Makapuku Forum

Makapuku Forum

20210312_171651.jpg
 
"Kuanzia Juzi hata leo asubuhi nimeona Watanzania wenzetu wenye husda, tena hawako ndani ya Nchi wako huko, wanashawishi Vyombo vya Kimataifa viseme ‘Rais wa Tanzania anaumwa,kajifungia’, tena hawako hapa, wapo huko, tulioko ndani tuko kimya, ni husda”-Waziri Mkuu Majaliwa akiwa Njombe leo

"Watanzania mtulie uongozi wenu upo,Rais Magufuli anaendelea vizuri, kumzushia ugonjwa ni chuki tu, inawasaidia nini?, ‘atoke’, atoke aende wapi?, ‘aje’ aje afanye nini?, umeshamkuta Rais siku moja anazurura kariakoo?, Rais ana mipango yake ya kazi sio Mtu wa kuzurura”-MAJALIWA

"Juzi tu Rais alikuwa Chato akatoka akaenda Kahama, Tabora, Dodoma, akarudi DSM, juzi kaapisha mnataka tena azunguke Nchi nzima, sisi tunafanya nini?, nini umuhimu wa kuwa na Wasaidizi!, azunguke yeye tena Nchi nzima kweli?”
20210312_173113.jpg
 
Bilionea wa Afrika Kusini na Mmiliki wa Club ya Mamelod Sundowns ya Afrika Kusini Patrice Motsepe (59) amechaguliwa kuwa Rais wa saba wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF)
20210312_173209.jpg
 
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila amesema leo asubuhi amempigia simu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli akimshukuru kwa kuidhinisha fedha za utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani humo.

Chalamila ameyasema hayo leo alipokuwa anazungumza kuhusu ziara ya siku mbili ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Mbeya inayotarajia kufanyika March 14 na March 15, mwaka huu.

“Ime-trend kidogo hapa katikati kwamba Rais yupo kwenye matibabu mahali fulani, inawezekana hao wanaozungumza ndio wapo kwenye matibabu, niwaambie Rais yupo imara na anaendelea kufanya kazi zake
20210312_173307.jpg
 
Waziri wa Viwanda na Biashara Godfrey Mwambe ametoa maagizo kwa Taasisi zote zilizoko chini ya Wizara hiyo kutofungia Biashara za Watu badala yake wakae na kuzungumza nao.

“Marufuku biashara yoyote yenye leseni kufungwa kwasababu yoyote ile, tutumie Sheria kuwezesha sio kufungia
20210312_173353.jpg
 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dr. Ndumbaro, amesema Watanzania wanne wanatarajia kufikishwa Mahakamani leo kwa tuhuma za kusafirisha vinyonga 74 na nyoka 6 kutoka milima ya Usambara, Tanga na kuwauza kwa Raia wa kigeni na wanyama hao kukamatwa nchini Austria.

“Tuwalinde hawa wanyama ambao wengine wanapatikana Tanzania pekee, tunaathiri uchumi na Utalii kwa kuwasafirisha”
20210312_173513.jpg
 
Polisi mkoani Arusha wanawashikilia Watu wawili akiwemo Raia mmoja wa China kwa tuhuma za kumteka Raia mwingine wa China na kutaka kulipwa Dola 100,000 ili wamwachie.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo amesema Mchina huyo ambaye jina lake linahifadhiwa alitekwa wilayani Karatu.

“Jeshi la Polisi Machi 7 lilipokea taarifa kutoka kwa Raia wa China, Lian Qiang(44) kuwa Mfanyakazi wao wa Kampuni ya Bonanza ambaye ni Raia wa China ametoweka katika mazingira ya kutatanisha akiwa kikazi Karatu”- RPC Arusha

“Baada ya uchunguzi wa kina Watuhumiwa walikamatwa kwenye nyumba ya kulala wageni iliyopo eneo la Ada Estate Kinondoni Dar es Salaam, Raia wa China aliyetekwa alikutwa akiwa amefungwa kamba mikononi na miguuni”- RPC Arusha
20210312_173618.jpg
 
Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi amepongeza jitihada zinazofanywa na Hospitali ya Taifa Muhimbili katika kuhakikisha kuwa huduma bora za afya na za kibingwa zinapatikana Tanzania, amesema haya wakati ya ziara yake hospitalini hapo kujionea hatua ambayo Muhimbili imefikia kwenye maandalizi ya kuanza kupandikiza Uloto (Bone Marrow transplant) kwa Wagonjwa wa Saratani ya damu na Selimundu.

