Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,971
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara Longinus Tibishimwamu amethibitisha kifo cha Askari Polisi mmoja aliyekua doria ya kawaida kando ya Ziwa Victoria Mwalo wa Makoko, Kata ya Makoko Mkoani humo.
Kifo cha Askari huyo kilitokea wakati akipambana na Mhalifu aliyekimbilia kwenye maji ziwani ambapo RPC Tibishimwamu amesema Muhalifu huyo inadaiwa alikuwa Mvuvi haramu na sio Jambazi kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari.
“Askari huyo alimfuata ndani ya maji ili kumkamata alipojaribu kukimbia, bahati mbaya Askari akanaswa na nyavu ya samaki na kupeleka kifo chake” ——— RPC Tibishimwamu.
Kifo cha Askari huyo kilitokea wakati akipambana na Mhalifu aliyekimbilia kwenye maji ziwani ambapo RPC Tibishimwamu amesema Muhalifu huyo inadaiwa alikuwa Mvuvi haramu na sio Jambazi kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari.
“Askari huyo alimfuata ndani ya maji ili kumkamata alipojaribu kukimbia, bahati mbaya Askari akanaswa na nyavu ya samaki na kupeleka kifo chake” ——— RPC Tibishimwamu.
