Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,977
“Naomba TAMISEMI mkakusanye mapato na matumizi yakafuate sheria na kanuni, nimemleta Mwana-Mama madhubuti (Ummy Mwalimu) nimempa Katibu Mkuu mzuri na Wasaidizi ni imani yangu kuwa kazi itafanywa”———Rais Samia Suluhu baada ya kuwaapisha Viongozi wapya Ikulu Dar es saalam mapema leo
“TAMISEMI mbali na majukumu mengine mna jukumu la elimu na afya, Shule za Sekondari za Wanawake zina bajeti maalum naomba mkasimamie, tunatarajia kujenga Shule 26 mpaka 2025 naomba hili likatimie pamoja na kuendelea kujenga Hospitali za Wilaya”———Rais Samia
“Natambua kuna Walimu wengi tu karibu Elfu 6 au zaidi ambao wameacha kazi, wamestaafu, wamefariki n.k na kunahitajika wakuziba nafasi, Utumishi mko hapa na TAMISEMI mkalisimamie, Walimu Elfu 6 wapatikane haraka ili wakawatumikie Watanzania”———Rais Samia
“Kuna ajira mpya za Madaktari upande wa afya, tumemaliza Hospitali na Vituo vingi, Bajeti ya mwaka huu ni kuweka vifaa na Watumishi kwahiyo Utumishi na TAMISEMI mkalisimamie hili la Watumishi na vitendea kazi kwenye huduma za afya”———Rais Samia
“TAMISEMI mbali na majukumu mengine mna jukumu la elimu na afya, Shule za Sekondari za Wanawake zina bajeti maalum naomba mkasimamie, tunatarajia kujenga Shule 26 mpaka 2025 naomba hili likatimie pamoja na kuendelea kujenga Hospitali za Wilaya”———Rais Samia
“Natambua kuna Walimu wengi tu karibu Elfu 6 au zaidi ambao wameacha kazi, wamestaafu, wamefariki n.k na kunahitajika wakuziba nafasi, Utumishi mko hapa na TAMISEMI mkalisimamie, Walimu Elfu 6 wapatikane haraka ili wakawatumikie Watanzania”———Rais Samia
“Kuna ajira mpya za Madaktari upande wa afya, tumemaliza Hospitali na Vituo vingi, Bajeti ya mwaka huu ni kuweka vifaa na Watumishi kwahiyo Utumishi na TAMISEMI mkalisimamie hili la Watumishi na vitendea kazi kwenye huduma za afya”———Rais Samia




ili raia waenda za faster faster, muda ni pesa...