ya Rais Samia Suluhu Hassan Katika utatuzi kero za Wananchi.

RC Makalla amewaelekeza DAWASA, TANROADS, TARURA, TTCL na TANESCO kufanya kazi kwa pamoja ili kuondoa tatizo la miradi kutomalizika kwa wakati kutokana na Taasisi husika kuchelewa kuhamisha miundombinu.

Pamoja na hayo RC Makalla amewaelekeza TANROADS na TARURA kuhakikisha wanasimamia utunzaji wa miundombinu ya Barabara ikiwa ni pamoja na usafi, ukarabati na uwekaji wa vibao vya kuzuia biashara Kwenye eneo la hifadhi ya Barabara.

RC Makalla ameonesha kufurahishwa na ongezeko la bajeti ya Ujenzi wa Barabara Dar es salaam kutoka Shilingi bilioni 25 hadi bilioni 40 na Nchi nzima kufikia Bilion 300.
Screenshot_20210811-042113_GBInsta.jpg
 
Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani amemuagiza Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) nchini kuhakikisha anashughulikia suala la kupanda kwa bei ya mitungi ya gesi nchini ndani ya kipindi cha siku 14 kuanzia leo.

Dkt.Kalemani ameyasema hayo Wilayani Chato Mkoani Geita wakati wa uzinduzi wa kongamano la uzinduzi wa bomba la mafuta ghafi litakalojengwa kutoka Uganda mpaka Tanzania litakalogharimu kiasi cha USD 3.2.

Dkt. Kalemani amewataka Wakurugenzi wa EWURA pamoja TPDC kuweka matangazo yao ya kazi kwa lugha ya kiswahili ili kuepukana na changamoto ya wasiojua lugha ya Kiingereza.
Screenshot_20210811-042228_GBInsta.jpg
 
May 24,2021 Rais Samia Suluhu alikutana na kufanya mazungumzo na Mfanyabiashara Alhaji Aliko Dangote ambaye amewekeza katika kiwanda kikubwa cha uzalishaji wa saruji mkoani Mtwara na Dangote akaahidi kuwa kampuni yake ambayo imewekeza USD Milioni 770 (Tsh.Trilioni 1.761) nchini Tanzania, itaendelea kuwekeza katika maeneo mengine ikiwemo Mpango wake wa kujenga kiwanda cha kuzalisha mboleo.

Sasa habari njema ni kwamba tayari taratibu za ujenzi wa kiwanda hicho zimeanza na mapendekezo yanaonesha kitajengwa Mtwara pia kutokana na uwezekano mkubwa wa kupatikana kwa umeme wa gesi asilia.

Hayo yamebainishwa na Meneja Mawasiliano wa Dangote, Recho Singo wakati Naibu Waziri wa Madini, Prof. Shukrani Manya alipotembelea Kiwanda cha Saruji cha Dangote.

“Dangote alipoonana na Mama Samia waliongea kuhusu kuwekeza kwenye viwanda vingine hasa mbolea na wakashauri iwe Mtwara au Lindi na kwa mazungumzo yetu tumeona kwamba kiwanda hiki kinaweza kikajengwa Mtwara”———Recho
Screenshot_20210811-042401_GBInsta.jpg
Screenshot_20210811-042423_GBInsta.jpg
Screenshot_20210811-042447_GBInsta.jpg
 
Baada ya gumzo la tuhuma za Wapenzi wawili kufumaniwa wiki iliyopita lililofanya mpaka Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tanzania George Simbachawene kupiga marufuku mafumanizi ya aina hiyo na kusema wenye uhalali wa kushitaki fumanizi ni wenye vyeti vya ndoa peke yake na sio Hawara, wengine walihoji kuhusu Ndoa ziitwazo ndoa za 'Dhahania' ambazo hazina vyeti.

Mwanasheria Henry Mwinuka ameiambia AMPLIFAYA ya Clouds FM kwamba ndoa za Dhahania ni kitendo cha Wapenzi wawili kuishi chini ya dari moja kwa zaidi ya miaka miwili, hizi pia ni ndoa zinazotambulika kisheria na iwapo kutatokea swala la fumanizi basi mmoja wa Wapenzi hao atatakiwa kuwa na Mashahidi na Mjumbe wa nyumba kumi eneo la tukio ambapo hata hivyo hawatotakiwa kufanya chochote kwenye eneo la tukio baada ya kushuhudia bali kwenda Mahakamani kwa ajili ya madai ya fidia na kutenganishwa.

"Sheria ya ndoa ya mwaka 1971 ambayo imerejewa mwaka 2019 ukisoma kifungu cha 160 inazungumzia Dhahania ya ndoa na kinaeleza kwamba Watu wakikaa pamoja kinyumba kwa miaka miwili na kuendelea huku Majirani wakiwachukulia basi watachukuliwa kama Wanandoa" ——— Henry Mwinuka

"Sasa kwenye swala la fumanizi hamna ukinzani wowote, kimsingi kwenye mazingira hayo wewe utakaposhiriki nae jambo lolote la kimapenzi maana yake utakua unamuingilia Mtu mwingine kwenye ndoa hiyo, sasa yule aliyekufumania itakua ni wajibu wake kuthibitisha kwamba yule ni Mke/Mume wake na uthibitisho huo unatakiwa utolewe Mahakamani na sio kwa uliemfumania na Mpenzi wako" ——— Henry Mwinuka
Screenshot_20210811-042750_GBInsta.jpg
 
Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Dk Rashid Chuachua amepiga marufuku magari yanayofanya matangazo ya misiba jijini hapa baada ya kuchukua miili ya watu waliofariki dunia hospitalini, akisema yamekuwa yakileta hataruki kwa wananchi na kujenga hofu.

Chuachua amesema hayo leo Jumanne Agosti 10, 2021 huku akiiagiza Kamati ya Ulinzi na Usalama kufanya doria na kuwachukulia hatua wamiliki wa magari hayo watakaobainika.

"Kumekuwa na tabia ya familia za watu wanaopoteza maisha kukodi magari ya matangazo na kuanza kutangaza maeneo mbalimbali ya jiji na kutaja majina ya wapendwa wao, sasa kwa niaba ya mkuu wa mkoa nimepiga marufuku rasmi leo Agosti 10 2021,"amesema Dk Chuachua.
Screenshot_20210811-043443_GBInsta.jpg
 
TETESI| Jaribio la Al Ahly kumnasana winga wa Simba Luis Miquissone huenda likakwama. Wamebaki kimya baada ya kufikia ada ya uhamisho ya kiasi cha dola 900,000 za Marekani.

Ahly kwa sasa jicho lao wamelielekeza kwa winga wa Afrika Kusini Percy Tau.
Screenshot_20210811-043621_GBInsta.jpg
 
Wakati wapo Ibiza wanakula bata, wachezaji wa PSG walipiga picha na Lionel Messi

Neymar alipoipost akaandika AMIGOS, akimaanisha MARAFIKI na hatimae marafiki wamekutana Paris kwenye klabu ya PSG

Picha ilisema jambo, pesa za Muarabu ikatimiza jambo
Screenshot_20210811-044116_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom