Muziki: Pona Haraka
...unaweza ukadhani huumwi, kila mtu na maradhi yake, maradhi yangu siyo yako na siku zote homa sio malaria , kaa unalijua hili na kama ndo unalisikia leo basi usiache kupokea salamu yangu ya upendo kwako wewe Kapuku unayelifanya Jukwaa hili kutochusha. Asante
Shunie kwa Je Wajua, imeandikwa kwa lugha rahisi sana kiasi kwamba hata ambaye moja haiingii mbili haikai (hayumo humu MF) nikimpelekea asome ataelewa na kuongeza maarifa.
Maradhi yako yasisumbue wengine bila taarifa, ukitaka yatusumbue basi tujulishe mapema, huu ni mwaka tofauti, mwaka wa roho mbaya kama sikupendi na kinyume chake. Hivi ninaandika nini, hiki si kipengele cha muziki na kesho ni furahiday...anyway, tuna tofauti, furahia maradhi yako kama daktari yuko mbali ishi nayo, ni yako na ninakutakia kupona haraka. Nimechanganya na tafasiri unavyoweza, yaani two in 1 kama twaarabu ya MY mlokole wa kiislam, usiniharibie siku yangu nami nitakaa mbali na siku yako