Makapuku Forum

Kiungi wa Kati wa Manchester City, Kevin de Bruyne, 27,anajiandaa kurejea uwanjani baada ya kupona jeraha alilopata wakati wa mchuano wa City dhidi ya Burnley Oktoba 20 baada ya klabu hiyo kuhofia kumchezesha kingo huyo wa kimataifa wa Ubelgiji mjini Liverpool siku ya Jumapili.(ESPN)
 
Aston Villa imehusishwa na uhamisho wa mwezi Januari wa mshambuliaji wa Chelsea Callum Hudson-Odoi wa miaka 17. (Birmingham Mail)
 
Manchester City, Tottenham na Southampton wamekuwa wakimfuatilia mshambuliaji wa Sunderland Josh Maja mwenye umri wa miaka 19. (Mirror)
 
Daktari wa Liverpool Matt Konopinski anatarajiwa kuiacha klabu hiyo na kuenda England kuchukua wadhifa mpya baadaya ya kuwa Anfield kwa muda mrefu. (Liverpool Echo)
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…