Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20210810-075424_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20210810-075443_Opera%20Mini.jpg
 
Kabla ya PSG kuhitaji saini ya Lionel Messi ni tayari walikuwa wamevunja kanuni ya FFP yani Financial Fair Play ambayo iliwekwa na UEFA kusimamia matumizi yanayoendana na mapato

Kwenye kikao chao weekend iliyopita kati ya PSG, Kamati ya FFP na serikali ya Ufaransa, wakalegeza baadhi ya vifungu (Flexibility) ili kukamilisha dili hilo

Taarifa za kiuchunguzi zinadai kuwa UEFA wanapokea maelezo kutoka kwa FIFA kwakuwa Maboss wa PSG ni waarabu wa Qatar ambao ni wenyeji wa kombe la dunia 2022

Hivyo kanuni zitarejea tena kuanzia 2023, kama walivyokubaliana, kwa mujibu wa taarifa za ndani za kiuchunguzi

Huo ndio mpira wa dunia yetu
Screenshot_20210810-101442_GBInsta.jpg
 
Bado vikao vinaendelea Wanaume pichani hapo Rais wa Real Madrid, Florentine Perez, Rais wa Barcelona Joan Laporta na Rais wa Juventus, Andrea Agnelli

Bado wanaendeleza harakati zao za EUROPEAN SUPER LEAGUE, vikao vinaendelea jijini Barcelona
Screenshot_20210810-101602_GBInsta.jpg
 
Kuanzia leo saa tano asubuhi mpaka masaa 48 yajayo Lionel Messi atatangazwa rasmi na PSG kuwa mchezaji wao

Kilichosalia ni Messi na ujumbe wake kupitia mkataba wake vyema kisha kusaini na mpaka sasa ni 80% tayari

Taarifa za Messi kurejea tena Barcelona hazina ukweli wowote
Screenshot_20210810-101714_GBInsta.jpg
 
Shikhalo aaga Yanga
.
"Imekua miaka miwili kamili tangia nijiunge na timu ya wananchi Yanga Sc.Ningependa kutoa shukrani zangu za dhati kwa mashabiki ambao wamekua sehumu kubwa ya maisha yangu tangu nijiunge na timu hii.

Hakika mmesimama na mm katika kipindi kigumu na mmenivumilia kwa mengi na kunipa sapoti yenu na motisha ili niendele kuipambania timu.

Ningependa pia kuwashkuru viongozi wote makocha na wachezaji wote amboa nimebahatika kufanya nao kazi hapa yanga.

Bila kusahau nitoe shukrani zangu pia kwa Kabwili na Metacha ambao tumepeana competition nzuri na kujifua nao kwa miaka hii miwili ndani ya club hii pendwa .Kwa sasa niseme kwaherini wananchi,ila mtabakia kua ndani ya moyo wangu siku zote.
Screenshot_20210810-101849_GBInsta.jpg
 
KUMBE KANE KESHAMALIZANA
.
Lisemwalo lipo Na kwenye hilo ni kwamba straika Harry Kane ameshamalizana na Manchester City juu ya makubaliano binafsi wakati huu akijiandaa kuachana na Tottenham Hotspur
.
Kane, 28, bado anafukuzia taji lake la kwanza kwenye maisha ya soka na jambo hilo ndilo linalotajwa kuwa sababu kubwa itakayomwondoa Spurs, mahali ambalo alizua utata siku za karibuni baada ya kukosekana mazoezini kwa wiki nzima.
.
Ripoti zinafichua kwamba mwenyekiti wa Spurs, Daniel Levy ambaye amekuwa akiweka ngumu kwenye kukubali kumuuza mshambuliaji huyo, sasa amelegeza msimamo wake na kwamba amekubali ofa ya Pauni milioni 120 pamoja na nyongeza nyingine ya Pauni 20 milioni ili kukamilisha dili hilo.
.
Kwa mujibu wa mwandishi wa habari, Ian McGarry amesema: “Harry Kane ni ameshakubaliana mambo binafsi na Man City na kinachosubiriwa ni Daniel Levy kukubali ada ya uhamisho.”
Screenshot_20210810-102201_GBInsta.jpg
 
Ducapel Moloco Jesus YANGA SC
.
Yanga imemalizana na winga Mkongomani Ducapel Moloko Jesus ambaye anakuja kuwa mbadala wa Tuisila Kisinda.
.
Kisinda muda wowote kuanzia sasa atasaini mkataba wa kujiunga na Berkane ya Morocco inayonolewa na kocha Florent Ibenge.
.
Moloko ndiye aliyeziba pengo la Kisinda alipoondoka AS Vita na habari zinasema Mukoko Tonombe ndiye amehusika kumpendekeza.
Screenshot_20210810-102307_GBInsta.jpg
 
Kadina Kabangu SIMBA SC
.
Simba wako kwenye hatua nzuri ya mazungumzo na straika wa DC Motema Pembe, Kadina Kabangu.
.
Simba ambao jana walifanya vipimo vya afya kwenye hospitali ya Taifa ya Muhimbili wanamchukua mchezaji huyo kama mbadala wa Meddie Kagere ambaye safari imemkuta.
.
Simba wanaamini fiziki na uwezo wa kufunga wa mchezaji huyo utawabeba kwenye michuano ya kimataifa inayoanza Septemba 11 mwaka huu.
.
Habari zinasema kwamba Simba pia huenda ikamuuza straika wake, Chris Mugalu muda wowote kama dili lao na Berkane litakubalika.
Screenshot_20210810-102442_GBInsta.jpg
 
Ukonde apigwa chini Yanga
.
Uongozi wa klabu ya Yanga umempa mkono wa kwaheri kiungo mshambuliaji wa UD Songo, Jimmy Ukonde baada ya kushindwa kuonyesha uwezo waliokuwa wanautegemea.
.
Mmoja wa viongozi wa Yanga ametudokeza kwamba wamegundua kiwango chake ni cha kawaida.
.
“Ukonde anaondoka leo hatakuwa miongoni mwa nyota tunaotarajia kuwa nao msimu ujao kwa lengo la kuona tunaonyesha ushindani ligi ya ndani na kimataifa, ni mchezaji mzuri lakini hafiti mahitaji ya kocha,” alisema.
Screenshot_20210810-102802_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom