Makapuku Forum

Makapuku Forum

Leo ni Kumbukumbu ya Siku ya kuzaliwa Rais Mstaafu wa Awamu ya 44 Nchini Marekani Barack Hussein Obama , Anatimiza Miaka 57 Tangu alipozaliwa Huko Honolulu, Hawaii - Marekani na anatimiza Miaka Hiyo akiwa ni Rais wa Kwanza Mwenye asili ya Africa Kuongoza Taifa hilo Kubwa Duniani.


Screenshot_20180804-182834.jpeg
 
Leo ni Kumbukumbu ya Siku ya kuzaliwa Rais Mstaafu wa Awamu ya 44 Nchini Marekani Barack Hussein Obama , Anatimiza Miaka 57 Tangu alipozaliwa Huko Honolulu, Hawaii - Marekani na anatimiza Miaka Hiyo akiwa ni Rais wa Kwanza Mwenye asili ya Africa Kuongoza Taifa hilo Kubwa Duniani.


View attachment 827009
Heri Ya Siku Ya Kuzaliwa Obama
 
Clarence Seedorf ameteuliwa kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya Cameroon akiwa anasaidiwa na Patrick Kluivert.
:
Urefu wa mkataba wa Seedorf na mabingwa wa mara tano wa AFCON, utatangazwa baadae.
.
Seedorf, 42, ambaye amewahi kuvifundisha vilabu vya AC Milan, Shenzhen na Deportivo La Coruna.
Alidumu kwa miezi 6 tu katika kila timu. :
Seedorf, ambaye anachukua nafasi ya Hugo Broos, na atakuwa na angalau mwaka mzima kuiandaa timu kabla ya mashindano ya AFCON 2019.
Screenshot_20180804-183226.jpeg
 
Wakala wa Thibaut Courtois - Christophe Henrotay, amesema mchezaji wake anataka kuondoka Chelsea na kujiunga na Real Madrid - lakini The Blues bado wanaweka ngumu kumuachia..
:
"Nimekuwa nikisoma kila mahala kwamba Chelsea wanasema ni uamuzi wa Thibaut kuondoka au kubaki, lakini mchezaji mwenyewe ameshawaambia kwamba anataka kwenda Madrid.’ Alisema Henrotay.
:
"Uamuzi wa kwenda Madrid pia unachagizwa na matamanio yake ya kuwa karibu na familia yake, na tayari Madrid wameshatuma ofa kwenda Chelsea, sasa uamuzi upo kwa Chelsea.”
:
Zimebaki siku 5 kabla ya dirisha la usajili kufungwa nchini England - Courtois na Madrid wanaombea Chelsea ikubali ofa na kukamilisha uhamisho huo kabla ya Alhamisi.

Screenshot_20180804-183452.jpeg
 
Clarence Seedorf ameteuliwa kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya Cameroon akiwa anasaidiwa na Patrick Kluivert.
:
Urefu wa mkataba wa Seedorf na mabingwa wa mara tano wa AFCON, utatangazwa baadae.
.
Seedorf, 42, ambaye amewahi kuvifundisha vilabu vya AC Milan, Shenzhen na Deportivo La Coruna.
Alidumu kwa miezi 6 tu katika kila timu. :
Seedorf, ambaye anachukua nafasi ya Hugo Broos, na atakuwa na angalau mwaka mzima kuiandaa timu kabla ya mashindano ya AFCON 2019.View attachment 827013
Wamelamba Jike watapigwa Goal hadi wakome ....Jamaa Sio Kocha Bora
 
Mshambuliaji wa Chelsea Álvaro Morata kuanzia msimu ujao atavaa jezi namba 29 badala ya namba 9 aliyokuwa anavaa mwanzoni.

Jezi namba 29 ina maana kubwa Kwa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Hispania kwani tarehe 29 July ni siku ya Birthday ya watoto wake mapacha
Screenshot_20180804-183852.jpeg
 
Mtanzania Jesca Ngisaise (jezi no.12), amepata nafasi ya kuweza kushiriki kwenye BWB Africa Girls All-Star Game inayofanyika Sun Arena Pretoria na kaweza kuonesha uwezo wake kwenye timu aliyoshiriki licha ya timu yake kushindwa kwa tofauti ya pointi 2.
.
Matokeo ni Team Grey point 25 na Team Black point 23.


Screenshot_20180804-184252.jpeg
 
Alikiba ambaye amesajiliwa na Klabu ya Costal Union ya Tanga ameanza Mazoezi na Wachezaji wenzie Siku ya Jana kujiandaa na Msimu Ujao wa VPL unaotarajia kuanza Agosti 22 Mwaka huu.

Unahisi Alikiba anaweza kutamba kwenye Soka kama alivyofanya kwenye Muziki?
Screenshot_20180804-184652.jpeg
 
DODOMA: Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) imetangaza Uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika majimbo matatu na wa udiwani katika kata mbili za Tanzania Bara utakaofanyika Septemba 16, mwaka huu
-
Akitangaza uchaguzi huo leo Agosti 4, Makamu Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mbarouk Salim Mbarouk amesema fomu za uteuzi wa wagombea wa Majimbo hayo zitatolewa kuanzia Agosti 13 hadi 14 mwaka huu na uteuzi utafanyika Agosti 20, 2018
-
Amesema kampeni zitaanza Agosti 21 na kumalizika Septemba 15, mwaka huu
-
Ameyataja majimbo hayo kuwa ni Korogwe Vijijini mkoani Tanga, Jimbo la Ukonga mkoani Dar na Jimbo la Monduli katika Mkoa wa Arusha
-
Uchaguzi huu mdogo wa majimbo matatu na kata mbili za Tanzania Bara, unafuatia uchaguzi mdogo wa Ubunge katika jimbo la Buyungu unaotarajiwa kufanya Agosti 12 pamoja na kata 37 za Tanzania Bara
Screenshot_20180804-185006.jpeg
 
Mshambuliaji wa Chelsea Álvaro Morata kuanzia msimu ujao atavaa jezi namba 29 badala ya namba 9 aliyokuwa anavaa mwanzoni.

Jezi namba 29 ina maana kubwa Kwa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Hispania kwani tarehe 29 July ni siku ya Birthday ya watoto wake mapachaView attachment 827016
Afunge magoli sio kubadili Jezi tu
 
IGP Sirro amesema Jeshi la Polisi nchini limejipanga kikamilifu ili kuhakikisha wahalifu wanaofanya mauaji nchi jirani ya Msumbiji wanadhibitiwa na hawapati nafasi ya kufanya uhalifu wao hapa nchini ambapo Wananchi wametakiwa kuendelea kutoa taarifa za watu wanaowatilia mashaka.
Screenshot_20180804-185515.jpeg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom