GREALISH NI SUALA LA MUDA TU ETIHAD
.
Staa Jack Grealish yupo kwenye hatua za mwisho kabisa za kukamilisha uhamisho wake wa rekodi kwenye Ligi Kuu England kwa kujiunga na Manchester City kwa ada ya Pauni milioni 100 (Sh 323 Bilioni)
.
Na kila kitu kinaonekana kuwa kwenye hali nzuri ambapo kwa taarifa za mtaalamu Fabrizio, Grealish atafanyiwa vipimo vya Afya hii leo Alhamisi.
.
Grealish anaenda kuvunja rekodi ya Paul Pogba ya kuwa mchezaji ghali zaidi kwenye Ligi Kuu England, wakati aliponaswa kwa Pauni milioni 89 na Manchester United kutoka Juventus mwaka 2016.
.
View attachment 1880467