Makapuku Forum

Aliyekua DC wa Hai Lengai Ole Sabaya pamoja na wenzake wamefikishwa kwenye Mahakama ya Wilaya iliyopo Sekei Arusha, kwa sasa yupo chumba cha Mahabusu Mahakamani hapa kabla ya kupandishwa kizimbani wakati wowote kuanzia sasa ili kujibu tuhuma zinazowakabili tutakufahamisha zaidi.
 
Mjadala wa kutaka jina la Nchi ya Nigeria libadilishwe umeendelea kuwa gumzo nchini humo wakati huu ambapo Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wanaendelea kukusanya mapendekezo ya kubadili Katiba, hii ni baada ya Raia mmoja aitwaye Adeleye Jokotoye kupendekeza jina la Nchi hiyo kuwa United African Republic (Jamhuri ya Muungano Afrika).

Jokotoye amesema sababu ya kuomba jina lirudiwe kupitishwa upya ni kwakuwa jina hilo ni la Kikoloni ambalo wakati linapitishwa yeye hakuwepo halikupendekezwa kwa matakwa ya Wanaigeria ila llilipendekezwa karne ya 19 na Mwandishi wa Habari wa Uingereza, Flora Shaw, ambaye baadaye aliolewa na Msimamizi wa Kikoloni, Frederick Lugard.

Bashir Ahmad ambaye ni Msaidizi wa Rais wa Nigeria amesema anashangazwa kuona Watu wameanza kumtupia lawama Rais Muhammadu Buhari wa Nchi hiyo kuhusu mapendekezo hayo wakati aliyependekeza ni Raia na wala sio Rais wala sio Serikali.
 
Dereva mmoja wa Newton Marekani ameilaumu App ya GPS kwa kumdanganya njia na kujikuta kapanda kwenye mwinuko nje ya barabara baada ya App hiyo kumuonesha njia ipo hapo na panapitika.

Polisi wamesema β€”β€”β€”> β€œhakuwa amelewa, anailaumu GPS kwani ndio alikua anaifata kumuongoza njia, hii sio kawaida… hata kama mnatumia gps tumieni na macho pia”

Msemaji wa Polisi amesema toka ameanza kufanya kazi Polisi miaka 37 iliyopita hajawahi kukutana na tukio kama hili ambapo hata hivyo amesema Dereva huyu hatoshtakiwa wala kutozwa faini yoyote kwa kilichotokea.
 
Za kuambiwa changanya na za kwako...
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…