Makapuku Forum

Makapuku Forum

We nenda katafute mioto hyo
tapatalk_1528367536799.jpeg
 
Tafasiri Unavyoweza: Jifunze Kipya Kila Wakati

.....sababu kubwa inayonifanya kutembelea hapa na kusoma mengi ni kwa sababu ninajifunza mengi sana kutoka kwenu wadau wa Makapuku na JF kwa ujumla. Kujifunza mengi ni jambo zuri kwa mtu binafsi na jamii kwa ujumla. Bila kujifunza na kujua mengi, kila siku wengi wetu tungekuwa tunatapeliwa zaidi ya tunavyotapeliwa sasa. Kujifunza mambo mapya ni nzuri kwa afya ya ubongo pia huongeza furaha. Ujinga ni kutokuona miti kwenye pori. Tafasiri unavyoweza.

Usijedhani kujifunza kitu ni jambo rahisi, linahitaji gharama na nyingi si gharama ndogo, kwa mfano, unahitaji muda kuingia humu JF, unahitaji bando na vitu kama simu, ni. Unaweza kujifunza kwa kutembea pia, unajipa nafasi ya kuona mengi. unajifunza kwa kuuliza ili ufahamu, unajifunza pia kwa kuwafunza wengine. Na unajifunza zaidi kwa kusoma machapisho na hapa ndo kuna shinda. Ndiyo, ipo shida kwenye kusoma na kujisomea.

Ni ukweli kuwa maarifa unaweza kuyapata kwa kuangalia (observing) lakini ukijisomea vitabu na majarida/mitandao kama huu wetu basi nafasi ya kujifunza mengi ni kubwa kuliko kukaa bila kusoma. najua wapo tunaoogopa au hatupendi maneno (words) marefu. Binafsi navutiwa kusoma kama ni kitabu basi maneno yaliyokaa kama ushairi fulani hivi, mafupi mafupi sio marefu maana hunipa uoga wa maneno marefu kwa lugha nyingine ninaogopa maneno marefu (hippopotomonstrosesquippedaliophobia)

Kwako wewe mwanaKapuku, usichoke kujifunza na kutunza wengine maana unaupa ubongo wako furaha na kutuongezea maarifa wengine kila siku. Tukutane wiki ijayo
 
Asante sana binamu yangu
Tafasiri Unavyoweza: Jifunze Kipya Kila Wakati

.....sababu kubwa inayonifanya kutembelea hapa na kusoma mengi ni kwa sababu ninajifunza mengi sana kutoka kwenu wadau wa Makapuku na JF kwa ujumla. Kujifunza mengi ni jambo zuri kwa mtu binafsi na jamii kwa ujumla. Bila kujifunza na kujua mengi, kila siku wengi wetu tungekuwa tunatapeliwa zaidi ya tunavyotapeliwa sasa. Kujifunza mambo mapya ni nzuri kwa afya ya ubongo pia huongeza furaha. Ujinga ni kutokuona miti kwenye pori. Tafasiri unavyoweza.

Usijedhani kujifunza kitu ni jambo rahisi, linahitaji gharama na nyingi si gharama ndogo, kwa mfano, unahitaji muda kuingia humu JF, unahitaji bando na vitu kama simu, ni. Unaweza kujifunza kwa kutembea pia, unajipa nafasi ya kuona mengi. unajifunza kwa kuuliza ili ufahamu, unajifunza pia kwa kuwafunza wengine. Na unajifunza zaidi kwa kusoma machapisho na hapa ndo kuna shinda. Ndiyo, ipo shida kwenye kusoma na kujisomea.

Ni ukweli kuwa maarifa unaweza kuyapata kwa kuangalia (observing) lakini ukijisomea vitabu na majarida/mitandao kama huu wetu basi nafasi ya kujifunza mengi ni kubwa kuliko kukaa bila kusoma. najua wapo tunaoogopa au hatupendi maneno (words) marefu. Binafsi navutiwa kusoma kama ni kitabu basi maneno yaliyokaa kama ushairi fulani hivi, mafupi mafupi sio marefu maana hunipa uoga wa maneno marefu kwa lugha nyingine ninaogopa maneno marefu (hippopotomonstrosesquippedaliophobia)

Kwako wewe mwanaKapuku, usichoke kujifunza na kutunza wengine maana unaupa ubongo wako furaha na kutuongezea maarifa wengine kila siku. Tukutane wiki ijayo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom