Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Innocent Bashungwa ametoa pongezi baada ya Serikali kuanzisha Tahasusi (Combination) mpya tano kwa ajili ya Wanafunzi wanaoingia kidato cha tano mwaka huu zikiwemo combination zenye masomo ya Michezo ili kuondoa changamoto ya ukosefu wa Wataalamu Nchini.
Combination zilizoongezwa hni Physics, Mathematics na Computer Studies (PMC), Kiswahili, French, Chinese (KFC), Kiswahili, English, Chinese (KEC), Physical Education, Biology ,Fine Art (PBF) na Physical Education, Geograph , Economic (PGE).
“Kufuatia vikao vya Wizara ya Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo, OR TAMISEMI, na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, somo la michezo litafundishwa kama Tahasusi (Combination) kuanzia mwaka huu, nawapongeza sana Waziri Jafo na Waziri Prof. Joyce Ndalichako kwa ushirikiano wao, hili ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuboresha mashindano ya UMITASHUMITA na UMISETA ili kupitia mfumo huo tupate Walimu wabobezi wa kufundisha Vijana wetu Mashuleni_Bashungwa