Makapuku Forum

Makapuku Forum

Hennock Inonga Varane Simba
.
Kwa lugha za kwenye vibanda umiza ni kwamba Yanga wamebipu, Simba wamepiga.
.
Kitendo cha Yanga juzi kutishia kwamba wamemsajili Peter Banda kiliwakera mabosi wa Simba na wakaapa kuwa watapiga kwenye mshono.
.
Sasa usiku wa kuamkia jana wamemshusha nchini beki Mkongoman, Hennock Inonga ‘Varane'ambaye Yanga walishamtumia kila kitu mpaka tiketi, malipo ya cheti cha corona ili aje Dar atue Jangwani.
.
Simba ilikuwa ikiwinda beki mzoefu kwani matarajio yao ni kufanya vyema katika Ligi ya Mabingwa inayoanza mwezi ujao Septemba na hapo imemnasa Inonga ambaye alikuwa nahodha wa DC Motema Pembe na timu ya taifa ya DR Congo kwa wachezaji wa ndani.
.

Screenshot_20210806-113058_GBInsta.jpg
 
Yanick Bangala Litombo YANGA SC
.
Baada ya beki Mkongomani, Henock Inonga kuingia tamaa na kusaini Simba, Yanga wamebadili gia haraka na kutua kwa kifaa kingine.
.
Ni beki mahiri wa zamani wa AS Vita, Yanick Bangala Litombo anayekipiga kwa sasa anakipiga klabu ya FAR Rabat ya Morocco iliyoko chini ya kocha wa zamani wa Simba, Mbelgiji Sven Vandebroeck.
.
Inaelezwa kwamba staa huyo hafurahii maisha Morocco na amemwambia meneja wake ambaye pia ni meneja wa Fiston Mayele na Juma Shabani kwamba mambo yakikaa sawa anakuja Dar kujiunga na Yanga.
.
Akitua Yanga Wakongomani watakuwa SITA Jangwani
Screenshot_20210806-113312_GBInsta.jpg
 
Bai Bai Lionel Messi
.
Barcelona wathibitisha Lionel Messi anaondoka
.
Barcelona wametangaza kuwa wanalazimika kumuachia Messi aondoke kwa sababu ya sheria za matumizi ya kifedha kwa vilabu vya LaLiga.
.
PSG na Man City zinapewa nafasi kubwa ya kumnasa Messi.
.
Screenshot_20210806-113607_GBInsta.jpg
 
Tayari Mwili wa aliyekua Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Elias John Kwandikwa (MB) umewasili katika viwanja vya Karimjee kwaajili ya Misa na kuagwa.
RIPKwandikwa
Screenshot_20210806-144551_GBInsta.jpg
Screenshot_20210806-144754_GBInsta.jpg
 
“Niliondoka kwenda Rwanda nikiwa nafahamu namuacha Kwandikwa akiwa anaugua ila sikuwa nafikiria kabisa kama nitapata taarifa za kifo chake, nilipata taarifa kwamba amefariki nikiwa na Kagame na amenituma nitoe pole kwa Serikali ya Tanzania na Watanzania wote kufuatia msiba huu”

“Msiba wa Kwandikwa umeacha pengo sio tu kwa Familia bali pia Serikalini, alikuwa msikivu,mtulivu asiye na makuu, sifa hizo na nyingine zilitusukuma Mimi na Hayati Magufuli kumpa dhamana ya kuwa Naibu Waziri wa Ujenzi mwaka 2017 na baadaye Waziri wa Ulinzi mwaka 2020”

“Sifa za Kwandikwa (za usikivu, utulivu, kutokuwa na makuu na nyingine) zilifanya niendelee kumuamini na kuendelea kumpa dhamana ya kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa”———-Rais Samia wakati wa kuuaga mwili wa Kwandikwa, Karimjee leo
RIPKwandikwa
Screenshot_20210806-144940_GBInsta.jpg
 
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na wenzake wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo kwa ajili ya kesi inayowakabili ya mashitaka mawili ikiwemo tuhuma za Ugaidi.

Itakumbukwa jana August 5, 2021 kesi hiyo ambayo upelelezi umekamilika ilishindwa kuendelea mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kutokana na changamoto ya kimtandao wakati ilipotaka kuendeshwa njia ya mtandao (Video Conference).
Screenshot_20210806-145144_GBInsta.jpg
 
Kiongozi Mkuu wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ni miongoni mwa Watu waliofika Mahakama ya Kisutu muda huu kufuatilia mwenendo wa kesi ya ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe.
Screenshot_20210806-145307_GBInsta.jpg
Screenshot_20210806-145332_GBInsta.jpg
 
Kutoka Mahakama ya Kisutu leo inatajwa kesi ya ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe baada ya kushindwa kuendeshwa jana kutokana na hitilafu za kimtandao, tayari Mbowe amefikishwa Mahakamani na hali ya ulinzi na usalama imeendelea kuimarishwa.
Screenshot_20210806-145453_GBInsta.jpg
 
Kesi ya Uhujumu Uchumi na Ugaidi inayomkabil Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe imeahirishwa hadi August 13, 2021 kwa ajili ya upande wa mashitaka kuwasilisha taarifa za kesi hiyo kutoka Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP).

Mbowe na wenzake watatu wamesomewa upya mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba ambayo ni kula njama na tuhuma za Ugaidi ambayo waliyatenda kati ya Mei 1 na August 1, 2020 maeneo ya Moshi, Dar es Salaam, Morogoro na Arusha.

Mbowe alifikishwa Mahakamani kwa mara ya kwanza July 26, 2021.
Screenshot_20210806-145720_GBInsta.jpg
 
Rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma amelazwa Hospitali ya kijeshi iliyopo nje ya Gereza kwa ajili ya uangalizi wa matibabu, Mamlaka inayosimamia Magereza nchini humo imethibitisha.

Zuma kwa sasa anatumikia kifungo cha miezi 15 jela tangu July mwaka huu, kwa kukaidi amri ya Mahakama.
Screenshot_20210806-183326_GBInsta.jpg
 
Ofisi ya Rais- TAMISEMI imesema na kitendo cha Watumishi wawili Mwalimu Omary Kwesiga , Mkuu wa Idara Elimu Msingi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha na Scolastica Kanje, Afisa Muuguzi Msaidizi Hospitali ya Mkoa wa Arusha kufanya igizo kwenye zoezi la chanjo ya Covid-19 kinyume cha taratibu na kanuni za utoaji wa chanjo hivyo kuleta sintofahamu kwa Wananchi kuhusu zoezi la chanjo linaloendelea nchini kote .

Kufuatia hali hiyo, Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu amemuagiza Katibu Mkuu OR-TAMISEMI kumsimamisha kazi Mwalimu Omary Kwesiga, ameagiza pia Scolastica apelekwe kwenye Baraza la Wauguzi na Wakunga kwa hatua zaidi.
Screenshot_20210806-183511_GBInsta.jpg
 
INASEMEKANA Haji manara

Anahamia Azam fc Na Hii ni Kwa Sababu Club inahitaji BOOST kibiashara

Kapewa Gari KALI na Nyumba ( Sio Yakupanga , YAKEEEE

-Mshahara MNONO BALAA

Nimepita Sehemu Nikakuta watu wanasema Haji manara NI KAMA CHURA ALIEPIGWA TEKE

Screenshot_20210806-185102_GBInsta.jpg
 
INASEMEKANA Haji manara

Anahamia Azam fc Na Hii ni Kwa Sababu Club inahitaji BOOST kibiashara

Kapewa Gari KALI na Nyumba ( Sio Yakupanga , YAKEEEE

-Mshahara MNONO BALAA

Nimepita Sehemu Nikakuta watu wanasema Haji manara NI KAMA CHURA ALIEPIGWA TEKE

View attachment 1883064
Awasalimie Aliikuta Simba na itazidi Kung'aa yaani Mimi Manara nilikua nampenda ila kwa sasa namtenganisha na Simba.Sihami Simba nimeanza kuipenda mwaka 1992 kama sikosei sitaacha kuipenda...!!!anatutingisha siyee
 
Carlos Carlinhos Sagrada Esperanca
.
Mabingwa wa Angola, Sagrada Esperanca wamemtambulisha aliyekuwa kiungo wa Yanga, Carlos Carlinhos Stenio Fernandes Guimaraes do Carmo.
.
Carlinhos mwenye umri wa mika (26) amejiunga kwa uhamisho wa bure.
Screenshot_20210806-201916_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom