Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mcheshi nguli Bill Cosby raia wa Marekani amehukumiwa kifungo cha kati ya miaka 3 - 10 gerezani.

Cosby ameshtakiwa kwa dhuluma za kimapenzi dhidi ya bi Andrea Constand mfanyikazi wa chuo kikuu kimoja nchini Marekani.

Kosa hilo yamkini lilifanyika mwaka wa 2004. Bi Andrea aliishawishi mahakama kuwa Cosby alimpa dawa aina ya Quaaludes ambayo ilimlegeza na hakuweza kumzuia kumbaka mwaka wa 2004.
Screenshot_20180926-084241.jpeg
 
Mkuu wa Umoja wa Ulaya anayehusika na sera za Kigeni, Federica Mogherini, ametangaza kwamba muungano wa Ulaya utaanzisha shirika la kisheria kudumisha biashara na Iran wakati Marekani itakapoweka tena vikwazo dhidi ya Iran.

Katika mkuano uliofanyika mjini New York, nchi zilizosalia katika makubaliano ya nyuklia yaliyofikiwa mwaka 2015, zimesema zimeazimia kuanzisha mbinu ya malipo ili kuendeleza biashara.

Bi. Mogherini ameongeza kuwa wataalam wa kiufundi, watajadili suala hilo kwa kina.

Thamani ya sarafu ya Iran, imeathirika pakubwa kutokana na sera mpya ya Marekani
Screenshot_20180926-084356.jpeg
 
  • Thanks
Reactions: Obe
Waanzilishi wa mtandao wa kijamii wa Instagram, Kevin Systrom na Mike Krieger wamejiuzulu.

Systrom ambaye amekuwa mkurugenzi mkuu mtendaji wa Instagram tangu kuasisiwa amesema wanajiondoa ilikufufua ubunifu wao upya.

Wawili hao walisalia katika bodi ya usimamizi wa Instagram hata baada ya kununuliwa na Facebook mwaka wa 2012 kwa gharama ya dola bilioni moja.
Screenshot_20180926-084510.jpeg
 
Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kuanzia Oktoba Mosi itaanza kutoza tozo ya ulinzi TZS 11,425 ($5) kwa wasafiri wa nje, na 4,570 ($2) kwa wasafiri wa ndani ili kuimarisha ulinzi na usalama katika viwanja vikubwa.
Hatua hiyo imekosolewa kuwa, huenda ikapunguza wateja.
Screenshot_20180926-084700.jpeg
 
Export Development Canada (EDC) imejitoa katika mpango wa kuifadhili Uganda kununua ndege nne mpya aina ya CRJ-900s kutoka Kampuni ya Bombardier kutokana na sababu za kifedha.

EDC ilikuwa imeahidi kutoa TZS bilioni 247 ($ 108 milioni) kwa ajili ya ununuzi
Screenshot_20180926-084824.jpeg
 
Mwanamke mmoja nchini Kenya amefikishwa Mahakamani Nakuru kwa tuhuma za kumwambukiza Virusi vya UKIMWI mtoto wa miezi 9 wa jirani yake, baada ya kumnyonyesha.

Imeelezwa kuwa, mtoto alikuwa analia, na katika kumbembeleza, mwanamke huyo anayeishi na Virusi vya UKIMWI akamnyonyesha.

Dah inasikitisha sana alishindwa kumbembeleza kwa njia nyingine au hata kumchemshia uji
Screenshot_20180926-085004.jpeg
 
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro amezipiga marufuku kampuni zote za udalali wa viwanja kutokufanya kazi wilayani humo, mpaka zitakapopata maelekezo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya.

Lengo ni kukabiliana na ongezeko la uuzwaji wa ardhi za vijiji pasipo kufuata
Screenshot_20180926-085149.jpeg
 
"Kijijini pale watu hatuvai viatu, nilipata viatu (raba) nilipotoka jandoni.

Nilipokwenda nazo shule, mwalimu akaniambia hivi, kesho usije na viatu, kila mtu hana viatu hapa."- Rais Mstaafu Dkt JM Kikwete akielezea sehemu ya kitabu kinachohusu
Screenshot_20180926-085257.jpeg
 
Mahakama ya Katiba nchini Uganda imetupilia mbali ombi lililoitaka mahakama hiyo kutamka kuwa, ni kosa mwanaume kuoa mwanamke zaidi ya mmoja.

Ombi hilo liliwasilishwa mahakamani hapo miaka 8 iliyopita na asasi isiyo ya kiserikali ya kutetea haki za wanawake
Screenshot_20180926-085404.jpeg
 
Serikali ya Rwanda imepitisha sheria mpya ya madini inayolenga kuondoa wachimbaji wadogo wadogo, kutokana na gharama ya kupata kibali kupanda hadi TZS bilioni 18 kutoka TZS milioni 183.

Kusudio la hatua hiyo, ni kupata wawekezaji wakubwa wenye teknolojia isiyoathiri
Screenshot_20180926-085501.jpeg
 
images%20(2).jpg


Najiandaa kuanza kuwaleteeni makala zangu kule Jamii Intelligence, i hope Makapuku wenzangu mtanipa ushirikiano wa hali na mali.

The Book

From,
The Intelligence Corridor.(TIC)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom