Makapuku Forum

Real Madrid inapaswa kumsaini mshambuliaji wa Manchester City Raheem Sterling, 24, badala ya kiungo wa Chelsea Eden Hazard, 28, anashauri kiungo wa zamani wa Blackburn Chris Sutton. (Mail)
 
Barcelona wapo tayari kuwapa Manchester United kiungo Philippe Coutinho, 26, ama Malcom, 22, kama sehemu ya ofa ya kumnasa mshambuliaji Marcus Rashford, 21. (Mundo Deportivo, via Mail)
 
Leicester hawapo tayari kuwatoa mabeki wake Harry Maguire, 26, na Ben Chilwell, 22, ambao wamekuwa wakinyemelewa na vilabu vikubwa vya Manchester United na Manchester City. (Mirror)
 
Manchester United hawana mpango wa kumuuza mchezaji wao anayepokea mshahara mkubwa zaidi, Alexis Sanchez, 30, licha ya kutoonesha makali uwanjani na ripoti kuwa suala la mshahara wake linatatiza mapatano ya mkataba mpya na kipa David De Gea. (London Evening Standard)
 
Kiungo wa Liverpool na Serbia Marko Grujic, 22, ambaye yupo kwa mkopo katika klabu ya Hertha Berlin, anataka kusalia kwenye klabu hiyo ya Ujerumani walau kwa mwaka mmoja zaidi. (Liverpool Echo)
 
.....ha hahahah, binamu hivi umesahau kuwa mimi ni mwanachama wa kila ambacho AHADI zetu zinasema "Nitasema kweli Daima, Fitina Kwangu Mwiko".
Siwezi kubadili gia angani maana ndege za sasa hivi wala haziaminiki.

Shari lakini
Hahaha sawa sawa binamu
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…