Kristo wa Nazareth, nasimama na wanawake wa Taifa hili, nikiomba rehema yako na upendo wako ukawe pamoja nao katika kusimamia malezi ya watoto, jamii na Taifa kwa ujumla, nakataa roho za kukata tamaa kwa wanawake wa Taifa hili katika Jina la Yesu, tupe moyo wa kusali, moyo wa kuendelea kusimama na familia zetu, moyo wa kutokata tamaa katika jina la Yesu!!
Asante Yesu kwa kuwa utasimama pamoja nasi, ni katika jina la Yesu nimeomba na kuamini, Amen.