“Kuna mageuzi makubwa sana yamefanyika kwenye kuboresha huduma za kawaida na kuanzisha za kibingwa, miaka ya nyuma kulikuwa na malalamiko lakini sasa hivi hakuna tena kwa kuwa tumepiga hatua na kwa sasa Tanzania inaongoza katika nchi za ukanda wa maziwa makuu kwenye eneo la huduma za tiba”- Prof. Makubi.

Prof. Makubi amesema kuwa ameona jinsi ambavyo maandalizi ya kupandikiza Uloto yanavyokwenda vizuri na kwamba kilichobaki ni ununuzi wa mashine moja tu ili huduma hiyo iweze kuanza hivyo ameutaka uongozi wa Hospitali kufanya jitihada ili ikiwezekana huduma hiyo iweze kuanza May 2021.
20210312_173646.jpg
 
Unaambiwa karibu robo ya Wajerumani wanapendelea Jurgen Klopp ndio awe Kocha mpya wa Timu ya Taifa ya Ujerumani atakapoondoka Kocha wa sasa Joachim Loew ambaye ataachia ngazi baada ya michuano ya kombe la Ulaya mwaka 2021.

Uchunguzi mpya wa maoni uliofanywa na YouGov umeonesha asilimia 24 ya Wajerumani 1,618 walioulizwa, walipendekeza Jurgen Kloop ambaye ni Kocha wa Liverpool ndioachukue nafasi hiyo huku asilimia 9 wakimpendekeza aliyekuwa msaidizi wa Loew, Hansi Flick ambaye kwa sasa yuko Bayern Munich.

Majina mengine yaliyopendekezwa ni Kocha wa Timu ya Taifa ya Soka ya Wachezaji chini ya miaka 21 Stefan Kuntz na Julian Nagelsmann pamoja na Thomas Tuchel wa Chelsea ya Uingereza, hata hivyo Klopp yeye anapendekeza Ralf Rangnick ndio achiwe hicho kijiti.
20210312_173714.jpg
 
UNAAMBIWA Wakati Pattie Mallette ambae ni Mama wa Mwimbaji Staa Justin Bieber amepata ujauzito wa Bieber akiwa na umri wa miaka 17, alishauriwa kufanya maamuzi ya kuutoa kwa lazima lakini akakataa, leo Justin ndio huyu Staa wa dunia anaetajwa pia kuwa miongoni mwa Waimbaji Matajiri chini ya miaka 30, ni ushauri gani ulishawahi kupewa ukaukataa alafu badae ukagundua hukukosea kuukataa?
20210312_173748.jpg
 
Mganga Mkuu wa Serikali Profesa Abel Makubi amesema Serikali haijakataza tafiti katika magonjwa ya mfumo wa hewa ikiwemo ugonjwa wa Corona, amesema pia tayari kuna tafiti mbalimbali zilifanyika mwaka jana kuhusu magonjwa hayo.

Amesema Serikali inachohitaji ni Watafiti kufuata mwongozo uliotolewa ambao unaelekeza vipaumbele vya Taifa katika eneo hilo la magonjwa ———> “hakuna aliyekatazwa kufanya tafiti naomba hilo lieleweke, tafiti tunazithamini, tunazihitaji katika Sekta ya Afya”

Profesa Makubi ameendelea kuipongeza Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa jitihada kubwa za kuhakikisha kuwa huduma bora za afya na za kibingwa zinapatikana Tanzania.
20210312_173813.jpg
 
Bondia Mtanzania Hassan Mwakinyo March 26 2021 anarejea tena ulingoni kupambana na bondia Brendon Dennis katika pambano la kuwania mkanda wa ABU litalofanyika Next Door Arena Masaki akiwa ndio anaanza safari ya kwenda kutimiza ndoto zake za kupigana Las Vegas Marekani.

“Kuna baadhi ya Mabondia wapo Ulaya wananigusa sana hisia zangu natamani siku moja kuona zile ndoto ambazo naziona niko nao Gym nafanya nao mazoezi ziwe ni kweli, kwa shauku yangu hiyo na morali yangu hiyo siamini kama kuna Bondia yoyote anaweza kunitoa nje ya malengo hayo mpaka kufika hiyo safari" ——— Mwakinyo.

"Naamini nitafanya vizuri japo changamoto zinaweza kutokea katika hali ya mchezo sababu huyu Mtu ninaekwenda kucheza nae yuko vizuri lakini siamini kama uzuri wake unaweza kunitoa katika ramani yangu ya kwenda nilipokusudia kwenda"
20210312_174206.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom