Makapuku Forum

Makapuku Forum

Waliishaga WW1
20210111_174353.jpg
 
Mchezaji wa Kijapan mwenye umri mkubwa Kazuyoshi Miura (54) anarudi tena uwanjani baada ya kuongeza mkataba wa mwaka mmoja na club yake ya Yokohama.

Kazuyoshi Miura atatimiza umri wa miaka 54 kamili February 26 2021 ikiwa ni siku moja kabla ya kuanza kwa msimu wa 2021 wa Ligi Kuu Japan (J-League) ambapo huu utakuwa ni msimu wake wa 17 akiwa na Club ya Yokohama toka pale alipojiunga nayo 2005.

Mara ya mwisho Miura anafunga goli ilikuwa 2017 dhidi ya Thespakusatsu Gunma katika Ligi daraja la pili na kuandika rekodi ya kuwa mchezaji mwenye umri mkubwa (miaka 50 na siku 14) kufunga goli katika professional League nchini Japan
20210111_184301.jpg
 
Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete amesema atampa shamba Mwanamitindo Flaviana Matata kama Asante baada ya msaada ambao amekuwa akiutoa katika shule ya Msinune.

Ridhiwani amesema anampongeza sana Flaviana kwa msaada ambao amekuwa akitoa kwa Wananchi wa Chalinze hususani Kijiji cha Msinune na kuahidi kumpa shamba la Heka mbili Kwa ajili ya kufanya kilimo cha mananasi

“Nimpongeze sana Flaviana Matata kwa jinsi ambavyo amekuwa anajitoa kusaidia Elimu hususani kwa Watoto wa kike, amejitoa sana kwa Watu wa Chalinze lakini hasa Watu wa hapa Msinune, Wadau wa maendeleo kama Flaviana na Wengine wanatupa nguvu kubwa zaidi kuendelea kufanya mambo mengine, kupitia mfuko wa Jimbo nitamuunga mkono kwa kuchangia cement na nondo”
20210111_184317.jpg
 
PICHA 10: Mbunge wa Muheza Hamis Mwinjuma MwanaFA akiwa ameambatana na DC wa Muheza Mhandisi Mwanaasha Tumbo wamefika kujionea uharibifu wa Barabara uliosababishwa na mvua zainazoendelea kunyesha Muheza .

Takribani Kilometres tano za Barabara zimeangukiwa na kufunikwa kabisa na miti, udongo na mawe na kusababisha kutokuwepo kwa mawasiliano kati ya vijiji vya Antakae na Vungwe vinavyounganishwa na Barabara hiyo ambapo kwa sasa havipitiki hata kwa usafiri wa pikipiki.

Viongozi hao wameambatana pia na wataalamu kutoka TARURA wakiongozwa na Mhandisi Athanas ambao kwa pamoja wamekubaliana wataanza kuifanyia matengenezo Barabara hiyo leo na kuirudisha katika hali yake ya awali ikiwa ni pamoja na kujenga Daraja.

Mbunge Mwana FA amewashukuru wataalamu hao kutoka Serikalini Chini ya Rais John Pombe Magufuli kwa kuhakikisha wanaitikia kwa haraka matatizo ya wananchi na kuyapatia ufumbuzi pale yanapojitokeza.
20210111_184335.jpg
20210111_184351.jpg
20210111_184407.jpg
 
“Rais Nyusi alinipigia simu anataka kuja Chato alisikia nipo hapa, nikamwambia njoo, nashukuru Nyusi kwa kuamua kuja Chato, unayajua maisha ya Tanzania na ni Rafiki wa muda mrefu wa Tanzania, sisi na Msumbiji ni Ndugu na tuna makubaliano ya kushirikiana”-JPM

“Biashara kati ya Tanzania na Msumbiji imeongezeka, hadi kufikia mwaka 2020 ilifikia Tsh. Bilioni 93.6, kuna makampuni ya Msumbiji yanafanya kazi hapa na baadhi ya makampuni ya Tanzania yanafanya kazi kule” -JPM

“Nawapongeza Wakandarasi, Wizara ya Fedha na pia Wizara ya Afya kwa kutaka Hospitali hii ya Rufaa ya Kanda ya Chato iwekwe jiwe la msingi na Nyusi, ila nitawabana kweli ili ikamilike mara moja, ni Hospitali kubwa itahudumia zaidi ya Watu Mil 18 Tanzania na Nchi za jirani” - JPM

“Nawapongeza Wakandarasi, Wizara ya Fedha na pia Wizara ya Afya kwa kutaka Hospitali hii ya Rufaa ya Kanda ya Chato iwekwe jiwe la msingi na Nyusi, ila nitawabana kweli ili ikamilike mara moja, ni Hospitali kubwa itahudumia zaidi ya Watu Mil 18 Tanzania na Nchi za jirani”
20210111_184508.jpg
 
“Nilipiga simu juzi kumuuliza Rais Magufuli uko wapi, na mara nyingi tunaongea asubuhi mapema, akasema yupo Chato, nikamuuliza Chato ni wapi? akasema Chato nyumbani, nikamwambia nakuja kuona kwenu, shule uliyosoma, akasema njoo, nikamwambia sili sembe nakula ugali wa kusaga akasema nitakusagia”-Filipe Nyusi,Rais wa Msumbiji

“Nakupongeza Rais Magufuli kwa kujenga Hospitali hii ya Rufaa ya Kanda ya Chato, Hospitali hii haina Chama itatumiwa na wote, nashukuru kwa kunipa heshima ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Hospitali hii, nitakuwa napiga simu kila Jumamosi kuulizia ujenzi umefikia wapi”-NYUSI

“Wakati najiandaa na Kampeni za Urais nilikuja Tanzania, Mama Maria Nyerere alinipokea akanipikia mbuzi nyumbani kwake, akaniambia ukiwa Rais, ukishindwa vingi angalau ujenge kiwanda kimoja cha dawa, kwahiyo nakupongeza JPM, kwa kushughulika na afya za Wananchi, afya muhimu”-NYUSI

“Tunaweza kusema kila kitu ila bila maisha yote tunayosema hayatoeleweka, JPM ni Rais mzuri, anashughulika na maisha ya Watanzania kutafuta nyumba nzuri, chakula, maji, afya na akiomba afya anataka ile afya ya Quality, hii ni zawadi Kwetu kuweka jiwe la msingi la Hospitali ya Rufaa Chato”
20210111_184541.jpg
 
“Nilipiga simu juzi kumuuliza Rais Magufuli uko wapi, na mara nyingi tunaongea asubuhi mapema, akasema yupo Chato, nikamuuliza Chato ni wapi? akasema Chato nyumbani, nikamwambia nakuja kuona kwenu, shule uliyosoma, akasema njoo, nikamwambia sili sembe nakula ugali wa kusaga akasema nitakusagia”-Filipe Nyusi,Rais wa Msumbiji

“Nakupongeza Rais Magufuli kwa kujenga Hospitali hii ya Rufaa ya Kanda ya Chato, Hospitali hii haina Chama itatumiwa na wote, nashukuru kwa kunipa heshima ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Hospitali hii, nitakuwa napiga simu kila Jumamosi kuulizia ujenzi umefikia wapi”-NYUSI

“Wakati najiandaa na Kampeni za Urais nilikuja Tanzania, Mama Maria Nyerere alinipokea akanipikia mbuzi nyumbani kwake, akaniambia ukiwa Rais, ukishindwa vingi angalau ujenge kiwanda kimoja cha dawa, kwahiyo nakupongeza JPM, kwa kushughulika na afya za Wananchi, afya muhimu”-NYUSI

“Tunaweza kusema kila kitu ila bila maisha yote tunayosema hayatoeleweka, JPM ni Rais mzuri, anashughulika na maisha ya Watanzania kutafuta nyumba nzuri, chakula, maji, afya na akiomba afya anataka ile afya ya Quality, hii ni zawadi Kwetu kuweka jiwe la msingi la Hospitali ya Rufaa Chato"
20210111_184434.jpg
20210111_184449.jpg
 
Mamlaka ya Indonesia imetambua eneo ilipotokea ajali na kilipo "kisanduku cheusi " cha ndege aina ya Boeing 737-500 iliyokuwa imebeba abiria 62 ilioanguka Juzi muda mfupi baada ya kuondoka kutoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Soekarno-Hatta.

Mkuu wa Shirika la Kitaifa la Utafutaji na Uokoaji Indonesia, Bagus Puruhito, amesema maafisa wanaoendesha operasheni hio wanaamini wametambua eneo la kinasa data na kinasa sauti cha ndege hiyo kinachojulikana kama black box baada ya tahadhari ya dharura inayotumwa na kifaa hicho kugunduliwa na mfumo wa Meli baharini.

Mkuu wa Jeshi Hadi Tjahjanto amesema wanaamini wanaweza kukitoa baharini kisanduku hicho kwa kutumia muda mfupi iwezekanavyo ili kubaini chanzo cha ajali hiyo, awali shirika la uokoaji lilikusanya mifuko mitano ya miili na mabaki ya Watu pamoja na mabaki ya ndege kutoka eneo la ajali, bado utafutaji unaendelea.
20210111_184557.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom