Tafsiri Unavyoweza: Tunza Mazingira
...nakumbuka kati ya masomo niliyokuwa nayaweza sana (sio kufaulu, ila kuhudhuria dakika zote class) mojawapo ilikuwa ni Jiografia, jingine lilikuwa ni somo la lugha ya Kiswahili. Hili nililipenda sema lenyewe halikunipenda kwa kuwa wenzangu wote na mimi tulikuwa tukifundishwa darasani, sisi nje tunaongea kilugha chetu. Ningeweza kufaulu sana na kufika mbali kama masomo yote yangefundishwa kwa kilugha changu ambacho nilikuwa nakimaster kama nyani porini.
Turudi kwenye mada ya kutafsiri unavyoweza, Jiografia, ilivutia kusoma. Mambo ya hali ya hewa, longityudo na latityudo, mito, maziwa, milima na mabonde, misitu na nyika, uoto wa asili na miamba. Nilipenda sana kwa kweli. Ilifikia hata tukaenda 'utalii' Serengeti na Ngorongoro-nilipiga picha lakini mkanda uliungua, hazikuwa zama za smartphone na dijital kamera. zilikuwa ni enzi za kwachaaa mara flashi myakaa kutahamaki umefumba macho na haina kudelete.
Mazingira yanabadilika sana, na hasa mabadiliko ya tabia nchi, mvua zinanyesha, mafuriko na joto linaongezeka. Nina hakika kuna maeneo mengi unayoyajua kuwa na msitu sasa yamekuwa jangwa. Hii pamoja na mambo mengine ya kijiografia yasipoangaliwa vizuri si salama kwa kizazi kijacho.
Tunapoharibu mazingira, tunaweza tusione matokeo yake leo lakini kwa kizazi kijacho kitahangaika na wakigundua ni sisi ndo tumewafanya waishi kwa ugumu basi watatembelea kaburi la kila mmoja, watalifukua na kuanza kuchapa viboko mifupa. labda tubadilike tuanze kuchomana moto tukifa, na kusubiria moto mwingine wa milele kama utabahatika kuukwepa. Tafasiri unavyoweza, nimekuandikia utunze mazingira, ukiyatunza yatakutunza, siuongo!