
TUOMBE:
Tunakushukuru Baba Mungu wa Mbinguni umetuamsha salama,wako wengi walitamani kuiona leo..hawajaweza.sisi ni nani Baba,mimi ni nani Mfalme wa Amani...Nakushukuru sana Baba mwema.
Umetulinda Usiku kucha kwa Upendo wako mkuu ,umetuepusha na hatari zote za mwili na za roho...
Ni siku nyingine Mpya ya Jumatano tarehe 13 Desemba 2017 ni kwa Neema Baba na Upendo Mkuu umetuchagua nasi ili kuuona Utukufu wako ooh Haleluya Asante Baba kwa yote unayotutendea
Tunaomba Roho Mtakatifu Ukae nasi Siku zote za maisha yetu
Tunakuomba Utulinde Utuongoze na Utubariki Mfalme wa Amani
Angalia Yatima, Wajane ,Wagane, Wafungwa na Waliokata tamaa, wapweke, wanaotafuta wenza , walioonewa, wanyonge, Wakutumaini wewe tu.
Tunaomba u ponye Wagonjwa majumbani na mahospitalini ponya dawa wanazotumia wabariki wanaowatunza wagonjwa na wazee wasipungukiwe Mfalme wa Amani wawe na Upendo na mshikamano
Baba kaa na familia zetu, Ndoa zetu, Wake, Waume, Watoto, Wasaidizi wa ndani, Majumbani, Ndugu, Jamaa na Marafiki wakutafute kwa bidii na wachukuliane mizigo kwa upendo maana kila mtu na mmoja wetu anapitia vita ngumu sana za kimwili na kiroho inua watu mbalimbali wa kumsaidia kila mmoja katika vita yake na tupe tumaini.
Baba tunaomba uwalinde watoto wetu wote wanaosoma na kuishi mbali nasi huko mashuleni na makazini waongoze Baba katika kila jambo uwe mlinzi wao na kiongozi wao na uwainue katika masomo yao na maisha yao kimwili na kiroho
Baba Ukawe dereva wa kila chombo cha Usafiri na kila Msafiri mfunike kwa Damu ya Yesu Majini Nchi kavu Angani tukawe salama Baba tunapotoka na tuendako ..
Ilinde nchi yetu Amani itawale,zuia ajali,machafuko na matatizo mbalimbali yanayosababisha maafa,nafunga roho zote za mauti,shetani ashindwe katika jina la Yesu Kristo
Bariki kazi za mikono yetu Ajira, kilimo, mifugo, uvuvi, Ujasiriamali, Biashara ,Huduma na Masomo ya kila mmoja wa watoto wako.
Baba Wabariki Watumishi wa Mungu katika huduma zao.
Wabariki viongozi wa Serikali wakutafute kwa bidii watende haki
Waangalie Wajawazito na wanaojifungua Baba yetu mwema ili kazi ya uumbaji uliyoikabidhi kwa kila mmoja iwe ya kukupendeza
Asante kwa kuwa Unatupenda sana sana na utatenda sawasawa na mapenzi yako
TUNAOMBA NA KUSHUKURU KATIKA JINA LA YESU MPATANISHI NA MWOKOZI WETU.
SIKU NJEMA
DAMU YA YESU ITUFUNIKE