Makapuku Forum

Makapuku Forum

NASA Parker Solar Probe chombo ambacho kwa sasa kinaelekea kwenye Jua kimefanikiwa kupiga picha ya kwanza kabisa karibu zaidi na Jua letu wakati chombo hicho kilipokuwa kinaingia kwenye Corona - eneo lenye joto kali sana kushinda hata joto lililokuwa kwenye uso wa Jua.

Kwa sasa hii ndiyo picha pekee iliyopigwa karibu zaidi kwenye Jua letu kutokea umbali wa maili milioni 16.9. Huo mvuke unaong'aa upande wa kushoto ni Coronial Streamer - pepo za joto zinazotoka kwenye Jua, na hicho kidoti cheupe kinachong'aa ni sayari ya Jupiter.

NASA Parker Solar Probe ni chombo pekee kuwahi kutengenezwa na binadamu ambacho kimelifikia Jua kwa ukaribu zaidi na kinategemewa kwenda kulichunguza na kurudisha majibu ya maswali mengi tusiyofahamu dhidi ya Jua letu ifikapo mwaka 2025.
Screenshot_20181214-133928.jpeg
 
Baada ya safari ya miaka 40 hatimaye Voyager 2 chombo dada cha Voyager 1 nacho kwa sasa kimefanikiwa kutoka kwenye mfumo wetu wa Jua na kuingia kwenye anga la ndani zaidi (Intersteller Space).

Kwa sasa Voyager 2 kimeshatembea zaidi ya maili bilioni 11, umbali huo ni sawa na kwenda na kurudi kwenye sayari ya Mars mara 164 kutokea Duniani. Tarehe 5 mwezi wa 11 Voyager 2 kilikuwa chombo cha pili kutengenezwa na binadamu ambacho kimetoka kwenye Heliosphere - eneo ambalo sayari zote zinazozunguka jua letu zimo ndani yake.

Siku hadi siku uwezo wetu binadamu wa kuuchunguza mfumo wetu wa Jua na sayari zake unakuwa mkubwa hata kuweza kwenda mbali zaidi kwa kutoka nje ya mfumo wetu wa Jua kupitia vyombo hivi viwili (Voyager 1 na 2) kwa sasa tumeweza kuweka chombo kwenye sayari ya Mars na tunaifahamu vizuri sayari ya Mars kuliko tunavyozifahamu bahari zetu, ifikapo mwaka 2025 tunategemea kulisogelea kwa ukaribu zaidi Jua letu kupitia Parker Solar Probe ila mafanikio haya yote bado yanachukua sehemu ndogo sana katika ufahamu wetu wa ulimwengu.
Screenshot_20181214-134032.jpeg
 
Mmorani mmoja kutoka jamii ya Maasai kutoka kaunti ya Kajiado nchini Kenya ameacha watu midomo wazi baada ya kufunga ndoa na wanawake wawili kwa mpigo.

Tom Mako, maarufu kama Junior, 27, alifanya harusi na Elizabeth Silamoi, 25, na Joyce Tikoyian, 23 Jumanne wiki hii.
Mako anatokea kwenye familia ambayo ndoa za wake wengi ama mitala ni jambo la kawaida.

Wanaume wa dar hawawezi hivi
Screenshot_20181214-134255.jpeg
 
Mmorani mmoja kutoka jamii ya Maasai kutoka kaunti ya Kajiado nchini Kenya ameacha watu midomo wazi baada ya kufunga ndoa na wanawake wawili kwa mpigo.

Tom Mako, maarufu kama Junior, 27, alifanya harusi na Elizabeth Silamoi, 25, na Joyce Tikoyian, 23 Jumanne wiki hii.
Mako anatokea kwenye familia ambayo ndoa za wake wengi ama mitala ni jambo la kawaida.

Wanaume wa dar hawawezi hiviView attachment 968005
King Mswati lee huyo amefunga ndoa na marrybaby pamoja na my damned demi kwa mpigo!!
 
Mahakama moja nchini Singapore inasikiza kesi ya kipekee inayowahusu madereva wawili wa “Forklift” raia wa China wanaotuhumiwa kudai hongo ya dola moja kwa kila lori wanalopakia mizigo bandarini. Dola hiyo moja ilikuwa ya kuharakisha upakiaji makasha.

Chen Ziliang, 47, na Zhao Yucun, 43,wanakabiliwa na kifungo cha miaka 5 gerezani.

Singapore Inajivunia kuwa taifa linaloshudia idadi chache zaidi ya visa vya rushwa duniani.
Screenshot_20181214-134613.jpeg
 
Somalia imeiuzia China haki ya kuvua samaki katika bahari yake. Rais Mohammed Abdullahi Farmajo amezipa kampuni 150 za China leseni ya kuvua samaki aina ya Tuna katika bahari ya taifa hilo kinyume na matarajio ya maelfu ya wavuvi wanaohofu hatua hii itaathiri uwezo wao wa kujitafutia riziki.
Screenshot_20181214-134918.jpeg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom