Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,971
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimechukizwa na kulaani kitendo kilichofanywa na baadhi ya Viongozi wa UWT Mkoa wa Arusha wakiongozwa na Mbunge wa Viti Maalum Catherine Magige.
“CCM inaamini katika kujenga uimara wa familia, kuheshimiana ndani ya jamii na kuendeleza upendo katika familia halali badala ya mivutano na uvurugaji usiokuwa na sababu, Chama kinatafakari kwa undani kwa mujibu wa kanuni za maadili na Katiba ya CCM, na kuchunguza kwa kina ili kuchukua hatua za kimaadili kwa wote watakaothibitika kuwa sehemu ya matukio yaliyokiuka katiba, kanuni na utamaduni wa kuheshimu na kuheshimiana uliojengeka ndani ya CCM” ——— Shaka Hamdu Shaka, Katibu wa Halmshauri Kuu ya Taifa Itikadi na Uenezi.
Kauli hii ya CCM imetolewa saa chache baada ya vurugu kutokea kwenye mazishi ya Mfanyabiashara Kuzola Madoda wa Arusha ambako Mbunge Magige alizuiwa geitini wakati akitaka kuingia katika eneo la maziko.
“CCM inaamini katika kujenga uimara wa familia, kuheshimiana ndani ya jamii na kuendeleza upendo katika familia halali badala ya mivutano na uvurugaji usiokuwa na sababu, Chama kinatafakari kwa undani kwa mujibu wa kanuni za maadili na Katiba ya CCM, na kuchunguza kwa kina ili kuchukua hatua za kimaadili kwa wote watakaothibitika kuwa sehemu ya matukio yaliyokiuka katiba, kanuni na utamaduni wa kuheshimu na kuheshimiana uliojengeka ndani ya CCM” ——— Shaka Hamdu Shaka, Katibu wa Halmshauri Kuu ya Taifa Itikadi na Uenezi.
Kauli hii ya CCM imetolewa saa chache baada ya vurugu kutokea kwenye mazishi ya Mfanyabiashara Kuzola Madoda wa Arusha ambako Mbunge Magige alizuiwa geitini wakati akitaka kuingia katika eneo la maziko.