Makapuku Forum

Makapuku Forum



...kumbe Prof Benno Ndulu yupo huku kwa Wachumi?!1 Labda kwenye mkutano wao wataongelea na ni sababu gani Jumuiya ya wafanyabiashara imeshindwa kukutana majuzi.
Watauchambua uchumi wetu inaosemwa kuwa unakuwa kwa asilimia 7 kwenye makaratasi ilhali uchumi wa mtu mmoja mmoja uko chini isivyo kawaida. Mtumishi wa umma (mind you; serikali kwa hapa kwetu ndo muajiri mkubwa) hajapandishiwa mshahara tangu mwaka 2015, bei zimekuwa zikiruka kila siku, uwezo wa mtu kununua umeshuka (consumer price index yetu inayasema haya kwa uzuri kabisa), gharama za maisha zimeshuka na hii si afya kwa kila aina ya biashara.

Anway Lyon Lee uko kwenye sekta binafsi ya biashara unajua hali ilivyo. wachumi wakikutana tutapenda kusikia wamesema nini ila wakija na mapambio na kaswida tutasema asante
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom