Makapuku Forum

Makapuku Forum

Tafasiri Unavyoweza: Kuishi Kinafiki Tatizo Letu Siasani

Mnafiki ni mtu ambaye anaishi na kutenda asivyo (pretense, au tumezoea kusema kupritend-kujifanya kuwa wakati sio). Kuishi kunatokana na neno maisha na kwa ufahamu usiotaka kutumia nguvu sana maisha ni siasa maana siku zote siasa ni ushawishi juu ya jambo au suala linaloshadadiwa na mtu au kikundi cha watu. Bahati mbaya sana, maisha yetu wengi tunayaishi kinafiki na mbaya zaidi wanasiasa wetu wamekuwa ni wanafiki zaidi sababu tumekaa kimya hatuwakosoi pale tunapoona unafiki umezidi. Tafasiri unavyoweza.

Tunawajua wanasiasa wengi ambao ni wanafiki kwa kiwango kikumbwa, yaani ni wale ambao wakifungua midomo yao huwezi kuamini chochote kinachotoka. wanasema hili huku wakimaanisha kitu kingine kabisa na wakiulizwa kesho wanabadili maneno na kuanza kuwapa majina wanaohoji kuwa si wazalendo. Mtawala kwa sababu ya unafiki wa maneno na matendo, kila siku anakuja na unafiki mpya kuficha unafiki wa jana na mbaya zaidi kwa kujua/makusudi wafuasi wa chama chake wanakuwa nyuma kutetea unafiki huu. Wanatetea maslahi si tu ya mtawala bali chama chao na hii inatokea kwa wanasiasa wote, walio madarakani na wanaosubiri nafasi ya kushika madaraka.

Mnafiki ni mtu mbaya, mnafiki anafitini na kufitini ni kutaka kugombanisha wananchi na hii si hulka tunayoitegemea kwa mwanasiasa au awaye yeyote. Ninajua kabisa ukweli una gharama na wakati mwingine ni gharama ya damu. Ifikie wakati tukae pembeni ya wanasiasa wanafiki ambao wanaamini unafiki wao hatuujui. Taifa makini ni la watu wanaohoji na si wanaokaa na kukubali kila kinachosemwa na wanasiasa
 
Muziki: Ramadhani Kareem

Ninakusalimia Kapuku mwenzangu na kukupongeza kwa kuweza kufika hapa na kulifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo mara zote. Najua kabisa kwa wengine wameanza mfungo leo, huu ni mwezi wa hisani (kareem maana yake genorous), na hakuna maana kama utaamua leo kuishi kama jana wakati kuna kesho. Nikutakie funga njema wewe unayefunga, funga yako ni siri yako na unayemwamini sio kukaa umepauka midomo na mdomo kunuka kisa umefunga, haifai.

Muziki sasa, ni jambo zuri kukuona anko wangu na wadau wote wa Makapuku, asanteni sana na niwatakie wakati mzuri.

 
Tafasiri Unavyoweza: Kuishi Kinafiki Tatizo Letu Siasani

Mnafiki ni mtu ambaye anaishi na kutenda asivyo (pretense, au tumezoea kusema kupritend-kujifanya kuwa wakati sio). Kuishi kunatokana na neno maisha na kwa ufahamu usiotaka kutumia nguvu sana maisha ni siasa maana siku zote siasa ni ushawishi juu ya jambo au suala linaloshadadiwa na mtu au kikundi cha watu. Bahati mbaya sana, maisha yetu wengi tunayaishi kinafiki na mbaya zaidi wanasiasa wetu wamekuwa ni wanafiki zaidi sababu tumekaa kimya hatuwakosoi pale tunapoona unafiki umezidi. Tafasiri unavyoweza.

Tunawajua wanasiasa wengi ambao ni wanafiki kwa kiwango kikumbwa, yaani ni wale ambao wakifungua midomo yao huwezi kuamini chochote kinachotoka. wanasema hili huku wakimaanisha kitu kingine kabisa na wakiulizwa kesho wanabadili maneno na kuanza kuwapa majina wanaohoji kuwa si wazalendo. Mtawala kwa sababu ya unafiki wa maneno na matendo, kila siku anakuja na unafiki mpya kuficha unafiki wa jana na mbaya zaidi kwa kujua/makusudi wafuasi wa chama chake wanakuwa nyuma kutetea unafiki huu. Wanatetea maslahi si tu ya mtawala bali chama chao na hii inatokea kwa wanasiasa wote, walio madarakani na wanaosubiri nafasi ya kushika madaraka.

Mnafiki ni mtu mbaya, mnafiki anafitini na kufitini ni kutaka kugombanisha wananchi na hii si hulka tunayoitegemea kwa mwanasiasa au awaye yeyote. Ninajua kabisa ukweli una gharama na wakati mwingine ni gharama ya damu. Ifikie wakati tukae pembeni ya wanasiasa wanafiki ambao wanaamini unafiki wao hatuujui. Taifa makini ni la watu wanaohoji na si wanaokaa na kukubali kila kinachosemwa na wanasiasa
Binamu asante sana bora uishi na mchawi kuliko mnafiki mchawi akitaka kukuua anakuua tu mnafiki anakuchekea huku anakumaliza
 
Muziki: Ramadhani Kareem

Ninakusalimia Kapuku mwenzangu na kukupongeza kwa kuweza kufika hapa na kulifanya jukwaa hili kuwa sehemu nzuri kuwepo mara zote. Najua kabisa kwa wengine wameanza mfungo leo, huu ni mwezi wa hisani (kareem maana yake genorous), na hakuna maana kama utaamua leo kuishi kama jana wakati kuna kesho. Nikutakie funga njema wewe unayefunga, funga yako ni siri yako na unayemwamini sio kukaa umepauka midomo na mdomo kunuka kisa umefunga, haifai.

Muziki sasa, ni jambo zuri kukuona anko wangu na wadau wote wa Makapuku, asanteni sana na niwatakie wakati mzuri.

Asante sana binamu
 
Binamu asante sana bora uishi na mchawi kuliko mnafiki mchawi akitaka kukuua anakuua tu mnafiki anakuchekea huku anakumaliza


...tena anakuja na kukukumbatia na kukupigapiga mgongoni kana kwamba yuko pamoja na wewe kumbe
6a00d834515f9b69e2015435bc1a10970c-320wi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom