Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mfano kama atatokea mtu muda huu na akauuliza swali hili "Je ni kitu gani tukikupa utakuwa na furah?" Naimani majibu yatukuwa mengi sana kuna wengine watasema "Ukinipa pesa nitafurahi", na kunawengine watasema "Ukinipa nyumba na magari nitafurahi", majibu yatakuwa mengi sana. Ila ukweli utabaki kuwa pale pale kuwa furaha ya moyo haitegemei nyumba wala pesa. Furaha ya moyo inategemea sana moyo wenyewe ulivyouzoesha na namna unavyoyapokea mambo katika maisha. Mfano nitakupa kuna watu wakifikwa na matatizo huwa hawawezi kabisa kufikiria utatuzi wa tatizo kwa haraka. Yani wao wakifikwa na tatizo kazi yao kubwa ni kulia na kulaumu watu waliowasababishia matatizo. Sasa kanuni za furaha zinalikataa hilo jambo kwa kiasi kikubwa sana, na zinaeleza kulipokea tatizo kwa mfumo huo ni kuongeza tatizo jengine. Siku zote ili uweze kurudisha furaha nafsini baada ya nafsi kuchafuka kwa jambo lililokusibu, unatakiwa kwanza usilikuze tatizo akilini mwako na kuliona kubwa sana. Yani kama hivi pengine umefukuzwa kazi kazini kwa kosa ambalo si haki wewe kufukuzwa kazi. Unachotakiwa kukifanya ni kulipokea tatizo kwa njia ya busara bila hamaki na hapo hapo uwanze kutafakari je nitarudi vipi kazini kwa kutaka ushauri kwa baadhi ya watu wako wa karibu. Kitendo hichi kitakupa uhuru na fikra mbadala zenye kujenga pia kitakusukuma kufanya maamuzi sahihi. Kwahiyo kikubwa tunachotakiwa kuwa nacho ninamna ya kuyapokea mambo na jinsi ya kuyatatua, hapa viwango vya furaha havitopungua ndani ya mioyo yetu. TAFAKARI KWA KINA Furaha ni chimbuko la namna unavyo yapokea mambo
 
Haijalishi ni mazingira gani unapitia katika maisha yako, lakini ni lazima ujue kuwa usafi ni kitu muhimu sana ndani ya nyumba na mazingira yote yanayokuzunguka. Kuna dhana imejengeka kuwa usafi hautakiwi kwenye mazingira duni, dhana hii sio sahihi nani dhana ya kijinga sana. Usafi ni jambo muhimu kwa kila binadanu na ndio utu na heshima. Mtu ambae anachukia usafi zipo dalili za wazi kabisa kuwa atakuwa anamatatizo ya akili kichwani mwake. Katika jambo hili la usafi mwanamke anatakiwa awe kipao mbele sana, kwasababu yeye ndio msimamizi na muangalizi wa familia muda mwingi kuliko mwanaume. Ni aibu sana ndani ya nyumba kukiwa kuchafu wakati mke halali yupo. Ni aibu sana mume kuvaa nguo chafu zenye uvundo wakati mkewe kipenzi yupo ndani ya himaya yake. Mwanamke anapaswa kuongeza thamani ya usafi kwa watu wake, kwasababu wakati mwengine utimamu wa mtu utizamwa kwa muonekano wake. Mwanamke ambae mvivu kusafisha nyumba yake na kuipamba ni hatari sana kwenye maisha ya ndoa. Kwasababu uchafu wake hauwezi kukupa amani na furaha maishani mwako. Kuna baadhi ya wanawake ni wachafu kiwango cha stashahada, yani yeye mwenyewe kuoga kwake kazi na hafikiri hilo kabisa. Mwanamke unapishana nae ananuka ng'onda kanakwamba anafanya kazi kwenye masoko ya samaki vile. Chumba kipo ovyo ovyo mito ina alama za mate na jasho na bado hashtuki kwa chochote mwanamke wa aina hii ni adhabu kuishi nae. Tunza nyumba yako, safisha eneo lako, fahamu kuwa usafi ndio umvuta mwanaume kuwa karibu na wewe. TAFAKARI KWA KINA Usafi ni kichocheo cha mapenzi
 
Kuna matatizo mengi sana yanaweza kumsababishia binadamu kupata matatizo ya akili. Moja kati ya visababishi hivyo ni mtu kufikiri kwa muda mrefu juu ya tatizo lililomfika. Mfano wa hilo ni mtu anapogundua kuwa mke wake au mume wake anamsaliti. Tatizo kama hili linapomfika mtu kama hajapata uwangalizi mzuri na ushauri, na njia za utatuzi, anaweza kufanya mambo ya ajabu sana tena bila kujali. Matatizo kama haya ndio yamesababisha watu wengi kufanya mauaji ya kinyama au wao wenyewe kujiua. Pia matatizo yenye mfumo huu tuliyoeleza huwa yanachangia sana mtu kujichukia yeye mwenyewe. Wapo watu wanatabia hii na unaweza kumuona ukasema kuwa karogwa kumbe undani wake ukichunguza utakuja kugundua kuwa aliwahi kufikwa na tatizo huko nyuma. (MKUSANYO WA TABIA ZA KUJICHUKIA) 1 Kujitenga na watu kwa muda mrefu (Hapa tunahusisha ile tabia ya mtu kukataa kukaa na watu, yani muda mwingi yeye ujificha ndani peke yake.) 2 Kukata tamaa ya maisha na kutamani kufa (Mtu anaweza akapata tabia hii ya kukata tamaa katika maisha yake tena kwa kiasi kikubwa. Kiasi ambacho haoni faida yoyote ya kufanya kazi na hata kuishi. Sasa tabia ya aina hii jua kuwa lipo tatizo hapo si bure) 3 Kuchukia aina fulani ya watu Kuna wanawake waliopitia unyanyasaji kwa wanaume zao huwa hawataki kabisa habari ya wanaume na wengine ukaa muda wote wa maisha yao bila kuolewa. Hii usababishwa na tatizo tulosema hapo juu. Tabia hizi tulizozisema chimbuko lake huwa ni fikra zilizokosa kikomo na anaefikiri hana mshauri mzuri wa kumrudisha kwenye hali yake ya kawaida. Mtu anapofikwa na tabia hizo si vyema ukaanza kumuhukumu na kumkalipia tu. Muhimu la kufanya ni kuanza kufatilia mabadilko hayo ya tabia yamesababishwa na nini. Hapa utatumia hekima maneno mazuri ili kugundua tatizo na kumuweka saba. TAFAKARI KWA KINA Kila jambo kuna aina yake ya kulitatua.
 
Kuna aina fulani ya marafiki ambao hatushauri kabisa kuwa nao au kuwa karibu nao. Aina hii ya marafiki wanaitwa (Toxic people) toxic people ni wale maarafiki ambao wanatabia kuu tatu. Kwanza huwa wanapenda kukatisha tamaa wenzao. Pili huwa wanapenda kulaumu wenzao mara kwa mara. Tatu huwa wanapenda kusema au kuzungumzia habari za watu wengine. Aina hii ya marafiki wenye tabia hii tunashauriwa kuwa hawafai kuweponao kwa ustawi wa mtu binafsi. Maisha hayatakiwi kuendeshwa kwa lawama wala shutuma, maisha yanatakiwa kuendeshwa kwa busara na hekima katika kila jambo unalofikiria kulifanya. Ikiwa kama kuna mtu amekusababishia madhara yoyote au anguko lolote la kimaisha kwako, busara sio kumlaumu mara kwa mara, busara ni wewe kutafuta mbinu au njia nyengine ya kujinasua kimaisha. Hivi kuendelea kumlaumu na kuwahadithia watu mtu alokusababishia matatizo fulani hivi faida yake huwa nini?. Ikiwa kama hakuna faida bali ni kuendelea kujiumiza tu, kwanini unaendelea na hilo wakati kuna mengi muhimu yanakuhitaji uyafanye na huyafanyi. Rafiki ambae kazi yake ni kukukatisha tamaa mara kwa mara kuwa hautoweza kufanikiwa, huyu hafai kuwa rafiki kama kweli unataka mafanikio maishani. Kuanguka katika maisha aina maana kuwa ulichofanya sio sahihi hapana. Wakati mwengine mtu anaanguka katika maisha ni kutokana na washirika alofanyanao jambo lake sio sahihi. Jambo lolote linapofanywa wakati husio sahihi au na watu wasio sahihi basi ni ngumu sana matoke ya jambo hilo kuwa sahihi. Hoff mantroy aliwahi kusema "When you fall ask yourselfe what is the lesson?" Akiwa na maana kuwa pindi utakapo anguka unabidi ujiulize mwenyewe kulinga na somo ulolipata kwenye anguko lako. Kwahiyo hapa unaona kuwa anguko lolote huwa linakufunza kitu fulani na linakukumbusha sehemu fulani uliokosea hili kesho yako usikose tena. Kwahiyo marafiki ni lazima tuwachangue sio kila anaecheka na wewe anafaa kuwa rafiki. TAFAKARI KWA KINA Rafiki lazima umchague yeye hasikuchague wewe tu.
 
Ustawi wa mtoto unategemea sana malezi na upendo wa wazazi wake wote wawili. Mtoto kulelewa na mzazi mmoja ni vyema lakini si bora kwa afya ya malezi. Inatakiwa tufahamu kuwa zipo aina nne kuu za malezi ya mtoto kulingana na mazingira yanayomzunguka mtoto. Katika aina zote hizi nne aina moja tu ndio wataalamu wa mambo ya mahusiano ya binadamu wanasema ndio bora na muhimu kwa malezi ya mtoto. Aina hiyo bora ni ile aina ambayo mtoto anapata malezi kutoka kwa wazazi wake wote husika. Mfumo huu wa malezi ndio umeshauri sana kuwepo kwenye jamii zetu kama uwezekano ukiwepo. Mtoto anapopata malezi kutoka kwa wazazi wake wote wawili moja kati ya faida ambazo zinapatika ni ukaribu baina ya mtoto na mzazi. Mtoto ujenga ukaribu na mapenzi ya dhati wakati wote na wewe. Pia anakuwa anajenga matumaini moyoni mwake kuwa yupo mtu ambae anaweza kutatua shida zake. Athari anazozipata mtoto kwa mtengano wa wazazi ni kubwa sana. Mtoto aliezoea akiamka anamuona baba yake na mama yake wapo kwenye meza moja wanakunywa chai, leo anakunywa na mama yake au baba yake tu ukweli inaumiza sana. Tena baya zaidi mtoto anajua kuwa mama kamfukuza baba au baba kamfuka mama hili ni jeraha zito ndani ya moyo wake. Inapaswa wazazi wajitathmini kwa makini kuhusu malezi ya watoto wao, kwani wao ndio chanzo mama cha kuzorota afya adabu kwa watoto wao. TAFAKARI KWA KINA Malezi ni ushirikiano sio utengano.
 
Moja kati ya vitu ambavyo vinachangia kwa kiasi kikubwa kuvunjika kwa ndoa nyingi kwenye kwenye miaka hii ya karibuni ni fikra za kimagharibi kuziruhuru zitawale ndoa zetu. Ndoa nyingi zimekosa hadhi ya kuitwa ndoa kwasababu ya mfumo wa kimagharibi kupasua misingi ya ndoa. Baadhi ya wanawake wameacha majukumu yao ya asili kwa kuitumikia fikra ya usawa kwa wote. Hakuna aliepinga kuwa sisi wote ni binadamu na inatakiwa tuishi kwa usawa,ila inatakiwa kufahamika kuwa usawa wetu wa ubinadamu hauwezi kuzuiya utofauti wa kijinsia. Itabaki kuwa tunatofauti za kijinsia,kifikra na hata kimtizamo. Hivi ndio alieumba ulimwe ndio ametaka tuwe hivi tena kwa makusudio maalumu. Sasa leo mwanamke anapoacha majukumu yake ya kiasili kama kuwahudumi watoto na mumewe kwasababu ya dhana hii ya usawa kamwe usalama wandoa hauwezi kuwepo. Mke mda wote yupo kazini hata muda wa kuwahudumi watoto wake na mume wake hana. Watoto wanalelewa na mfanyakazi wa ndani au na majirani, alafu unataraji kuwa ndoa itakuwa na mapenzi na kudumu. Mume anahangaika na vifuko vya chipsi kila siku na mke anapojaribu kuambiwa majibu yake ni ya kinyama nasiyakiungwana. Mke anamjibu mumewe "Siwezi kukupikia wiki hii yote niko bize na kazi za ofisini kwahiyo nitakuwa nachelewa kurudi nyumbani". Hapa ndio tulipofikia, kwa mfumo huu kudumu kwa ndoa itakuwa ni ndoto tu za nyembo kutaka ufalme wakati yupo kifungon. TAFAKARI KWA KINA Mifumo ya kuiga ndio inayotuponza maishani.
 
Hutakiwi kukata tamaa kwenye maisha yako eti kwasababu ya mapungufu fulani uliokuwa nayo kwenye kwenye mwili wako. Fahamu kuwa Mungu hakupi jambo lolote ila lazima kutakuwa na sababu maalumu. Kuziba kwa macho masikio yakiwa bado yanasikia kwa umakini hiyo nayo ni fursa na ukiitumia inaweza kuwa daraja zuri la kupandisha kipato chako. Kulemaa miguu sio ishara kuwa na akili nayo imelemaa hapana. Kuna watu walemavu wa miguu na mikoni lakini wanaakili nzuri sana kiasi cha kustajabisha ufahamu wao. Tuondoe ile fikra kuwa mtu akiwa na mapungufu mwilini mwake kuwa yeye ni mzigo tu na hapaswi kupewa nafasi yoyote katika maisha. Maisha yanataka sana akili na busara kuweza kuyakabili. Ukiwa mchache wa busara na hekima maishani kamwe utabaki kuwa duni kila siku na hakuna lolote litalokuwa linaendea mikoni mwako. Watu wengi waliokosa hekima na busara kwenye maisha yao mara nyingi huwa wanashutumu uchawi na majini kuharibu mipango yao. Kumbe undani wake ni wao wenyewe kukosa kwao hekima na busara ndomana kila siku wanakuwa duni maishani. Unaishi maisha yenye mfumo mweusi mfumo ambao kifikra huoni mbele,nyumba wala pembeni vipi utaweza kufanikiwa kwa hali hii. Maisha ambayo hutaki kujifunza kwa njia yoyote ile na kila sehemu yenye mafunzo wewe unaikwepa na kuiyona inakupotezea time yako. Ni vyema tukabadilisha mifumo ya maisha yetu ili tuweze kuwania tunzo hii ya mafanikio. Kinyume na hivyo mafanikio tutayaona kwa wenzetu tu sisi tutabaki kushutumu uchawi na tawala za kidunia kuwa ndio zinatuzibia rizki zetu. TAFAKARI KWA KINA Mapambano si lazima siraha.
 
Nivyema kufanya maamuzi ukiwa na akili timamu ninani unamchagua kuwa mshirika wako kwenye jambo kubwa kama ndoa. Watu wengi mara wanapofatwa tu na wenza wao na kupewa habari zinazohusu ndoa ujikuta wanafurahi na wanalipokea jambo hilo kwa mikono miwili wakiwa wanaamini kuwa ni tunu mwenyezimungu kawapatia. Ni jambo jema na si vibaya kufurahikia jambo kubwa na la heshima kama hilo la ndoa. Lakini lazima ujuwe kuwa ndoa na uchumba ni vitu viwili tofauti. Ndoa inataka utulizano wa akili na fikra pana zilizojaa busara,hekma na weledi ngazi ya phd. Kuikurupukia ndoa kwenye wakati ambao unahisi sio sahihi kuingia ni sawa na kujikaribishia chakula chenye sumu ukiwa unadhani ni salama kwako. Miaka hii watu wengi sio wakweli kwenye ndoa, na wengi wamekuwa na tabia za kishenzi hawafungi ndoa na mtu paka kwanza wafanye mapenzi. Kufanya mapenzi kabla ya ndoa ni sawa na ukiinajisi ndoa yako. Mfano mzuri wa hili tuupeleke kwenye bidhaa. Hivi bidhaa inayonunuliwa kihalali na ile bidhaa iliyochukuliwa kwa magendo ni hipi inauhuru kuitumia?. Bila shaka jawabu litakuwa hii iliyochukuliwa kwa halali ndio itakuwa huru na salama kwa matumizi. Sasa mwanaume akikuwambia mufanye mapenzi kwanza ndio atafanya maamuzi ya kukuoa jua kuwa huyo sio mwanaume sahihi kwako ni muhuni tu. Na hapo unatakiwa kujiuliza maswali mengi huyu atanioa kwakuwa ananipenda au atanioa kwakuwa amevutika tu na mwili wangu. Mwanaume mkweli hawezi kuthubutu hata siku moja kutamka kinywani mwake kuwa anakuhitaji kimwili kabla ya ndoa. Na hata kama siku akitamka hilo basi atakuomba msamaha sana kwakuwa anajua katenda kosa la jinai kwa kutamka hilo. Jiepushe na wanaume wataka napenzi kabla ya ndoa. TAFAKARI KWA KINA Mume mkweli ni yule mwenye heshima na mwili wako.
 
Kulipwa mshahara mkubwa kazini haina maana kuwa ndio umefunguka mlango wa mafanikio katika maisha yako. Bali usipoakuwa makini inaweza ikawa ndio sababu ya kuanguka zaidi kimaisha. Wakati unapewa kiwango cha kawaida cha mshahara inawezekana ndio ilikuwa sababu iliokuwa inakufanya kupanga vizuri matumizi yako na akiba yako. Lakini punde tu lilipoongezeka pato lako ukajiachia na ukawa unatumia pesa ovyo ovyo bila nidhamu. Na ukweli watu wengi tumekuwa na tabia hii mtu anapokuwa na kidogo huwa makini na nidhamu sana ili kisiishe. Lakini anapopata kingi ujiachia na akawa anatumia bila mpangilio kwasababu anajua kipo na hakijaisha. Inatakiwa kufahamu kuwa nidhamu ya pesa katika maisha ndio jambo muhimu sana kuliko hata hiyo pesa yenyewe. Leo mtu akitokea akikupa kijarida kidogo chenye kurasa kumi ambacho kinaelezea namna ya matumizi ya pesa kwa usahihi unaweza kukidharau na kukitupa. Lakini fahamu kuwa jarida lenye kuelekeza matumizi mazuri ya pesa ni bora kuliko hata hiyo pesa yenyewe. Kuna watu wengi kwenye jamii zetu walipata pesa lakini kwakuwa walikosa elimu ya pesa leo hii watupu mbuni kipande hawana mfukoni. Lakini kuna watu walipata kiasi kidogo tu cha pesa kwakuwa walikuwa na nidhamu ya pesa na elimu ya matumizi sahihi leo wapo vizuri na kila mtu anatamani kuwa kama wao. Lakujifunza hapa ni wewe kupambana kupata elimu ya matumizi ya pesa ili uweze kukipa thamani kidogo utakacho kipata na kikubwa chake. TAFAKARI KWA KINA Elimu ya pesa ni kitu muhimu maishani.
 
Wengi tunatamani na tunataraji mara kwa mara kupata mafanikio katika maisha yetu. Lakini ukweli utabaki kuwa mafanikio hatuwezi kuyapata bila kufata njia sahihi ya mafanikio. Hivi unawezaje kupanda maharagwe kwenye shamba lako alafu ukataraji kuvuna mpunga?. Bila shaka hizi ni ndoto za juha kamwe haziwezi kutimia. Itabaki kuwa kile ulichopanda ndio utakacho kivuna kwenye shamba lako. Mfano huu ndio unatakiwa uulete kwenye dhana ya mafanikio unayotamani katika maisha yako. Inatakiwa kufahamu kuwa kuna tabia ambazo ukiwa nazo kwenye maisha ni ngumu sana kupata mafanikio. Jonathan kennedy anaeleza moja ya tabia ambazo sio rafiki kwa mafanikio ya mtu katika maisha. Moja ya tabia hizo ni mtu kupenda kulaumu laumu kila wakti katika maisha yake. Lawama siku zote huwa hazina faida yoyote kwenye ulimwemgu wa mafanikio kinachotakiwa ni wewe kuliendea jambo lako husika bila kumlaumu mtu yoyote. Kuna watu utawasikia wakisema"Fulani ndio amesababisha paka mimi sijapata pesa" maneno ya aina hii sio maneno salama kwako. Kwani kinachojengeka kwenye moyo wako kwa kupita maneno haya ni wewe kukata tamaa na kutoendelea na jambo fulani kwasababu ya fulani. Ukiwa unatamani mafanikio basi jitahidi sana kujitenga na tabia za lawama. Fahamu kuwa lawama ukimbiza fursa kwa harakwa kwenye maisha. Hata kama kuna fursa ulitakiwa upate katika maisha. Lakini kwasababu ya tabia za lawama utajikuta watu wanakukimbia na wanawapa watu wengine hizo fursa. Siku zote tabia ujengwa kwa tabia, hili tujiepushe na tabia hii ya lawama tujitahidi kuwa na tabia ya kuridhika na kusameheyana mara kwa mara. TAFAKARI KWA KINA Adui wa mafanikio ni mifumo mibaya ya maisha yetu.
 
Ujana ni daraja la kupitia kuwelekea uzeeni kama ilivyokuwa utoto ni daraja la kupitia kuwelekea ujanani. Katika ujana ndio sehemu ya kupambana na kupigana ili kutengeneza misingi mizuri itakayokunufaisha katika uzee wako. Unatakiwa kutambua kuwa nguvu uliokuwa nazo leo baada ya miaka thelathini kamwe hazitokuwepo kwenye kiwiliwili chako. Na hata cheo ulichokuweponacho leo baada ya miaka thelathini pia hakitokuwepo tena. Muhimu na adhimu kwa kijana anaejitambua anatakiwa atumie kwa umakini sana ujana wake, kwani kesho ujana hautokuwepo tena kwenye miliki yake. Kutumia ujana wako kwa kulewa na umalaya kila mtaa kamwe haiwezi kuwa ujanja bali ni kuiweka rehana afya yako na heshima yako. Kutumia ujana wako kwa kuharibu nguvu zako kwa mahadarati na magenge yasiyofaa kamwe haitokuwa historia njema baada ya kifo chako. Heshima ya binadamu ni kuacha historia njema baada ya kifo chake. Historia ambayo walobaki watajifunza na hata moyo wa kukuombea dua watakuwa nao. Lakini kama utaishi katika misingi mibaya nayaovyo ni ngumu sana kukumbukwa kwa tunu ya heshima bali utakumbukwa kama mtu mjinga aliyoyafisidi maisha yake. Maisha yako ya leo hayotowacha kuwa historia kwa watu wa kesho. Kijana unatakiwa kujizatiti kwenye elimu na mambo ambayo yatapanua bongo lako kwa haraka. Kijana mwenye akili niyule ambae anaweka akiba 40% ya mshahara wake ili kutengeneza mji utakomfaa yeye na familia yake baada ya kupoteza nguvu mwilini mwake. Kuuchezea ujana wako leo ni sawa na kujikaribishia matatizo uzeeni mwako. TAFAKARI KWA KINA Ujana ni wazimu ni vyema ukatumia dawa za kutibu wazi huu
 
Ukiona mtu anaemiliki mali na cheo lakini jicho linatoka machozi kwa kukosa furaha ya nafsi hapo ndio unapotakiwa kuamini na kuthibitisha kuwa pesa sio kila kitu katika maisha ya binadamu. Matatizo ya ndoa yananoga kuyasikia kwa mwenzio tu ila wewe yasikupate. Yakikupata unaweza kujihisi upo kingugi hata kama unaishi london. Kamwe uwepo wa sehemu yoyote bora unayoishi utakuwa na maana kama unapokea penzi la dhati kutoka kwa mwenza wako. Lakini kama kila kukicha vita na matusi tu ndani ya ndoa nivigumu kuona thamani ya sehemu uliokuwepo hata iwe na raha kiasi gani. Nimekuwa nikipokea jumbe nyingi za kuombwa ushauri kuhusu matatizo ya ndoa. Wengi wao katika hao ni wanawake tena mabinti wadogo sana. Inasikitisha kuona mtu anakueleza mambo mazito mazito anayofanyiwa na mume wake ya udhalilishaji, na hajui ufumbuzi wa tatizo lilomfikia wapi pakuanzia. Mume anafikia hatua ya kwenda kuzaa nje ya ndoa na rafiki wa mke wake na ile hali anajua wazi kuwa huyu ninaezaa nae ni rafiki wa mke wangu. Huu ni unyama mkubwa sana ambao hautakiwi kuvumiliwa kabisa. Kama mwanamke umemchoka ni bora ukampa talaka aendelee na maisha yake kuliko kumtia majeraha mazito kama haya kwenye moyo wake. Lengo la kuitwa binadamu na alietuumba sio kutesana na kunyanyasana. Tumeitwa binadamu nineno la kiarabu lenye maana(Sisi wote ni watoto wa mtu mmoja anaeitwa adamu) hivyo basi hatupaswi kufanyiana unyama kwenye maisha yetu. Ila inatupaswa kupendana kuheshimiana pamoja na kusaidia panapohitajika msaada. Kumnyanya mwanamke aliekubali kukuonesha mwili wake kwa dhamana ya pendo, nisawa na kujifungulia milango ya laana tu mbele ya muumba wako. TAFAKARI KWA KINA Ogopa kuolewa na mtu husiemjua katika maisha
 
Utamaduni wa kufanya mazoezi wengi wetu tumekuwa tukiiupuuzia sana na kuona labda unawahusu watu fulani hivi katika maisha. Lakini ukweli utabaki kuwa mazoezi ni tiba kubwa sana kwa maradhi mengi ambayo yanamuinda mwanadamu. Maradhi mengi tumekuwa tukiyapata kwa mifumo mibaya ya maisha tunayoishi nayo. Mtu anaamka asubuhi kabla hajatia kitu kinywani kwanza anakimbilia pakti la sigara au bangi na kuanza kuvuta. Mfumo wa maisha wa aina hii sio rafiki kabisa na afya yako wakati wowote tarajia anguko la afya. Tumejengeka kuwa vyakula bora ni vile vilivyopikwa kwa mafuta mengi na marosti shatashata. Kumbe si kweli hivyo ndio vyakula hatari sana kwenye maisha yetu japo kuwa tunaviona ndio vyakula bora na vyenye hadhi ya juu. Wataalamu wanatueleza kuwa mazoezi umsaidia mtu kuhimarisha misuli ya ubongo wake. Pia huufanya mwili kuwa na nguvu zaidi na kuwa na umbile lenye mvuo. Maradhi mfano wa sukari licha kuwa visababishi vipo vingi kwa mujibu wa majarida ya afya. Lakini kutofanya mazoezi napo kunasababisha maradhi mazito kama haya. Mazoezi hayana umri wala tabaka la watu fulan ndio walengwa hapana. Mazoezi kila mtu anawajibika nayo uwe mzee,kijana au hata mjaamzito, wote wanapaswa kujitahidi kufanya mazoezi kwa uchache hata dakika thelathini tu kwa siku. Afya aliokupa Mungu ni vyema ukaitunza na kuithamini kwa dhati ya thamani maana kuna wengine hawana. TAFAKARI KWA KINA Mazoezi ni muhimu
 
Kuna aina fulani ya ndoa inaitwa(Marriage slavery)ndoa hii ni matokeo ya watu kuowana bila kupendana au ndoa za kulazimishwa na wazazi. Ifahamike kuwa mapenzi ni uhuru wa mtu binafsi kwenye moyo wake, hivyo anahaki ya kumchagua mtu anaemuona yeye sahihi ndani ya moyo wake na si kumlazimisha wa kumpenda. Kumlazimisha mtoto wako kuolewa na mtu unaempenda wewe na si yeye ni sawa na kuzibaka tu hisia zake. Ndoa yenye utumwa mara nyingi uzalishwa na tabia kama hizi za kuingia kwenye ndoa na mtu ambae moyo wako haujampenda. Matokeo yake nyumba inakuwa kama mahabusu kila kukicha matusi na vita. Kuolewa kwa ajili ya kuridhisha watu ni hatari sana katika ulimwengu wa mahusiano. Kwasababu moyo wako huwa haupo huru kufurahikia ndoa yako bali wewe unafanya kwa ajili ya kuridhisha watu wako na kukwepa aibu. Ogopa sana kuolewa kwa msukumo wa kitu chochote au mali. Kumbuka kuwa mali haina uwezo wa kutunza penzi la dhati kwenye moyo wa mtu. Ndoa nyingi siku hizi zinagharamikiwa harusi zake. Yani ukunbi mkubwa mc na vyakula paka vinamwagwa ila ukija kuwatizama hao wanandoa hawana maarifa yoyote kuhusu ndoa yao. Kukosa maarifa kuhusu ndoa ndio usababisha watu wengi kuingia kwenye utumwa wa mapenzi. Mume hamjali mke wake na mke hana heshima mbele ya mume wake. Nyumba imejawa na vita kila wakati kiasi ambacho paka majirani wanajua tabia yenu ya kugombana gombana. Ndoa ya aina hii sio salama kabisa kwa ustawi wa watu wema wenye adabu na hekima. TAFAKARI KWA KINA Utumwa haufai kuuridhia kwenye ndoa.
 
Siku zote ukimjenga mtoto wako kwenye misingi mizuri lazima ataleta matokeo mazuri na yenye natija. Mtoto inabidi ajengwe upendo juu ya ndugu zake na jirani zake. Kwasababu ndani ya upendo ndio huwa kumebeba huruma na usawa. Kumfundisha mtoto kibri na choyo ni sawa na kuharibu ustawi wa maisha yake. Mzazi anapaswa kumlea mtoto wake kwenye malezi yenye kujenga na yenye faida kwake binfsi na jamii kwa ujumla. Mvunze mtoto wako wa kiume kuwa yeye ni kama baba yako. Hivyo basi anawajibu wa kusoma kwa bidii na anawajibu wa kukutunza wewe mzazi wake na ndugu zake kwa ujumla. Lizoeshe jina la baba kwa mtoto wako wa kiume mara kwa mara. Hii itamjenga ukaribu mtoto wa kuwa na wewe wakati wote pia na kukuthamini zaidi. Jiepushe sana na kumkashifu mtoto na kumwambia maneno yasiofa. Mfano mtoto wako wa kiume kakosea kitu unamwambi"Wewe shoga kazana wewe kuna jela utakaza" maneno haya na yenye mfano kama haya hayatakiwi kulelewa nayo mtoto kabisa. Waswahili wanasema"Nyimbo mbaya habebembelezewi mtoto" wakiwa na maana maneno mabaya na machafu kama hayo si busara kabisa kumpachika nayo mtoto. Mzazi unatakiwa wewe ndio uwe mstari wa mbele kupinga maneno mabaya kuitwa mtoto wako na watoto wa mwenzako. Lakini sio wewe tena ndio unakuwa kinara wa maneno mabaya na machafu kwa mtoto wako. TAFAKARI KWA KINA Malezi bora ujengwa hayaji kwa bahati.
 
Siku zote mwenye kukosea njia huwa ngumu sana safari yake kutimia. Mfano wa maisha yetu ni kama mtu aliekuwa safarini, misukosuko,vishindo na hata vitisho vyote hana budi msafiri kuvipokea. Kwasababu lengo na tamanio la msafiri yoyote huwa anahitaji afike salama kwenye safari yake. Bila shaka kila mtu anatamani mafanikio katika maisha yake, lakini ukweli ni kwamba hakuna mafanikio ambayo yanakosa njia zake maalumu tufahamu kuwa kila mafanikio lazima yafate njia zake. Jonatha conneely kwenye kitabu chake cha (The secret to real success) amendika njia nne ambazo mtu yoyote anaetaka mafanikio akizifata anaweza akapata moja kati ya mawili. Anaweza akafanikiwa kwa asilimia mia moja au hata akapata nusu ya hitajio lake katika mafanikio. Njia hizo ameziita kama "Four keys to success" funguo nne za mafanikio. (Four keys to success) 1 CHAGUA UNACHOTAKA NA WAPI UNATAKA KUWA (Huwezi kupata mafanikio kama haujui unataka mafanikio kwenye jambo gani. Lazima ujue jambo maalumu ambalo kwenye jambo hilo ndio utafanikiwa. Mfano unataka kufanikiwa kwenye nini? Elimu,Biashara au tabia. Sasa ili ufanikiwe hakikisha unajua je unataka kufanikiwa katika jambo gani.) 2 WEKA KIKOMO CHA MPANGO WAKO WA MAFANIKIO (Hapa anakusudia lazima ujiweke mda maalumu wa mwisho wa mafanikio yako. Yani kama vile kusema"Ikifika January 20/2019 nataka niwe nimeshajenga nyumba yangu" maneno haya yatakusaidia kuwa na juhudi kwenye kazi zako ili ufike tu kwenye lengo lako kabla ya mda ulojiwekea. Lakini unapoweka tu wazo kichwani bila deadline ni ngumu kufanya jambo kwa dhati na kwa msukumo.) 3 ANZA HATUA KATIKA LENGO LAKO UNALOTAKA (Watu wengi wamekuwa waoga sana kuanza kuchukuwa hatu pindi tu wanapoweka mpango wa mafanikio. Yani unakuta mtu anawazo zuri la biashara na kashalifanyia utafiti kaona hasa kuwa akianza biashara hiyo itamlipa. Lakini tatizo lipo kwenye kuanza ndio anapositasita na kuona kuwa hatofanikiwa. Kanuni za mafanikio zinataka uwanze kufanya katika lengo lako hii itakusaidia kupiga hatu zaidi. Wazo bila utendaji ni sawa na mboga bila chumvi hailiki.)
 
Siku zote mafanikio huwa yanaletwa na wazo la unachotaka kufanikiwa. Kamwe huwezi kufanikiwa kama hauna wazo kichwani la hicho unachotaka kufanikiwa. Lazima ujue unataka kufanikiwa kwenye nini au jambo gani?. Wataalamu wa mafanikio wanasema kuwa si lazima ulete wazo lako jipya kwenye jambo unalotaka kufanikiwa,wakati mwengine unaweza kuchukuwa wazo la mtu mwengine na ukaliboresha likawa hai kwa mafanikio. Mfano unaweza kumsikia mtu anatamka wazo lake mbele za watu kuwa anataka kufanya biashara ya matunda. Unachotakiwa kukifanya baada ya kupata wazo hili kutoka kwa mtu ni wewe kuboresha hilo wazo na kuanza utekelezaji mara moja. Kama yeye alikuwa anataka kufanya biashara ya matunda bila kuweka kwenye pakeji nzuri basi wewe weka kwenye pakeji nzuri ambayo itamvutia na kumfurahisha mteja. Tatizo si kuwa hakuna biashara za kufanya ila tatizo ni ubunifu kwenye biashara ambazo tunazifanya. Watu wengi hawana ubunifu kwenye biashara zao, unakuta mteja anakwenda kununua bidhaa kwa mfanya biashara yule mfanyabiashara baada ya kumjali na kumvuta mteja ili kesho aje tena na awashawishi wengine waje kwenye biashara yake, ndio kwanza mwenye biashara anamkasirikia mteja na kumtukana matusi ya nguoni. Kwahiyo tatizo letu ni ubunifu ndio kitu ambacho kinachofanya biashara zetu zikateketea mara kwa mara. Chukuwa karoti zako na nyanya zioshe kwa maji safi kisha ziweke kwenye kitenga zikauke maji. Kisha anda mifuko yako au pakeji zako za kisasa kwa kuzipanga bidhaa zako kwa ustadi mzuri na mvuto wa aina yake. Ingiza mzigo wako sokoni utajikuta unafanya biashara zaidi kuliko hao waliokutangulia. TAFAKARI KWA KINA Ubunifu ni zaidi ya uchawi kwenye biashara
 
Mfano kama atatokea mtu muda huu na akauuliza swali hili "Je ni kitu gani tukikupa utakuwa na furah?" Naimani majibu yatukuwa mengi sana kuna wengine watasema "Ukinipa pesa nitafurahi", na kunawengine watasema "Ukinipa nyumba na magari nitafurahi", majibu yatakuwa mengi sana. Ila ukweli utabaki kuwa pale pale kuwa furaha ya moyo haitegemei nyumba wala pesa. Furaha ya moyo inategemea sana moyo wenyewe ulivyouzoesha na namna unavyoyapokea mambo katika maisha. Mfano nitakupa kuna watu wakifikwa na matatizo huwa hawawezi kabisa kufikiria utatuzi wa tatizo kwa haraka. Yani wao wakifikwa na tatizo kazi yao kubwa ni kulia na kulaumu watu waliowasababishia matatizo. Sasa kanuni za furaha zinalikataa hilo jambo kwa kiasi kikubwa sana, na zinaeleza kulipokea tatizo kwa mfumo huo ni kuongeza tatizo jengine. Siku zote ili uweze kurudisha furaha nafsini baada ya nafsi kuchafuka kwa jambo lililokusibu, unatakiwa kwanza usilikuze tatizo akilini mwako na kuliona kubwa sana. Yani kama hivi pengine umefukuzwa kazi kazini kwa kosa ambalo si haki wewe kufukuzwa kazi. Unachotakiwa kukifanya ni kulipokea tatizo kwa njia ya busara bila hamaki na hapo hapo uwanze kutafakari je nitarudi vipi kazini kwa kutaka ushauri kwa baadhi ya watu wako wa karibu. Kitendo hichi kitakupa uhuru na fikra mbadala zenye kujenga pia kitakusukuma kufanya maamuzi sahihi. Kwahiyo kikubwa tunachotakiwa kuwa nacho ninamna ya kuyapokea mambo na jinsi ya kuyatatua, hapa viwango vya furaha havitopungua ndani ya mioyo yetu. TAFAKARI KWA KINA Furaha ni chimbuko la namna unavyo yapokea mambo
Kweliiii kabisaaa...thanks
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom