Numbisa
JF-Expert Member
- Dec 12, 2016
- 348,121
- 1,249,297
Kwenye suala la uwindaji simba hupenda kuwinda nyati kwakuwa nyati hana spidi sana na ni kitoeo kikubwa na nyati mmoja hukalishwa chini na simba 4,5...sasa simba huyu anayeanza kubalehe ataweza kumkalisha nyati ? La hasha
Simba hawindi swala ni aghalabu sana simba kuwinda swala sababu swala ana mbio sana na simba hana mbio za kumkimbiza swala huwa inatokea simba anavizia kwa kunyata mpaka ahakikishe amefika mita 3 au 2 ndio amstukize swala..chakula kingine cha simba ni nyumbu na pundamilia
Kwakuwa simba huyu alikuwa anashiriki na mama ,shangazi ,Dada zake kwenye kuwinda basi instincts za kuwinda anazijua ila simba huwa wanapenda kuwinda kwa ushirikiano na yeye yupo pekee yake hapa ndio shida ilipo.
Kama simba dume walizaliwa 2 basi hufukuzwa pamoja na simba ndugu huwa wanapendana sana hivyo inakuwa bahati simba hawa watashirikiana kwa kila kitu kwenye kuwinda ,kupigana na adui nk na kama yupo pekee yake basi ataishi maisha yake kwa uangalifu na ugumu kiasi labda itokee akutane na simba dume mwingine aliyefukuzwa na mzee wake na wataunda timu moja na sababu kubwa ni kwaajili ya kuwinda ,ushirikiano wao utakuwa umekutanishwa na lengo moja kuwinda na watakaa pamoja kwa muda kidogo na baada ya muda kila mmoja atachukua hamsini zake.
Maisha yataenda hivyo mpaka atakapofikisha miaka 5 hapo atakuwa shababi haswa na atakuwa na misuli mikubwa na nywele nyingi hata ukimuona lazima utetemeke ,akikutana na koo ya fisi wapatao 15 lazima fisi hao watimue mbio wote ,mngurumo wake husikika kwa umbali wa mile kadhaa.
Kwa umri huu aliofikisha simba huyu anakuwa kivuruge chochote humwambii yupo kwenye peak yake ,akimuona simba jike pekee yake ataenda kumtongoza na simba jike huyo hatomkubalia kirahisi kwanza atampima ubavu je yupo fiti ,je ataweza kumlinda yeye na watoto ,akisha thibitisha hilo ndio ataruhusu kuwa nae na hapo watafanya mapenzi sana hata mara 35 kwa siku .
Simba huyu asipopata jike maana ni aghalabu sana kumuona simba jike awe pekee yake basi atatakiwa aingie kwenye eneo linalomilikiwa na simba na hapo watapigana na akishinda atalimiliki hilo eneo na jike waliokuwepo na kama jike atakuwa na watoto basi atawaua wale watoto wake ili aweke damu yake na genes zake na endapo akipigwa basi atapigika kiukweli na kuumizwa vibaya na kutimuliwa.
Endapo akishinda pambano simba anayemiliki eneo ataondoka na simba huyu atajitawalia eneo hilo na ataweka alama ili simba yeyote mvamizi akitokea apate onyo hii sehemu ni hatari hupaswi kuwepo.,endapo wakizaa watoto na jike basi wataitwa pride na simba jike huwa wanaenda kuwinda huku dume akiondoka zake kwenda kutizama mipaka na hutembea mile kuhakikisha hakuna mvamizi yeyote anaingia kwenye ardhi yake kisha ana nguruma na mngurumo huo husikika kwa umbali wa mile kadhaa kama kutoa tahadhari kwa madume wengine kuwa eneo fulani kuna mfalme hivyo haipaswi kuingia na kama kuna dume karibu haswa wadogo au wasio tayari kupambana basi huondoka zao ,simba dume huyu akishafanya patrol ya eneo lake huweka alama ili hata dume yeyote akikatiza kwa bahati mbaya apate tahadhari na onyo hilo kisha hurudi kwa familia yake na jike wakishawinda wa kwanza kula ni dume na ukiwa mbishi utakutana na kisago sababu huyu dume hufanya kazi kubwa hivyo lazima ale ashibe
Simba dume maisha yake yote hutegemea nguvu ,ndio maana kila siku anakagua eneo lake na kutoa tahadhari kwa simba wengine lakini lazima akumbane na misukosuko wapo simba dume ni mabachelor nao wanataka familia na msosi wa bure na njia rahisi ni kuvamia eneo la pride na kupigana na dume mpaka kieleweke ,simba hutofautiana wapo wanaotembea kindugu wawili wawili haswa waliozaliwa tumbo moja hawa wanapovamia eneo linalomilikiwa na simba mmoja ni rahisi wao kushinda na eneo linalomilikiwa na simba dume 2 ni vigumu kupokwa na wavamizi.
Siku zote mapambano ya simba dume kugombea na kulinda eneo huleta maafa makubwa;
1.simba wanapopigana hukimbilia kung'ata na kunyofoa mapumbu na simba aliyenyofolewa mapumbu hushindwa tena kuzalisha na kusambaza damu yake ,
2.simba anayeshindwa huwa anaumizwa vibaya sana mithili ya mtu aliyegongwa na fuso na wengi hufa sababu simba ni mbishi,hakati tamaa kwenye kupigana
3.endapo simba mvamizi akishinda pambano basi vitoto vyote huuliwa labda mama simba akiona mumewe kazidiwa hukimbia na watoto na kuwaacha majike wengine ambao watatawaliwa na simba mpya huyo
Haya ndio maisha ya simba dume hakuitwa mfalme wa nyika kwa bahati mbaya ,simba humiliki mile kadhaa za eneo wanyama wote nyati,nyumbu,pundamilia,twiga na hata tembo ni wa kwake sasa ole wake simba mwingine au fisi ajipendekeze kwenda kuwinda eneo lake atauliwa kama sio kujeruhiwa
Simba maisha yake mengi hutawaliwa na hofu ya kupinduliwa ndio maana mwanaye wa kiume akifikisha miaka 2 humfukuza ,jihadhari sana kuingia kwenye territory ya simba hautobaki salama bora ukutane na jike kuliko dume utararuriwa tu.
Simba hawindi swala ni aghalabu sana simba kuwinda swala sababu swala ana mbio sana na simba hana mbio za kumkimbiza swala huwa inatokea simba anavizia kwa kunyata mpaka ahakikishe amefika mita 3 au 2 ndio amstukize swala..chakula kingine cha simba ni nyumbu na pundamilia
Kwakuwa simba huyu alikuwa anashiriki na mama ,shangazi ,Dada zake kwenye kuwinda basi instincts za kuwinda anazijua ila simba huwa wanapenda kuwinda kwa ushirikiano na yeye yupo pekee yake hapa ndio shida ilipo.
Kama simba dume walizaliwa 2 basi hufukuzwa pamoja na simba ndugu huwa wanapendana sana hivyo inakuwa bahati simba hawa watashirikiana kwa kila kitu kwenye kuwinda ,kupigana na adui nk na kama yupo pekee yake basi ataishi maisha yake kwa uangalifu na ugumu kiasi labda itokee akutane na simba dume mwingine aliyefukuzwa na mzee wake na wataunda timu moja na sababu kubwa ni kwaajili ya kuwinda ,ushirikiano wao utakuwa umekutanishwa na lengo moja kuwinda na watakaa pamoja kwa muda kidogo na baada ya muda kila mmoja atachukua hamsini zake.
Maisha yataenda hivyo mpaka atakapofikisha miaka 5 hapo atakuwa shababi haswa na atakuwa na misuli mikubwa na nywele nyingi hata ukimuona lazima utetemeke ,akikutana na koo ya fisi wapatao 15 lazima fisi hao watimue mbio wote ,mngurumo wake husikika kwa umbali wa mile kadhaa.
Kwa umri huu aliofikisha simba huyu anakuwa kivuruge chochote humwambii yupo kwenye peak yake ,akimuona simba jike pekee yake ataenda kumtongoza na simba jike huyo hatomkubalia kirahisi kwanza atampima ubavu je yupo fiti ,je ataweza kumlinda yeye na watoto ,akisha thibitisha hilo ndio ataruhusu kuwa nae na hapo watafanya mapenzi sana hata mara 35 kwa siku .
Simba huyu asipopata jike maana ni aghalabu sana kumuona simba jike awe pekee yake basi atatakiwa aingie kwenye eneo linalomilikiwa na simba na hapo watapigana na akishinda atalimiliki hilo eneo na jike waliokuwepo na kama jike atakuwa na watoto basi atawaua wale watoto wake ili aweke damu yake na genes zake na endapo akipigwa basi atapigika kiukweli na kuumizwa vibaya na kutimuliwa.
Endapo akishinda pambano simba anayemiliki eneo ataondoka na simba huyu atajitawalia eneo hilo na ataweka alama ili simba yeyote mvamizi akitokea apate onyo hii sehemu ni hatari hupaswi kuwepo.,endapo wakizaa watoto na jike basi wataitwa pride na simba jike huwa wanaenda kuwinda huku dume akiondoka zake kwenda kutizama mipaka na hutembea mile kuhakikisha hakuna mvamizi yeyote anaingia kwenye ardhi yake kisha ana nguruma na mngurumo huo husikika kwa umbali wa mile kadhaa kama kutoa tahadhari kwa madume wengine kuwa eneo fulani kuna mfalme hivyo haipaswi kuingia na kama kuna dume karibu haswa wadogo au wasio tayari kupambana basi huondoka zao ,simba dume huyu akishafanya patrol ya eneo lake huweka alama ili hata dume yeyote akikatiza kwa bahati mbaya apate tahadhari na onyo hilo kisha hurudi kwa familia yake na jike wakishawinda wa kwanza kula ni dume na ukiwa mbishi utakutana na kisago sababu huyu dume hufanya kazi kubwa hivyo lazima ale ashibe
Simba dume maisha yake yote hutegemea nguvu ,ndio maana kila siku anakagua eneo lake na kutoa tahadhari kwa simba wengine lakini lazima akumbane na misukosuko wapo simba dume ni mabachelor nao wanataka familia na msosi wa bure na njia rahisi ni kuvamia eneo la pride na kupigana na dume mpaka kieleweke ,simba hutofautiana wapo wanaotembea kindugu wawili wawili haswa waliozaliwa tumbo moja hawa wanapovamia eneo linalomilikiwa na simba mmoja ni rahisi wao kushinda na eneo linalomilikiwa na simba dume 2 ni vigumu kupokwa na wavamizi.
Siku zote mapambano ya simba dume kugombea na kulinda eneo huleta maafa makubwa;
1.simba wanapopigana hukimbilia kung'ata na kunyofoa mapumbu na simba aliyenyofolewa mapumbu hushindwa tena kuzalisha na kusambaza damu yake ,
2.simba anayeshindwa huwa anaumizwa vibaya sana mithili ya mtu aliyegongwa na fuso na wengi hufa sababu simba ni mbishi,hakati tamaa kwenye kupigana
3.endapo simba mvamizi akishinda pambano basi vitoto vyote huuliwa labda mama simba akiona mumewe kazidiwa hukimbia na watoto na kuwaacha majike wengine ambao watatawaliwa na simba mpya huyo
Haya ndio maisha ya simba dume hakuitwa mfalme wa nyika kwa bahati mbaya ,simba humiliki mile kadhaa za eneo wanyama wote nyati,nyumbu,pundamilia,twiga na hata tembo ni wa kwake sasa ole wake simba mwingine au fisi ajipendekeze kwenda kuwinda eneo lake atauliwa kama sio kujeruhiwa
Simba maisha yake mengi hutawaliwa na hofu ya kupinduliwa ndio maana mwanaye wa kiume akifikisha miaka 2 humfukuza ,jihadhari sana kuingia kwenye territory ya simba hautobaki salama bora ukutane na jike kuliko dume utararuriwa tu.