Makapuku Forum

Kila mtu abaki na simu yake
Sema wanaume za kwao ni zao za wenzao ni zao
 
Mdukuzi kutoka nchini Taiwan amesema ataifuta akaunti ya Mark Zuckerberg.

Mdukuzi huyo anayefahamika kwa jina moja la Chang alishawahi kushitakiwa na dereva wa basi nchini humo kwa kosa la kudukua mfumo wa tiketi na kujiwekea bei ya tiketi ya dola 0.03 (takribani shilingi 68).

Hii si mara ya kwanza kwa Mark Zuckerberg kudukuliwa akaunti yake, mwaka 2011 akaunti yake ilidukuliwa na mtu ambaye aliandika "Let the hacking begin" kwenye ukurasa wa Mark Zuckerberg ambaye ndiye muanzilishi na mkurugenzi wa mtandao wa Facebook, hii ilifuatiwa na uamuzi wa Facebook kufuta jumbe zote binafsi za Zuckerberg kwenye akaunti yake kwa kuhofia udukuzi mwingine unaweza ukafanyika kwake au kwa kampuni.
 
Google wanawalipa Apple dola bilioni 9 (sawa na trilioni 20 za Tanzania) kwa mwaka ili waendelee kubakia kama chaguo-msingi la utafutaji kwenye kivinjari wavuti cha Safari kilichomo kwenye simu za iPhone.

Hivyo kama wewe ni mtumiaji wa Google kwenye simu za Apple basi tambua Google wanatoa dola bilioni 9 kila mwaka ili wewe uendelee kutafuta vitu kwa Google kwenye simu za Apple.
 
Inasemekana Apple wataingiza pesa nyingi kwa kila iPhone Xs itakayouzwa. Gharama ya kutengeneza iPhone Xs moja ni dola 443 (1,000,000) huku bei ya kuuzia iPhone Xs ni dola 1,249 (3,000,000) ikiwa na GB 256.
 
Mke wa rais wa Marekani Donald Trump amewasili Ghana katika hatua ya kwanza ya ziara yake ya kwanza barani Afrika.

Melania alizuru hospitali ya watoto ya Accra na akaahidi ufadhili kupitia kwa USAID.

Melania atasalia Ghana kwa siku mbili kabla ya kuelekea Malawi Kenya na kisha Misri
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…