Makapuku Forum

Makapuku Forum

Yanga imeachana na Golikipa Mkenya FARUK SHIKHALO baada ya mkataba wake kumalizika, kwa mujibu wa Kaimu Katibu Mkuu wa Klabu hiyo Haji Mfikirwa amesema, wamezingatia mapendekezo ya mwalimu.
Screenshot_20210809-185339_GBInsta.jpg
 
WACHEZAJI WAANZA KUREJEA MSIMBAZI

Wachezaji wa Simba PERFECT CHIKWENDE na CLATOUS CHAMA wamesharejea ncchini kama alivyoagiza kocha wa timu hiyo Didier Gomes ambaye anataka kuanza maandalizi ya msimu ujao.

Simba inatarajia kwenda nchini Morocco kuweka kambi ya maandalizi kuelekea msimu ujao wa mashindano.
Screenshot_20210809-185732_GBInsta.jpg
 
Klabu ya RS Berkane ya Morocco inayofudishwa na Kocha Florent Ibenge imetuma ofa kwa klabu ya Yanga kwa ajili ya kumsajili winga Tuisila Kisinda.

Tayari nyota huyo ambaye yupo mapumziko nchini kwao DR Congo amepata VIZA ya mwezi mmoja (August 06 -September 06) kwenda nchini Morocco kukamilisha usajili huo.
Screenshot_20210809-190058_GBInsta.jpg
 
Sadio Kanoute "fundi" SIMBA SC
.
Kiungo wa timu ya Taifa ya Mali na klabu ya Al Ahly Bengazi ya Libya, Sadio Kanoute yuko mbioni kutua Simba SC ili kuja kuongeza nguvu katika eneo la kiungo.
.
Kanoute ana mkataba wa miaka mitatu na Al Ahly Bengazi hivyo Simba watalazimika kuvunja mkataba wake.
Screenshot_20210809-190229_GBInsta.jpg
 
ABDI BANDA SIMBA, YANGA, AZAM
.
Aliyekuwa beki wa Highland Park na Baroka za Afrika Kusini, Abdi Banda anahusishwa huenda msimu ujao akacheza Ligi Kuu Bara.
.
Zipo tetesi amefikia makubaliano na moja ya vigogo wa soka la nchini, watu wake wa karibu wamethibitisha hilo.
Screenshot_20210809-190748_GBInsta.jpg
 
Rekodi Simba balaa Yanga
.
Kipigo cha mabao 3-1 ilichopewa Yanga na Express ya Uganda juzi kwenye mechi ya mwisho ya Kundi A, imeifanya Yanga kuendelea kuteseka kuifikia rekodi ya Simba katika michuano ya Kombe la Kagame.
.
Yanga iliyotwaa taji la michuano hiyo mara TANO, imeng’olewa na kushindwa kutimiza ndoto za kuifikia idadi ya mataji waliyotwaa watani wao, Simba iliyo kinara kwa kulibeba mara SITA tangu 1974.
.
Jangwani walionekana wana nafasi kubwa baada ya Simba kujitoa kushiriki na kusalia kama moja ya timu iliyobeba mara nyingi taji hilo, lakini kutumia kikosi cha vijana na wale wasio na nafasi kikosi cha kwanza pamoja na wale wapya iliyowasajili iliwafanya watoke michuanoni wakiwa na alama mbili.
Screenshot_20210809-191042_GBInsta.jpg
 
Jangwani inogile, Sasa ni zamu ya Bangala
.
Yanga wamerudi nchini DR Congo na sasa wanataka tena kuchukua beki mwingine na matajiri wa GSM wako katika hatua za mwisho kabisa kumleta beki Yannick Bangala Litombo.
.
Yanga imeshamalizana kila kitu katika makubaliano na Bangala ambaye wakati wowote wiki hii atawasili nchini kuja kusaini mkataba na klabu hiyo kongwe.
.
Bangala sasa anakuja kuchukua nafasi ya Mghana na aliyekuwa nahodha wa timu hiyo Lamine Moro ambaye amesitishiwa mkataba baada ya makubaliano ya pande zote mbili.
.
Screenshot_20210809-191213_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom