Makapuku Forum

Joseph Michael Palmer aliyeishi kuanzia miaka ya 1789 hadi 1873, alikuwa ni mtu ambae ana mandevu mengi sanaa kama anavyoonekana pichani.

Sasa bwana watu wa kijiji alichokua anaishi walikua wanachukia sana ndevu zake kipindi iko fashion ya kufuga ndevu nyingi haikuwepo, mara kwa mara walikua wanamwambia anyoe lakini alikataa. Wengine walikua wanamwambia kama hataki kunyoa basi wasimuone mtaani kwasababu anatisha kama shetani.

Siku moja mwaka 1830, Wanaume wanne wakiwa na mkasi na wembe walimvamia Palmer nje ya hoteli ya Fitchburg na kujaribu kutaka kumnyoa ndevu zake. Palmer alifanikiwa kujitetea dhidi ya watu hao.

Katika pulukushani za kujitetea Palmer aliwajeruhi miguuni wawili miongoni mwa wavamizi wale. Kwa kitendo icho Palmer, alishtakiwa kwa "shambulio lisilokuwa na sababu",

Palmer alishtakiwa siku chache baadaye mbele ya Jaji David Brigham na kupigwa faini. Palmer alikataa kulipa faini ambayo ilitokana na kuhukumiwa kwake kwa uhalifu wa kujitetea. Palmer alitupwa jela kwa zaidi ya mwaka mmoja kwa kukataa kulipa faini hiyo.
 
Kama ulikua haufahamu ndo ilikua hivi Sasa

Huko Uingereza, katikati ya miaka ya 1960 kabla ya kuwepo kifaa cha kupimia mimba, vipimo vya ujauzito vilifanywa kwa kuingiza mkojo wa mwanawake kwa chura na kuangalia ikiwa kama atataga mayai ndani ya masaa kumi na mbili. Kama akifanikiwa kutaga basi mwanamke mwenye huo mkojo ana mimba.
Yote hii ilifanyika katika maabara.

Kipimo cha kwanza cha upimaji wa ujauzito kilitengenezwa mnamo mwaka 1971 ambacho mwanamke angeweza kupima mkojo wake mwenyewe na kungoja kwa masaa mawili ili kuthibitisha.

NaddySL njoo uone huku
 
Mwanasaikolojia Winthrop Niles Kellong na mkewe, katika miaka ya 1930 walichukua mtoto wa sokwe na kujaribu kumlea pamoja na mtoto wao wa kiume, Donald, ili kuona kama hii inaweza ikasababisha sokwe kujifunza tabia za kibinadamu.

Baada ya miezi tisa, walisitisha jaribio lao kwa sababu mtoto wao alianza kufanya matendo kama sokwe.
 
Mwaka 2019, Elizabeth Hoad, mwanamke wa Uingereza mwenye umri wa miaka 49, aliolewa na mbwa wake.

Alielezea kuwa alifikia uhamuzi huo baada ya kuchumbiwa mara nne na kujihusisha kwenye mapenzi na wanaume 220 bila kuolewa. Hivyo amechoshwa na binadamu (waanaume) na kuamua kuolewa na mbwa wake aliyefahamika kwa jina la Logan.

Kwa upande wake anaona kuolewa na mbwa wake amejiokoa yeye pamoja na mbwa kutoka kwenye upweke.
 
Tim Friede, mwanasayansi kutoka Wisconsin, Marekani.

Huyu ni binadamu asiyedhulika na sumu ya nyoka wa aina yoyote. Ameng'atwa na nyoka wa aina tofauti tofauti zaidi ya mara 200 katika miaka 20. Amevumilia hata kuumwa na Black Mamba wa Kusini mwa Jangwa la Sahara, ambae inaaminika ni miongoni mwa nyoka wenye sumu kali zaidi duniani.
 
Mwaka 2019, wakati jiji la Bhopal, India, lilipokumbwa na ukame, makuhani wa huko waliwafungisha vyura wawili ndoa ili kumuomba Mungu wa mvua awape mvua.

Kwa bahati mbaya, ndoa ya vyura hao ililazimika kuvunjwa miezi michache baadaye ili kuzuia mvua kuendelea kwa sababu ya mvua kubwa iliyoendelea kunyesha ambayo ilisababisha uharibifu wa nyumba zaidi ya 9,000
 
Simulizi maarufu kutoka katika kabila la Kamba nchini Kenya, kuhusu asili ya Tembo, Wakamba wanasema kwamba Tembo awali walikuwa binadamu.

Katika simulizi hiyo wanasema mtu masikini alisikia kuna tajiri mkarimu aliyeitwa Ivonya-Ngia (Yeye anayewalisha Masikini), alianza kugundua siri ya kuwa tajiri, aliamua kufunga safari kwenda kumuona.

Baada ya safari ndefu, yule maskini alifika kwenye jumba zuri lenye kuzungukwa na malisho mabichi na mifugo mingi ya ng'ombe na kondoo. Ivonya-Ngia alimpatia maskini kondoo mia moja na ng'ombe mia moja, lakini yule maskini alikataa, hakutaka misaada bali alitaka kujua siri ya Ivonya-Ngia ya kufanikiwa kuwa tajiri. Kwa hivyo Ivonya-Ngia alimpa mtu huyo maskini marashi (dawa ya kupaka) na kumwambia ampake mkewe kwenye meno.

Mtu masikini alirudi nyumbani na kumshawishi mkewe wafanye hivyo ili wawe matajiri, mkewe akakubali. Baada kupaka meno yake yalianza kuwa makubwa na urefu wa mkono wa mtu ( hapa nadhani wanazungumzia mfanano sawa na pembe za ndovu). Maskini alianza kuyang'oa meno yale na kuyauza, akawa anaendelea kufanya hivyo mara kwa mara.

Siku moja meno ya mkewe yalipokua tena, alikataa kumruhusu mumewe kuyang'oa, alimkimbia mumewe na kwenda porini na mwishowe mwili wake wote ulibadilika, ulikua na kubadilika rangi, mpaka akabadilika kuwa tembo. Alizurura msitu ambapo badae alizaa watoto ambao ndio walikua uzao wa Kwanza wa tembo.
 
Huko nchini Scotland katika miaka ya 1500's - 1600's kulikuwa na mtu hatari sana aliyejulikana kama Alexander "Sawney" Bean. Maisha aliyokuwa anaishi huyu jamaa ni ya kutisha haijawahi tokea, alikuwa anamiliki watu, yaani kama jinsi watu wanavyomiliki mifugo kama kuku, n'gombe au mbuzi basi ndivyo jamaa naye alivyokuwa anamiliki watu.

Nikizungumzia watu katili niliowahi kuskia simulizi zao hapa duniani, basi huyu jamaa nimemvulia kofia. Bean alikufa kwa kunyongwa kutokana na makosa ya kuwafanya binadamu wenzake nyama huku akiwa ameacha jumla ya watoto 29.

Kwa zaidi ya miaka 25 aliyaishi maisha hayo ya kinyama mapangoni mjini East Lothian. Alikuwa ameshawafanya nyama watu zaidi ya 5,000 na wengine bado walikutwa amewafungia.

Baada ya Bean kuhama nyumbani alienda kuishi mapangoni na mkewe Agnes Douglas huko Bennane Head nchini humo ambako katika maisha yao walifanikiwa kupata watoto sita, baadaye familia ikakua na kufika wanafamilia 45, hakuna aliyekua anajua mapangoni humo kama kuna watu wanaishi.

Yeye pamoja na wanawe walianza kuteka watu, wanawafungia mapangoni humo alafu wanawachinja na kuwala nyama kama jinsi tunavyokula mifugo yetu nyumbani. Mabaki walikua wanayatupa ufukweni hali iliyopelekea watu kuamini kuwa kulikuwa na wanyama wakali wanaokula watu, hawakujua kabisa kama kuna familia inaishi katika mapango hayo yaliyopo karibu.

Bean na familia yake hiyo kubwa waliendelea kufanya uhalifu huo hadi siku moja walipomvamia bwana mmoja aliyekua mjuzi kupigana, baada ya kuwadhibiti maadui akawapeleka kwa viongozi, ikabidi waongozane hadi mapangoni wakiwa na kikundi cha askari 400 wa mfalme James VI.

Kufika mapangoni walistaajabu kuuona ukoo mkubwa wa Bean ukiishi humo, mabaki ya miili yalikuwa mengi mnoo huku sehemu nyingine zikining'inizwa ukutani, miili iliyopatikana mapangoni humo kwa siku hiyo ilifika 1000, wengine walikuwa wamefungwa wakiwa wazima. Bean alikamatwa na kunyongwa siku hiyo hiyo.
 
Alifahamika kama Shi Gulan, lakini watu wake wa karibu walimbatiza jina la Shi Jianqiao kumaanisha 'Upanga' unaoashiria ahadi yake ya kulipiza kisasi kifo cha babake aliyeuawa kwa kukatwa kichwa na kiongozi Sun Chuanfang, mwaka 1925.

Shi Jianqiao alitumia miaka 10 kulipiza kisasi kifo cha babake.

Miaka kumi baada ya Sun Chuanfang kustaafu, Shi Jianqiao, alimvizia na kumuua kwa kumpiga risasi kichwani akiwa anaomba katika hekalu la kibudha .

Badala ya kutoroka eneo la tukio, Shi Jianqiao aliamua kubaki na kuwasimulia wapita njia kuhusu kitendo alichofanya. Inadaiwa hatua hiyo ilikuwa njama ya kuvutia vyombo vya habari na kutafuta huruma ya watu.

Alifikishwa mahakamani na kusamehewa mashtaka mwaka 1936 kwasababu kosa lake lilionekana kama kisasi halali cha wazazi wake.

Shi Jianqiao alifariki mwaka 1979 akiwa na miaka 73
 
Mwaka 2012, kamanda wa Taliban wa Afghanistan Mohammad Ashan alikua anatafutwa na polisi kwa tuhuma za kupanga mashambulizi ya kigaidi, yakabandikwa mabango yanayoonesha sura yake na kutangazwa zawadi ya dola $100 (230k ya sasa) kwa atakaefanikisha kumkamata.

Jamaa baada ya kuona hivyo alijipeleka polisi mwenyewe na kudai apewe zawadi ya $100 ambayo ilikua imeahidiwa kwenye bango la kukamatwa kwake.
 
Mwaka Jana (2020) nchini Kenya katika shule ya msingi Kakamega Wanafunzi 14 walikufa na wengine 39 kujeruhiwa baada ya kuona jini live.
Baadae vyombo vya usalama viliripoti kuwa vifo na majeruhi hao vilitokana na mkanyagano uliosababisha Wanafunzi hao kukosa hewa hadi kufa na wengeni kujeruhiwa kutokana mshtuko wa kuona jini huyo.

Jambo ambalo lilionekana la ajabu zaidi kwenye tukio hili ni kwamba waliokufa hakuna aliyetokwa damu.
 
Mwaka 1898 ilichapishwa riwaya ya "Futility" iliyoandikwa na Morgan Robertson ambayo ilipata umaarufu zaidi kuanzia miaka ya 1912 baada ya kuzama kwa Meli ya Titanic na kubadilishwa jina na kuitwa "The wreck of the Titan".

Riwaya hii iliyokuwa imeandikwa miaka 14 kabla ya kuzama kwa Meli ya Titanic ilipata umaarufu na kuonekana kama mwandishi alitabiri kilichotokea katika kuzama kwa Meli ya Titanic kutokana na mfanano wa mambo mengi yaliyoelezewa kwenye riwaya na uhalisia wa kuzama kwa meli hii pamoja na kuendana kwa ukubwa wa Meli hizi na ata pia katika riwaya ilielezea Meli kuzama mwezi April na baadae baada ya miaka 14 kupita katika uhalisia Meli ya Titanic ilizama pia April 1912.
 
Mnamo July, 1518 wakazi wa mji wa Strasbourg walikumbwa na ugonjwa wa ajabu wa kucheza mfululizo bila kupumzika! Picha lilianza kwa mwanamke mmoja anaejulikana kama Frau Troffea alipoingia mtaani na kuanza kucheza kwa siku sita mfululizo. Baadae kundi kubwa la watu likajumuika na kuanza kucheza kiajabu ajabu yaani dansi isiyoeleweka. Mpaka kufika Agosti, ugonjwa huu ulikuwa umeshawakumbuka watu wapatao 400 na kukiwa hakuna majibu nini haswa kimetokea kwa wakazi hao, baadhi ya wataalamu wakadai ni kuchemka kwa damu na kuwa ya moto "hot blood" na kusababisha stress iliyopelekea mwili kufanya vitu vya ajabu/hatari bila hiari yako.

Jitihada za serikali zilipelekea kujengwa kwa jukwaa maalumu na kuwaita wataalamu wa muziki ili waweze kuwapigia mziki pengine ugonjwa huo ungetoka lakini hawakufanikiwa. Watu walianza kuanguka na kufa kutokana uchovu mwingi. Wengine walikufa kutokana na magonjwa ya moyo na stroke. Kisanga hiki kiliendelea mpaka Septemba pale ambapo wanakijiji walienda milimani na kuanza kuomba ili kuyashinda yanayowasibu.

Kisa kama hiki kilishawahi kutokea huko Uswisi, Ujerumani, na Uholanzi lakini haikuwa babu kubwa kama hii ambayo ilichukua uhai wa watu.
 
Mnamo karne ya 12, kulikuwa na watoto wawili ambao walikuwa na ngozi za kijani ambao walikutwa na wanakijiji kwenye shimo kubwa la kutegea mbwa mwitu (Wolf pits-Woolpit) huko St. Mary's Uingereza katika kijiji cha Woolpit, ambalo liliwekwa kuzuia mbwa mwitu hao wasidhuru wakazi wa eneo hilo.
Watoto hao walikuwa wanaongea lugha isiyoeleweka ambayo ni tofauti sana na lugha ya wanakijiji hao ambao ilikuwa kingereza. Ajabu ni kwamba hawakuweza kula chakula cha kawaida cha binadamu, wao walitaka majani mabichi na nyama mbichi ila baadae walianza kuzoeshwa kula maharage na mikate.
Watoto hao walikuwa kaka na dada na walikuwa wadogo kiumri... Mtoto wa kiume hakuweza kuvumilia maisha hayo mapya kwani aliugua kwa msongo wa mawazo, akashindwa kula na kufariki. Aliebaki ambae ni wa kike aliweza kuvumilia mazingira na kuzoea vyakula vyao na mwishowe akaanza kujifunza lugha ya kingereza.
Baada ya kujua kiingereza alieleza kuwa yeye na kaka yake wametoka sehemu inaitwa "Land of Saint Martin" ambapo hakukuwa na jua, hakuishia hapo akawaelezea kuwa huko walipotoka kila kitu kilikuwa na rangi ya kijani ikiwemo aina ya binadamu wanaopatikana huko. Akaulizwa ilikuwaje akafika huko, akasema walikuwa wanaangalia ndege waliokuwa wakisafiri kwa makundi na waliwapenda sana hivyo ikabidi wazidi kusogea mbele ili wasiwapotee.
Akaendelea, walipofika sehemu moja wakasikia sauti ya ajabu (ilikua sauti ya kengere) inatokea ndani ya pango ikabidi waachane na ndege hao na kuifuata sauti hiyo. Walipofika mbele kidogo ndipo walipokutana na jua la ajabu na liliwasababisha kutoona vizuri kutokana na mwanga wa jua kuwaziba na wakajikuta wanatumbukia kwenye shimo na ndipo walipokutwa katika mazingira hayo.

Haikuwahi kubainika kama "Land of Saint Martin" walipotokea watoto hao ni sehemu gani lakini watafiti na wanasayansi wengi walidai kuwa inawezekana watoto hao walidongoka kutoka katika sayari nyingine.
 
Mnamo mwaka 1815 mtu mmoja anayeitwa Diderici alivaa nguo za bosi wake, ambaye alikufa kwa kiharusi, akavaa wigi na akaenda benki kujaribu kutoa pesa kutoka katika akaunti ya marehemu.

Mpango wake ulishindikana. Diderici alikamatwa na kuhukumiwa kifungo cha miaka kumi. Alikuwa anatumikia kifungo chake katika gereza la Prussia, Weikselmünde. Kulingana na rekodi za gereza, wakati Diderici pamoja na wafungwa wengine walipelekwa ndani ya uwanja kwa matembezi, kitu cha kushangaza kilianza kutokea: mwili wake ulionekana ukiwa mtupu (uchi) na mwishowe alitoweka ndani ya hewa nyembamba kama moshi.

Hii ilitokea mbele ya wafungwa na walinzi ambao walishangaa sana. Wakati wa mahojiano, mashahidi wote walisema kitu kimoja. Haikuweza kuelezeka na kuingia akilini kilichotokea. Mwishowe viongozi wa gereza walifunga kesi hiyo na wakachukulia kama "mapenzi ya Mungu". Tangu siku hiyo Diderici hakuwai kuonekana tena mahali popote.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…