“Naomba nijinukuu mwenyewe nilisema ‘huu ni wakati wa kuzika tofauti zetu’, ukiingia kwenye Mitandaoni ya Kjamii kuna uzandiki mkubwa sana kila Mtu anazua lake, kinachokuja kichwani anaweka kule na kuwaamisha Wananchi mambo kadhaa, Viongozi wa Dini mlipige vita hili”———Rais Samia Suluhu kwenye kongamano la Viongozi wa Dini Dodoma leo
“Viongozi wa Dini mkiongea yanabaki kwenye mioyo ya Watu, Sisi Viongozi wa Siasa tukiongea yanabaki kwenye vichwa vya Watu, vichwa vikichanganywa na mambo mengi yanatoka na huu ndio umuhimu wa Viongozi wa Dini kufanya kazi na Sisi, mtatusaidia kusema tunayotaka kusema”———Rais Samia
“Tukumbuke tupo kwenye Mwezi wa Toba (Ramadhan), naomba muendelee kuliombea Taifa letu, Nchi yetu haina Dini lakini Katiba ya Nchi yetu imetoa uhuru kwa Wananchi kuabudu Dini wanazotaka na hii imefanya kuwe na ushirikiano mkubwa, sio kila Nchi jambo hili linawezekana”———Rais Samia