Makapuku Forum

Makapuku Forum

Ebu uko tuache na unene wetu
giphy.gif
 
Tafasiri Unavyoweza: Usijidanganye, Umoja Mbele Sawa, Haki na Uwazi Havikai Nyuma!

...kama unalijua hili, ukimya haujawahi kuwa njia sahihi ya kuelezea amani au umoja miongoni mwa wananchi wengi. Ipo dhana na inaonekana kukuzwa zaidi na watawala kuwa kuongea wazo tofauti lenye nia ya kujenga basi muongeaji anahatarisha umoja wa kitaifa (national unity). Siku zote watawala wanafanya yale yatakayowafanya wakae madarakani siku zote (hasa kwa nchi zetu), mifumo wanaitengeneza katika namna hata kama hawako madarakani basi waliopo madarakani watawalinda. Tafasiri unavyoweza.

Neno umoja limekuwa midomoni mwa watawala wote, kuanzia rais, waziri hadi wakuu wa wilaya, ukiwasikiliza wanavyoliongea utasema wanamaanisha. Midomo yao imejaa mate maana wanaongea wameshiba na wanaosikiliza wengi wamevaa mashati kupunguza njaa ya kukosa kazi, elimu bora, miundombinu rafiki ya kijamii na mambo mengine wanayoambiwa yapo hawayaoni. Haki za binadamu zinavunjwa kwa kisingizio cha kuleta maendeleo, haki inaminywa na katiba ya chama iko mbele ya katiba ya nchi, hatufiki kwa ukimya.

Neno umoja wa kitaifa linapotamkwa na kiongozi wa serikali kuwa makini, hata kama umekaa kimya, upe ubongo wako kazi ya kuchambua, usiyaachie masikio kusikiliza tu na kukariri. Mara zote kiongozi yeyote wa serikali aisema kuhusu kudumisha umoja wa kitaifa tambua kwamba anamaanisha mambo yafuatayo, usihoji matendo ya serikali, usihoji matumizi ya kodi yako, usihoji hali duni ya maisha kwa wengi. Ukihoji unaonekana mpinzani na utapata taabu sana. Tafasiri unavyoweza
 
Muziki: Una Thamani Kubwa, Tunza Afya

..ninakusalimia wewe Kapuku ambaye bila kificho (siwezi kusemea pembeni) unalifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo. Haijalishi umeandika nini, ile kujua tu uko hapa basi unachokiongeza hapa ni zaidi ya unavyofikiria. Asante kwa kuendelea kulifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri wewe Tumosa , Shunie , moudgulf , shululu ABJ na kaa ukijua kabisa tunakumiss SHIMBA YA BUYENZE , Transcend , Sakayo , Clkey , Lyon Lee , BlessedHope na wewe ambaye nimesahau kukutaja kwa jina hapa.

Muziki sasa, furahia kwa umakini maana maisha ni haya haya na wala usiyafanye yakawa ya tofauti mno. Tunza afya

 
Muziki wa Mdhamini: Mapumziko Kidogo Muhimu

...kama ilivyo ada, mapumziko yanahitajika sana na hata kama sio yale yaliyopo kisheria au kiutaratibu wakati mwingine ni vizuri kujipa personal space, unaamua kuwa mwenyewe kwa masaa machache, usitumie muda mwingi sana peke yako, kama hutoikaribia kamaba basi utajichua, ninasema tu wala sina nia ya kukufanya ufikirie sana.

Ni udhamini wake Da'Vinci na anadedicate kwa watu wake wa nguvu Shunie Sakayo ABJ na husna muba

 
Muziki: Una Thamani Kubwa, Tunza Afya

..ninakusalimia wewe Kapuku ambaye bila kificho (siwezi kusemea pembeni) unalifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo. Haijalishi umeandika nini, ile kujua tu uko hapa basi unachokiongeza hapa ni zaidi ya unavyofikiria. Asante kwa kuendelea kulifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri wewe Tumosa , Shunie , moudgulf , shululu ABJ na kaa ukijua kabisa tunakumiss SHIMBA YA BUYENZE , Transcend , Sakayo , Clkey , Lyon Lee , BlessedHope na wewe ambaye nimesahau kukutaja kwa jina hapa.

Muziki sasa, furahia kwa umakini maana maisha ni haya haya na wala usiyafanye yakawa ya tofauti mno. Tunza afya

 
Muziki wa Mdhamini: Mapumziko Kidogo Muhimu

...kama ilivyo ada, mapumziko yanahitajika sana na hata kama sio yale yaliyopo kisheria au kiutaratibu wakati mwingine ni vizuri kujipa personal space, unaamua kuwa mwenyewe kwa masaa machache, usitumie muda mwingi sana peke yako, kama hutoikaribia kamaba basi utajichua, ninasema tu wala sina nia ya kukufanya ufikirie sana.

Ni udhamini wake Da'Vinci na anadedicate kwa watu wake wa nguvu Shunie Sakayo ABJ na husna muba

Asantee ankoo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom