Makapuku Forum

Makapuku Forum

20210527_153030.jpg
 
Kama haukua unafahamu, Kocha wa Villarreal Unai Emery ambae usiku wa kuamkia leo ameondoka na ushindi wa Europa League kwa kuishinda Manchester United kwenye matuta, amecheza fainali tano za Europa League na kushinda nne, alipoteza moja 2018/2019 akiwa na Arsenal.
20210527_154209.jpg
 
"Sio Wachagga wala sio Wasukuma, wala sio Wamasai wala sio Wameru, tunataka Watanzania wa makabila yote tukaishi kama Ndugu, kila kabila likawe na haki ya kula keki ya Nchi yetu, tusiingize siasa za kipumbavu za kikabila zilizopitwa na wakati, tunamwambia Mama Samia na Chama chake cha CCM, Chama cha Mapinduzi kijirekebishe, kisiruhusu siasa na sera za kikabila kwa kabila lolote Nchi hii" ——— Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe sasa akiwa Arusha.
20210527_154404.jpg
 
"Hatutashiriki Uchaguzi wa Udiwani, Ubunge au Urais hadi tutakapokuwa na Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya na hatusemi tunakwenda kulala tukisubiri vishuke kama maji tutavipigania kuanzia leo kwa nguvu zetu zote” ——— Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe akiongea sasa hivi Arusha.
20210527_154534.jpg
 
"Kama kuna baadhi ya Watu iliwapendeza kuwatesa Watanzania wenzao, CHADEMA tukarejeshe tumaini kwa Watu wote, Tanzania tukaongoze safari ya kurejesha utengemano wa Taifa, tukaongoze mapambano ya kuirejesha haki katika Nchi yetu, tukarejeshe utawala wa kisheria na kikatiba katika taifa letu na kamwe tusimruhusu Kiongozi mwingine yeyote tena aligeuze Taifa letu shamba lake la kuliendesha anavyotaka" - Freeman Mbowe leo Arusha.
20210527_154726.jpg
 
"Tunakuomba Rais Samia katengeneze amani na suluhu ya Taifa hili, mioyo ya Watu inavuja damu, msione aibu kuomba radhi pale mlipowakosea Watu, tunatambua kwenye Serikali yako Mama Samia wako wale Mawakala waliotumika kutesa Watanzania”

“Tunasikia kauli zako za kurejesha matumaini lakini haitoshi kwasababu unafahamu kwa miaka mitano mlibadilisha kanuni, sheria ili kuminya uhuru wa Vyombo vya Habari, uhuru wa Vyama vya siasa, Demokrasia, kuminya haki za Biashara, kuwatesa Wafanyabiashara wetu kwa kupitia kodi”

“Mama Samia kabla sijakutana na wewe na Viongozi wenzangu wa CHADEMA anza kuwekeni utaratibu wa kulitengamanisha Taifa kwa kurekebisha sheria zote ambazo ni kandamizi zinawaumiza Watanzania ili tukafanye ushindani wa haki na iwe haki kwa Watu wote"

"Nawaomba CHADEMA Watanzania wengi mna hasira na mnatamani kulipiza kisasi, Mimi kama Kiongozi wenu nasema, siku ambayo mtageuka kuwa Chama cha kulipiza visasi kwanza niondoeni Mbowe kama Mwenyekiti kwasababu siwezi kuwa Mwenyekiti wa Visasi, lazima tumuweke Mungu kwenye Uongozi wetu na Mungu ametuambia tusiwe Watu wa visasi” ——— Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe akiwa Arusha leo.
20210527_154820.jpg
 
Chama cha Soka Ulaya (Uefa) jana Jumatano kimemtoza faini ya Euro 50,000 (sawa na Sh141.7 za Kitanzania) mwanasoka nyota wa Sweden, Zlatan Ibrahimovic baada ya kubaini kuwa ana maslahi ya kifedha na kampuni inayoendesha michezo ya kubashiri matokeo, chama hicho kimetangaza.

Rais wa kamati ya rufaa ya UEFA pia ameagiza mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 39 anayechezea AC Milan aache kujihusisha na tovuti inayoendesha michezo hiyo ya kubeti.
Kujihusisha kwake kumechukuliwa kuwa kunakiuka kanuni za UEFA za "uadilifu katika mechi na mashindano".
20210527_155453.jpg
 
Zinedine Zidane amejiuzulu kazi ya ukocha wa Real Madrid, kwa mujibu wa vyombo vya habari, baada ya kuvuliwa ubingwa wa soka wa Hispania na Atletico Madrid.

Taarifa za kuondoka kwa Mfaransa huyo zimekuja mwishoni mwa kampeni iliyokuwa mbaya kwa vigogo hao ambao wametwaa ubingwa wa Ulaya mara 13, baada ya kuondolewa katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya na Chelsea katika nusu fainali na hivyo kumaliza msimu kwa mara ya kwanza katika miaka 11 bila ya kombe lolote.
20210527_155554.jpg
 
“Baada ya kupokea Simu na Jumbe mbalimbali nimeona nitumie nafasi hii kuweka kumbukizi sawa. Mzee wetu na Mzazi wetu Dr. Mrisho Jakaya Kikwete yupo salama wa Afya Nyingi sana. Hana tatizo lolote kiafya na anaendelea na majukumu yake. Taarifa za aina yeyote ni za Kipuuzi na za kupuuzwa.”
20210527_155714.jpg
 
Leo Alhamisi Mei 27, 2021 Emmanuel Macron amekuwa rais wa kwanza wa Ufaransa kuhutubia katika kumbukumbu ya mauaji ya kimbari nchini Rwanda yaliyotokea mwaka 1994.

Pichani ni Macron akiwa na mwenyeji wake, Paul Kagame ambaye ni rais wa Rwanda baada ya kuwasili mjini Kigali. AFP
20210527_161748.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom