Obe
Platinum Member
- Dec 31, 2007
- 10,278
- 35,639
Tafsiri Unavyoweza: Ajira
...ajira inahusisna na kitendo cha kufanya kazi kwa ujira/malipo. Malipo/ujira yapo ya aina nyingi, fedha na ujuzi vikiwa ni moja ya malipo. Hakuna ubishi kuwa Tanzania kuna tatizo la ajira, tena likiwa kubwa miongoni mwa vijana. zipo takwimu zinazokadiria kuwa angalau watu 900,000 huingia mtaani kusaka ajira kila mwaka, wengi wao wakiwa ni vijana. Ninajiaminisha takwimu hizi zimeongezeka maana kuna uandikishaji mkubwa wa vijana shuleni na vyuoni.
Kufanya kazi ni haki ya kila mwenye uwezo wa kufanya kazi. shida inatokea pale mwenye uwezo huo wa kufanya kazi anapokosa hiyo kazi kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo, mtaji, ujuzi na miundombinu inayowezesha mtu kufanya kazi. Kukosa kazi si jambo zuri si tu kwa mtu anayekosa kazi bali pia kwa serikali na jamii kwa ujumla.
Kijana asiye na mwenye nguvu za kufanya kazi asiwe na kazi ni kama bomu la muda, saa yoyote linalipuka na kama lisipolipuka lenyewe basi kuna uwezekana rahisi wa kulipukishwa na yeyote mwenye nia ovu dhidi ya jamii anayoishi kijana huyu.
Zama za serikali kuwa mwajiri mkubwa nchini zimepita, tuko kwenye zama za serikali kuweka miundombinu ikiwemo sera kamilifu za kutatua tatizo la ajira nchini. Sekta binafsi ipewe kipaumbele ili iajiri wengi, hizi habari za cherahani nne ni kiwanda ni propaganda zisizo na mashiko.
Mtazamo wangu binafsi; sekta ya kilimo inaajiri wengi lakini haijapewa mkazo mkubwa nchini, bajeti iongezwe kama azimio la Maputo lilivyosema. Mwaka jana sekta ya kilimo ilitarajiwa kupanda kwa 2.9 asilimia lakini ilifikia asilimia 2.1 tu. Fedha haikupelekwa ilivyohitajika
Vyuo vya kati viimarishwe na kuwafikia wengi zaidi
Umeme uwepo wa uhakika sio huu ambao mvua ikinyesha tu umekatika
Kufanya kazi iwe ni imani inayoanzia nyumbani, kisha waajiri kuanzia wenye mikahawa wawape kipaumbele vijana katika kuwapatia kazi.
Hii ni mada yenye mambo mengi, lakini tafasiri unavyoweza, bila kuwapatia ujuzi vijana wetu, soko la ajira ni gumu kuliko maelezo.
...ajira inahusisna na kitendo cha kufanya kazi kwa ujira/malipo. Malipo/ujira yapo ya aina nyingi, fedha na ujuzi vikiwa ni moja ya malipo. Hakuna ubishi kuwa Tanzania kuna tatizo la ajira, tena likiwa kubwa miongoni mwa vijana. zipo takwimu zinazokadiria kuwa angalau watu 900,000 huingia mtaani kusaka ajira kila mwaka, wengi wao wakiwa ni vijana. Ninajiaminisha takwimu hizi zimeongezeka maana kuna uandikishaji mkubwa wa vijana shuleni na vyuoni.
Kufanya kazi ni haki ya kila mwenye uwezo wa kufanya kazi. shida inatokea pale mwenye uwezo huo wa kufanya kazi anapokosa hiyo kazi kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo, mtaji, ujuzi na miundombinu inayowezesha mtu kufanya kazi. Kukosa kazi si jambo zuri si tu kwa mtu anayekosa kazi bali pia kwa serikali na jamii kwa ujumla.
Kijana asiye na mwenye nguvu za kufanya kazi asiwe na kazi ni kama bomu la muda, saa yoyote linalipuka na kama lisipolipuka lenyewe basi kuna uwezekana rahisi wa kulipukishwa na yeyote mwenye nia ovu dhidi ya jamii anayoishi kijana huyu.
Zama za serikali kuwa mwajiri mkubwa nchini zimepita, tuko kwenye zama za serikali kuweka miundombinu ikiwemo sera kamilifu za kutatua tatizo la ajira nchini. Sekta binafsi ipewe kipaumbele ili iajiri wengi, hizi habari za cherahani nne ni kiwanda ni propaganda zisizo na mashiko.
Mtazamo wangu binafsi; sekta ya kilimo inaajiri wengi lakini haijapewa mkazo mkubwa nchini, bajeti iongezwe kama azimio la Maputo lilivyosema. Mwaka jana sekta ya kilimo ilitarajiwa kupanda kwa 2.9 asilimia lakini ilifikia asilimia 2.1 tu. Fedha haikupelekwa ilivyohitajika
Vyuo vya kati viimarishwe na kuwafikia wengi zaidi
Umeme uwepo wa uhakika sio huu ambao mvua ikinyesha tu umekatika
Kufanya kazi iwe ni imani inayoanzia nyumbani, kisha waajiri kuanzia wenye mikahawa wawape kipaumbele vijana katika kuwapatia kazi.
Hii ni mada yenye mambo mengi, lakini tafasiri unavyoweza, bila kuwapatia ujuzi vijana wetu, soko la ajira ni gumu kuliko maelezo.
ZEKARIA 2


