Makapuku Forum

Makapuku Forum

Hizi ni picha za Mkuu wa zamani wa Majeshi wa Uganda Jenerali Katumba akiwa na Mtoto wake aitwae Brenda kabla ya kifo chake leo, Brenda amefariki leo baada ya Watu wasiojulikana kulishambulia kwa risasi gari walilokuwemo ambapo pia Dereva naye amefariki, Jenerali Katumba amejeruhiwa na amelazwa Hospitali.

“Brenda amerudi hivi karibuni kutoka Marekani ambako amehitimu masomo yake, inaumiza sana sijui Serikali itafanya nini kuhusu tukio hili maana Katumba hajafanya lolote baya kustahili mateso haya”———Joyce Sentongo, Ndugu wa Katumba.

Jenerali Katumba Wamala ambaye amekuwa Waziri wa uchukuzi na ujenzi kwenye Serikali ya Rais Yoweri Museveni ya muhula wa tano anatambulika kama Mtu asiyependa makuu na hatembei na msafara wa Walinzi kama wenzake walio kwenye ngazi za juu za Serikali. View attachment 1805011View attachment 1805012View attachment 1805013View attachment 1805014
......ukiwa na nguvu, mamlaka au uwezo tenda haki. Ukionea kisasi hakilipwi kwako tu, kinawafuata na walio karibu yako, ushuhudie akili ikuingie
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom