Ulimwengu ni sehemu pana iliyojawa na siri nyingi nzito ambazo sisi binadamu tuliokuwa kwenye hiki kidunia chetu kidogo hatutoweza kuja kuzifahamu bali sehemu ndogo sana ya siri hizo tena kwa kupitia darubini kubwa kama Hubble Space Telescope iliyokuwa huko angani ambayo inazidi kutuonesha maajabu ya ulimwengu kwa mfano kama hii picha ambayo imepigwa hivi karibuni na darubini hiyo.
Picha hii unaweza ukasema imechorwa au kitu ambacho kimetoka kwenye filamu ila si kweli bali ni picha halisi iliyopigwa huko nje ya Dunia na kila kitu unachokiona hapo kipo kweli.
Kwenye picha hii kuna mkusanyiko wa galaksi kila moja wapo imebeba nyota ambazo kila moja inazungukwa na sayari, miezi, mawe na uchafu mwingine.
Je? kati ya hizo nyota ni ngapi ambazo zinaweza kuwa na viumbe hai (Aliens)? hatujui na hatutokuja kujua kamwe kwa sababu kama tukisema tuanze safari ya kwenda huko sasa, hiyo ndege itatumia miaka 100,000,000,000,000,000,000,000,000,000,000,000,000 mpaka kufika huko